google haifai!!

Dangote

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2012
Posts
204
Reaction score
76
Kamati ya bunge la uingereza imebainisha kua kati ya mwaka 2006 hadi 2011 kampuni ya google ilitengeneza faida ya $18 billion kwenye biashara zake ndani ya uingereza lakini ndani ya kipindi hicho walilipa corporate tax kiasi cha $16 million tu.huu ni ukwepaji mkubwa wa kodi kuwahi kutokea ndani ya taifa hilo inadaiwa pia kampuni zingine zinazoshutumiwa ni pamoja na amazon.com,starbucks na apple.

Note:kama wanaweza kukwepa hivi kwenye nchi zilizoendelea na zenye taasisi imara pamoja na utawala bora inakuwaje kwenye nchi zetu huku zilizojaa rushwa na taasisi zisizokua imara sana.research 1 inadai katika kila $2 inayokuja africa kama msaada kutoka mataifa yaliyoendelea $8 inaondoka africa kwenda nchi hizo kama pesa ambazo hazijalipiwa kodi kutoka na faida makampuni hayo makubwa ya kimataifa yameyapata kwa kufanya biashara ndani ya africa wanatorosha fedha hizi kwenda mabank yao huko kwenye tax heavens na switzerland.do africa need aid or fair share of its taxes?
 
mkuu there is no free lunch in this world, labda kule Mars!
 
Yap mkuu itabidi viongozi wetu wakomalie haya makampuni makubwa sio kutukamua tu sie masikini kwenye viline vyetu vya simu na wajue misaada inatuathiri kuliko kutufaidisha
 
wewe inakuhusu, walipe kodi wasilipe wanakupunguzia nini?
 
Tax avoidance is unavoidable!
 
wewe inakuhusu, walipe kodi wasilipe wanakupunguzia nini?
UK hapo imetumika kama mfano tu kumbuka hata hapa tz google wanafanya biashara so ni wajibu kulipa kodi kama mimi na wewe tunavyolipa iwe income tax au vat.
 
The hardest thing to understand in this world is the income tax-albert einsten@zinedine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…