π—šπ—’π—’π—šπ—Ÿπ—˜ 𝗠𝗔𝗣 π—œπ— π—˜π—¨π—” π—ͺ𝗔𝗧𝗨 π—ͺ𝗔𝗧𝗔𝗧𝗨

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
π—šπ—’π—’π—šπ—Ÿπ—˜ 𝗠𝗔𝗣 π—œπ— π—˜π—¨π—” π—ͺ𝗔𝗧𝗨 π—ͺ𝗔𝗧𝗔𝗧𝗨



Watu watatu wamepoteza maisha baada ya gari walilokuwa wamepanda kupata Ajali, walipokatiza katika Eneo ambalo barabara haijakamilika huko nchini India.

Google maps imewadanganya watu watatu na kupelekea kufa baada ya gari walilokuwa wamepanda kupotea njia na kuanguka kwenye Eneo ambalo daraja halijakamilika kwenye mto wa Ramganga nchini India.



Daraja Hilo lilikua limevunjika kipindi Cha mafuriko. Miezi kadhaa iliyopita, wanaume hao watatu walikua wanasafiri usiku kuelekea mjini ambapo hawakuona kama Daraja limekatika maana kwenye Google maps imeonyesha daraja Liko vyema ndipo walipoanguka kwenye mto na kupelekea kufa.



Familia za waathilika, zinataka mamlaka husika kuwajibika maana hawakuweka Alama yoyote kuhashiria Kuna tatizo na uchunguzi uliofanywa unaonyesha wahusika walitumia Google maps wakati wanapata Ajali.

Nani wa kuwajibika Google maps au Serikali ?πŸ₯±

#bongotech255
 
Mamlaka za Kwao ndio zina makosa hapo kwa kutoweka signs za Kuonesha daraja Ni Bovu, Google hahusiki mkuu, Afu google pia most of data mle za Kama road Closure au Congestion tuna update sisi sisi Users
 
Kikawaida Google inakupitisha mahala ambapo watu wengi wanapita kwa wakati huo. Ilikuwaje akapewa njia ambayo watu hawapiti.

Hata hivyo njia zenyemarekebisho hufungwa na mamlaka husika
 
Mamlaka za Kwao ndio zina makosa hapo kwa kutoweka signs za Kuonesha daraja Ni Bovu, Google hahusiki mkuu, Afu google pia most of data mle za Kama road Closure au Congestion tuna update sisi sisi Users
Wote wana sehemu ya lawama.

Serikali ina wajibu mkubwa zaidi kuweka physical barrier, barabara ifungwe zaidi ya mita 100 kabla ya daraja.

Pili, serikali iliwajibika kuiarifu Google i update maps haraka sana.

Tatu, Google wanaweza kuweka system ya ku scan madaraja periodically kwa muda mzuri zaidi ili kupata taarifa sahihi zaidi.
 
Google map haijaua ila wahusika kutokuwa makini, daraja mbele halipo lazima kulikuwa na alama za barabarani
 
Siku hizi naona wanaweka tahadhari,Juzi kati baada ya jengo la kariakoo kudondoka nilikua nataka niende mitaa hiyo nikacheki googlemaps ikanipa warning kuhusu hiyo ajali iliyotokea
 
Google map imewauwaje sasa. Bora hata useme serikali ya india kwa kushindwa kuifunga barabara inayojua daraja linevunjika. Pia unaweza mlaumu dreva Kawa uwa wenzake kwa kukosa umakini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…