Goma: Raia waandamana kupinga uwepo wa MONUSCO na majeshi ya nje

Goma: Raia waandamana kupinga uwepo wa MONUSCO na majeshi ya nje

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
350
Reaction score
576
Leo hii, tarehe 17 Februari 2025, mjini Goma, asubuhi ya leo kumekuwa na maandamano; lengo likiwa wanajeshi wa UN waliopo Congo,hususani Goma, kwa zaidi ya miaka 20, waondoke, na kwamba usalama wao watahakikisha unatokana na wao wenyewe.
Si MOUNUSCO tu, bali na jeshi la SAMIDRC(Afrika kusini, Malawi na Tanzania). Jeshi la Burundi pia, limeombwa kufanya kila linalowezekana liondoke.

Raia hawa, wameiomba pia MONUSCO kuhakikisha wanajeshi waliokimbia vita na kupewa hifadhi kambini mwao, baada ya wenzao kujisalimisha na kupokelewa na M23, kuwaachia waliobaki na wao kuungana na wenzao, ambao kwa sasa wapo mafunzoni, kwenye kambi ya jeshi ya Rumangabo.

Wamesema,hawana imani na MONUSCO, kwa kitendo ilichofanya siku za nyuma,cha kuachia badhi yao wakiwemo wapiganaji wa kikundi cha FDLR, ili wavuruge amani mjini, huenda ikaachia na wengine tena.

Baada ya Goma kuangukia mikononi mwa M23, January 27, kwa sasa raia wanadai bora kuliko walivyokuwa wakiishi awali, na kutangaza kwamba, kwa sasa, wamehimizwa kuacha pombe kabla ya saa sita na kuwataka wafanye kazi, na wahalifu wakishughulikiwa bila huruma, jambo ambalo wanasema limegeuza hali ya usalama mjini humo, kuwa ya uhakika.
 
jeshi la SADC(Afrika kusini, Malawi na Tanzania).

Jeshi la ukanda la SAMIDRC, limpewa majukumu (mandate) :

1739801655803.jpeg

SAMIDRC mission yake kwa niaba ya SADC yaani Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika katika limepelekwa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa misheni ya kijeshi ya kulinda amani wa kikanda huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. SAMIDRC wameipa jina Operesheni Thiba inajumuisha wanajeshi kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi.

TOKA MAKTABA MWAKA 2024 :

17 Mei 2024

KAMANDA WA KIKOSI CHA SAMIDRC azungumza kuhusu Ujumbe nchini DRC



View: https://m.youtube.com/watch?v=8FwYjttdhVo
Kamanda anasema SADC ina wasiwasi kuhusu kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia yanayofanywa na vikosi hasi na makundi haramu yenye silaha Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mashambulizi hayo yamesababisha idadi kubwa ya watu kuhama makazi yao, na kuziba njia za usambazaji bidhaa kwenda Goma na kuzidisha hali ya kibinadamu.

Wakati huo huo, barabara kuu za kwenda Goma ambazo ni muhimu kwa usafirishaji wa raia, bidhaa na misaada ya kibinadamu zimekuwa hazipitiki kutokana na ukatili usio na huruma na wa kuchukiza wa makundi yenye silaha, na hivyo kuwazuia zaidi watu kupata huduma na vifaa muhimu.


Kwa mujibu wa Mamlaka ya SAMIDRC, kwa ushirikiano na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC), SAMIDRC itafanya oparesheni kupunguza vikosi hasi na vikundi haramu vyenye silaha Mashariki mwa DRC ili kurejesha na kudumisha amani na usalama ili kuweka mazingira salama pamoja na kulinda raia na mali zao chini ya vitisho au mashambulio yanayokaribia.

Operesheni hizo zinanuia kufungua njia za usambazaji bidhaa na kuhakikisha kuwa raia wako huru kutokana na vitisho, kufurushwa na mauaji ili jamii ziweze kuendesha maisha yao ya kila siku bila kuingiliwa au vitisho vyovyote
 


Unaelewa lugha hiyo?
Wakazi wa Goma waliomba MONUSCO, jeshi la Burundi na SADC kuondoka DRC

Wakazi wa mji wa Goma waliandamana asubuhi ya Februari 17, 2025 wakitaka wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani (MONUSCO), Burundi na Jumuiya ya Afrika Kusini (SAMIDRC) kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waondolewe.

Wakaazi hawa walisema kuwa wanajeshi katika vituo vya MONUSCO nchini DRC wanaweza kutishia usalama wao, hivyo wanapaswa kuondoka na kuwakabidhi kwa wapiganaji wa kundi la waasi la M23 ili kuwalinda.

Walisema, “Askari wa FARDC katika vituo vya MONUSCO wanaweza kutishia usalama wetu. Tunawaomba waondoke kwenye taasisi hizi na wanyooshe mikono ili tuwe na amani."

Wakongo waliendelea kusema, "Jambo lingine tunalouliza ni kwamba askari wa SAMIDRC, Burundi na MONUSCO warudi nyumbani. Tutatua tatizo letu kama watu wa Kongo.

Ujumbe mwingine waliokuwa nao ni kwamba Rais Félix Tshisekedi wa RDC hana uwezo wa kulinda usalama wao, hivyo anapaswa kuachia ngazi.

Wapiganaji wa kundi lenye silaha la M23 wanadhibiti mji wa Goma tangu Januari 27, 2025. Wale walio katika muungano wa RDC wamekimbilia vituo vya MONUSCO tangu siku hiyo, huku wengine wakishuka hadi Kivu Kusini. Pia kuna wakimbizi nchini Rwanda.

M23 hivi majuzi ilitangaza kuwa baadhi ya wanajeshi wa RDC waliruhusiwa kuondoka katika kambi ya MONUSCO, pamoja na magaidi wa FDLR, ili kuvuruga usalama wa Goma. Wawili kati yao walikamatwa
 
Wakazi wa Goma waliomba MONUSCO, jeshi la Burundi na SADC kuondoka DRC

Wakazi wa mji wa Goma waliandamana asubuhi ya Februari 17, 2025 wakitaka wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani (MONUSCO), Burundi na Jumuiya ya Afrika Kusini (SAMIDRC) kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waondolewe.

Wakaazi hawa walisema kuwa wanajeshi katika vituo vya MONUSCO nchini DRC wanaweza kutishia usalama wao, hivyo wanapaswa kuondoka na kuwakabidhi kwa wapiganaji wa kundi la waasi la M23 ili kuwalinda.

Walisema, “Askari wa FARDC katika vituo vya MONUSCO wanaweza kutishia usalama wetu. Tunawaomba waondoke kwenye taasisi hizi na wanyooshe mikono ili tuwe na amani."

Wakongo waliendelea kusema, "Jambo lingine tunalouliza ni kwamba askari wa SAMIDRC, Burundi na MONUSCO warudi nyumbani. Tutatua tatizo letu kama watu wa Kongo.

Ujumbe mwingine waliokuwa nao ni kwamba Rais Félix Tshisekedi wa RDC hana uwezo wa kulinda usalama wao, hivyo anapaswa kuachia ngazi.

Wapiganaji wa kundi lenye silaha la M23 wanadhibiti mji wa Goma tangu Januari 27, 2025. Wale walio katika muungano wa RDC wamekimbilia vituo vya MONUSCO tangu siku hiyo, huku wengine wakishuka hadi Kivu Kusini. Pia kuna wakimbizi nchini Rwanda.

M23 hivi majuzi ilitangaza kuwa baadhi ya wanajeshi wa RDC waliruhusiwa kuondoka katika kambi ya MONUSCO, pamoja na magaidi wa FDLR, ili kuvuruga usalama wa Goma. Wawili kati yao walikamatwa
Watano. siyo wawili
 
Wazalendo Cannibals waliokamatwa na M23 wengi wao ni FDLR.
 
Leo hii, tarehe 17 Februari 2025, mjini Goma, asubuhi ya leo kumekuwa na maandamano; lengo likiwa wanajeshi wa UN waliopo Congo,hususani Goma, kwa zaidi ya miaka 20, waondoke, na kwamba usalama wao watahakikisha unatokana na wao wenyewe.
Si MOUNUSCO tu, bali na jeshi la SAMIDRC(Afrika kusini, Malawi na Tanzania). Jeshi la Burundi pia, limeombwa kufanya kila linalowezekana liondoke.

Raia hawa, wameiomba pia MONUSCO kuhakikisha wanajeshi waliokimbia vita na kupewa hifadhi kambini mwao, baada ya wenzao kujisalimisha na kupokelewa na M23, kuwaachia waliobaki na wao kuungana na wenzao, ambao kwa sasa wapo mafunzoni, kwenye kambi ya jeshi ya Rumangabo.

Wamesema,hawana imani na MONUSCO, kwa kitendo ilichofanya siku za nyuma,cha kuachia badhi yao wakiwemo wapiganaji wa kikundi cha FDLR, ili wavuruge amani mjini, huenda ikaachia na wengine tena.

Baada ya Goma kuangukia mikononi mwa M23, January 27, kwa sasa raia wanadai bora kuliko walivyokuwa wakiishi awali, na kutangaza kwamba, kwa sasa, wamehimizwa kuacha pombe kabla ya saa sita na kuwataka wafanye kazi, na wahalifu wakishughulikiwa bila huruma, jambo ambalo wanasema limegeuza hali ya usalama mjini humo, kuwa ya uhakika.
Hatare

Wananchi wameamua
 
Back
Top Bottom