Golden State Warriors yatwaa Ubingwa wa NBA kwa kuifunga Boston Celtics

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Golden State Warriors imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Kikapu ya NBA 2022 ikiwa ni mara ya nne ndani ya miaka nane iliyopita.

Imeifunga Boston Celtics kwa vikapu 103-90 katika mchezo wa Fainali ya 6 uliomalizika alfajiri ya leo Juni 17, 2022.

Stephen Curry amebeba Tuzo ya Mchezaji Bora wa Fainali (MVP) ambapo timu yake ya Warriors imeshinda kwa jumla ya mechi 4-2.





 
Dub nation wako on fire, wali'deserve asee..Klay Thompson karudi vizuri toka injury na timu inacheza kwa ushirikiano sana,kina Jordan Poole,Draymond Green,Wiggins wako fit sana..Nilijua2 Chef Curry game5 alikosa 3Points 9 bac game6 ataua mtu
 
Watakuwa majini hawa, kila final wanabeba
 
celtic this was their year ila sasa wamkutana na kale kajamaa 30curry
 
KD alijua katengeneza ufalme, kaondoka lkn GSW wanachukua tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…