Graduates shitukeni mapema hali sio nzuri

Meja mstaafu

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2017
Posts
531
Reaction score
1,121
Habari zenu ndugu zangu,

Katika tafiti zangu zisizo rasmi, nimegundua kizazi kinacholalamika kuhusu ajira, naongelea degree holders ni waliomaliza kidato cha nne mwaka 2010 na kurudi chini. Na ukiangalia kwa kina kipindi hicho ufaulu wa kidato cha nne ulikuwa ni chini ya asilimia 11. But kuanzia miaka ya 2013 BRN ilipoanzishwa kumekuwa na ufauru mkubwa sana wa kidato cha nne na kuendelea.

Hivyo basi kaa ukijua wasomi wanaongezeka kwa kasi sana na hakuna haja ya kulalamika kwamba serikali haitoi ajira, manake hata ikitoa bado hazitoshi na kupata ni probability. Hivyo basi ndugu zanguni tuanze kutumia elimu zetu na utashi tulio nao katika kutumia fursa zinazotuzunguka kama kilimo, ujasiriamali ili kujiletea maendeleo.

AHSANTENI.
 
Umeongea ukweli mchungu ambao wengi wataitazama hii thread na kupuuza ila huu ndio ukweli na ni halisi kwa sasa. Batch zaidi ya mbili zipo mtaani ila bado mtu haelewi anapoambiwa tumia fursa ndogo za kilimo n.k uanze utekelezaji wa hatua za kujiajiri mwenyewe. mfano hata bustani za mboga n.k
MWENYE MASIKIO NA ASIKIE NA MWENYE MACHO AONE.
 
Hiyo 2013 walifeli mpaka serikali iliingilia na kuyarekebisha matokeo yao.
 
Ufauru>>>UFAULU
Maake>>>Maana yake


Asante kwa taarifa, wamekupata wahusika
 
elimu bado si rafiki kwa mtanzania jaman toka unaanza kozi mpaka unamaliza huongozwi kujitegemea au swali rahisi kuna maprof wangapi waliojiajiri au masters holder wenye uwezo wa kumiliki gari au nyumba ya milion thelathin elimu yetu ipo midomon na kwenye vitabu hii nikutokana na nchi kupuuza vipaji vya watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili pia nakumbuka kauli*you can't solve the problem with the same level of thinking which created them*
 
Huko kwenye kilimo na biashara ya mazao! Nimeshakula risasi nyingi kuliko alizopigwa Lisu... Loss niliyopata huko, hapa niko ICU. Maumivu niliyoyapata ni zaidi ya kupigwa risasi 28!
 

Kujiajiri watu hawshindwi ila watoa maamuzi wanatuangusha sana, mfano mie nililima nafaka nakilenga soko la North Kenya hadi Sudan Kusini!! Watoa maamuzi wanapiga marufuku kusafirisha nafaka nje ya nchi na ndani soko bovu sana, aagh!! Inakera sana, wanatuangusha kwa kweli
 
Ni kweli ndugu yangu, hata Mimi mwaka Jana nililima viazi lishe heka tano , na soko lake kubwa kwa huku kwetu huwa ni Kenya. Afu eti sijui kiongozi uchwara akapiga marufuku kuuza mazao nje ya nchi. Kiukweli inauma sana Ila ndio hivyo tusikate tamaa.
 
nakuunga mkono
 
Njooni mikoani Kuna fursa nyingi sana musi ng'ang'anie Dar es salaam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…