Google Doodle wameuweka Mlima Kilimanjaro leo

Google Doodle wameuweka Mlima Kilimanjaro leo

singojr

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2014
Posts
5,313
Reaction score
6,895
Leo kama ilivyokatika miaka yote ni siku ya Dunia. Huwa siku hii inaadhimishwa kwa kujadiliana namna gani tunaweza kuifanya dunia iendelee kuwa sehemu salama ya kuishi. Changamoto zote na namna ya kuzitatua kufuatia mabadiliko ya tabia nchi.

Nimefarijika kuona mlima Kilimanjaro leo utafahamiaka kwa watumia google kote duniani, japo kuwa leo utafahamika zaidi kwa jinsi tulivyoshindwa kuutunza.

Picha inayoonekana leo ni ulinganifu wa kiwango cha barafu kwa miaka tofauti kwa mwezi Dec kutokea mwaka 1986-2020. Picha hiyo ikionyesha kuwa barafu imepungua kwa asilimia kubwa.

Kama taifa tunapitia mambo mengi ya kimazingira na utunzaji wa uoto wa asili. Picha hii imenifanya niwaze kuhusu sakata la Ngorongoro. Ni kiasi gani shughuli za kibinadamu katika eneo lile zinavyoadhiri maisha ya wanyama na uoto wa asili?

Je, tusubiri baada ya miaka ishirini tuwekewe picha ya jinsi Ngorongoro ilivyokuwa hapo kabla na jinsi itakavyokuwa? Pakiwa na ng'ombe na mbuzi badala ya nyumbu na swala?

Picha hii itupe funzo la namna gani tusipokuwa makini kizazi kijacho kitakosa fursa za kiuchumi kwa kutoweka kwa vivutio mbalimbali

1650606450563.png
 
Leo kama ilivyokatika miaka yote ni siku ya Dunia. Huwa siku hii inaadhimishwa kwa kujadiliana namna gani tunaweza kuifanya dunia iendelee kuwa sehemu salama ya kuishi. Changamoto zote na namna ya kuzitatua kufuatia mabadiliko ya tabia nchi.
Nimefarijika kuona mlima Kilimanjaro leo utafahamiaka kwa watumia google kote duniani, japo kuwa leo utafahamika zaidi kwa jinsi tulivyoshindwa kuutunza.
Picha inayoonekana leo ni ulinganifu wa kiwango cha barafu kwa miaka tofauti kwa mwezi Dec kutokea mwaka 1986-2020. Picha hiyo ikionyesha kuwa barafu imepungua kwa asilimia kubwa.
Kama taifa tunapitia mambo mengi ya kimazingira na utunzaji wa uoto wa asili. Picha hii imenifanya niwaze kuhusu sakata la Ngorongoro. Ni kiasi gani shughuli za kibinadamu katika eneo lile zinavyoadhiri maisha ya wanyama na uoto wa asili?
Je, tusubiri baada ya miaka ishirini tuwekewe picha ya jinsi Ngorongoro ilivyokuwa hapo kabla na jinsi itakavyokuwa? Pakiwa na ng'ombe na mbuzi badala ya nyumbu na swala?
Picha hii itupe funzo la namna gani tusipokuwa makini kizazi kijacho kitakosa fursa za kiuchumi kwa kutoweka kwa vivutio mbalimbali

View attachment 2196134
Loyal Tour....
 
Changamoto za kimazingira ni za kidunia. Kama nchi sijui ninkitu gani kitafanyika ili kulinda hadhi ya mlima kilimanjaro
 
shughuli za Kibidadamu zimeongezeka kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya watu.

Enzi hizo eneo kubwa lililokaribu na mlima lilikua pori lenye uoto wa asili, kwasasa ni mashamba ya mazao na miti ya mbao ambayo huvunwa baada ya muda.

ni changamoto kama ilivyo kwa ngorongoro.
 
Jinsi technology inavyo ongezeka na na effect zinaongezeka ndio maana mpaka wali fikilia kuanza kupanda kwa kutumia viberenge je mazingira ya mlima Kilimanjaro yata endelea kuwa salama?
 
Changamoto za kimazingira ni za kidunia. Kama nchi sijui ninkitu gani kitafanyika ili kulinda hadhi ya mlima kilimanjaro

Ni kucontrol shughuli za kibinadamu kuzunguka mlima
 
shughuli za Kibidadamu zimeongezeka kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya watu.

Enzi hizo eneo kubwa lililokaribu na mlima lilikua pori lenye uoto wa asili, kwasasa ni mashamba ya mazao na miti ya mbao ambayo huvunwa baada ya muda.

ni changamoto kama ilivyo kwa ngorongoro.

Kwanini pasiwe na control mbona shughuli zimeongezeka lakini eneo la Ikulu halijapungua toka mwaka 1961
 
U can't fight natural forces. Over the years, dunia imepitia vipindi vya baridi kali (ice ages) na vipindi vya joto kali.

Barafu unayoina sasa hasa south na north pole ni masalia ya kipindi cha mwisho cha ice age kilichoisha almost 10k years ago. Sasa tunaelekea kipindi cha joto kali.

Binadamu na viumbe wengine wakifa kwa joto other organisms will evolve and take their place. Nature has its way of keeping balance of things and there is nothing you can do to get in its way.
 
Hapo inabidi tuwahamishe wachaga wapelekwe mbeya au mtwara maana wanaharibu sana mazingira.
 
Sisi watanzania tunafaidika na nini hapo mkuu.
 
Asee CM 1774858 Mama kafanya jambo huko mpaka mlima umewekwa google!.

Tuendelee kumuunga mkono 🤗!.
 
jukumu la kuulinda mlima Kilimanjaro nila dunia nzima ,zaidi watz wenyewe .nadhani pia tupo kwenye mpango wa dunia wa mazingira ,Kuna haja hata wao wawe wakari ktk utunzaji wa mazingira hasa kwa maeneo ambayo ni wonders of the world.sio Kilimanjaro tu hata Everest,elgon.n.k
 
Back
Top Bottom