Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Kumbe wakati Lema anachangisha pesa za Join The Chain, Wenje alikuwa bize na utalii?
Siku ya leo Godbless Lema akizungumza na wanahabari kuhusu a tuhuma zilizotolewa na Ezekia Wenje, Mgombea wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara na Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Victoria amesema:
"Mimi nilikuwa ninakesha kwenye mitandao ya kijamii kama Clubhouse kukusanya pesa kwa ajili ya Join the Chain, kwasababu Australia wakiamka inabidi niwe Clubhouse kuhamasisha, Australia wakilala na Japan wakiamka lazima niwe kwenye Clubhouse.
Huyu Wenje tulikuwa naye huko Canada labda kazi yake ilikuwa ni kupiga picha kwenye madaraja, kwasababu hajawahi kushughulika na kazi yoyote ya kimataifa ya kusaidia chama hiki.
"Ule mtandao nilioutengeneza wa kukusanya pesa ndani na nje ya nchi ukaanza kufanya kazi moja ya msingi sana, wakati Mwenyekiti Mbowe alipokuwa jela, ikabidi Tundu Lissu awe anasafirishwa kwenda Ujerumani na kwingine kuongea wahisani wa kimataifa kwa ajili ya kuweka shinikizo Mwenyekiti atoke gerezani
Lakini huyu Wenje nimesikia anasema kwamba hawa watu walikuwa wanakusanya pesa ya Join the Chain kumfanyia mapinduzi Lissu awe Mwenyekiti badala ya Mbowe. Kimsingi mtandao wetu ulimsaidia hata Lissu kuwezesha Mwenyekiti atoke"
Source: Jambo TV Online
Tazama pia: Ezekiel Wenje: Kuhusu zilipoenda pesa za Join The Chain muulizeni Godbless Lema. Yeye ndo alikuwa Mwenyekiti!
Kumbe wakati Lema anachangisha pesa za Join The Chain, Wenje alikuwa bize na utalii?
Siku ya leo Godbless Lema akizungumza na wanahabari kuhusu a tuhuma zilizotolewa na Ezekia Wenje, Mgombea wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara na Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Victoria amesema:
"Mimi nilikuwa ninakesha kwenye mitandao ya kijamii kama Clubhouse kukusanya pesa kwa ajili ya Join the Chain, kwasababu Australia wakiamka inabidi niwe Clubhouse kuhamasisha, Australia wakilala na Japan wakiamka lazima niwe kwenye Clubhouse.
Huyu Wenje tulikuwa naye huko Canada labda kazi yake ilikuwa ni kupiga picha kwenye madaraja, kwasababu hajawahi kushughulika na kazi yoyote ya kimataifa ya kusaidia chama hiki.
"Ule mtandao nilioutengeneza wa kukusanya pesa ndani na nje ya nchi ukaanza kufanya kazi moja ya msingi sana, wakati Mwenyekiti Mbowe alipokuwa jela, ikabidi Tundu Lissu awe anasafirishwa kwenda Ujerumani na kwingine kuongea wahisani wa kimataifa kwa ajili ya kuweka shinikizo Mwenyekiti atoke gerezani
Lakini huyu Wenje nimesikia anasema kwamba hawa watu walikuwa wanakusanya pesa ya Join the Chain kumfanyia mapinduzi Lissu awe Mwenyekiti badala ya Mbowe. Kimsingi mtandao wetu ulimsaidia hata Lissu kuwezesha Mwenyekiti atoke"
Tazama pia: Ezekiel Wenje: Kuhusu zilipoenda pesa za Join The Chain muulizeni Godbless Lema. Yeye ndo alikuwa Mwenyekiti!