graduation za nursery school nazo zinachangamoto yake!

evangelical

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2011
Posts
5,035
Reaction score
8,218
Maisha ya siku hizi kweli ni changamoto,
Kid wa nusery ameleta letter kutoka school, inayomtaka mzazi achangie elfu 20 za kufanya sherehe
y kumaliza nusery (graduation). mtoto asiyechanga haudhurii sherehe.
Mzazi wa kiume ni mshkaji wangu analalamika hali ya kifedha sio nzuri, anapendekeza mtoto asihudhurie sherehe.
mama mtoto haelewi analazimisha ichangwe mtoto akasherehekee na wenzake graduation yao.
Nimemshauri mshkaji wangu aachane na huo, mchango kama fedha hairuhusu.
Nusery school yenyewe, ni haya madarasa ya awali ya shule za msingi za Serikali, ipo town,
siyo internationa school, mshaji wangu mwenyewe ni dereva tax wa kuajiriwa.
Kutokana na hali za uchumi za wa tz wengi kuwa duni, ni ngumu sana kwa wao kufanya vitu kama hivi vya
kusherehekea graduation za watoto wao wanapomaliza chekechea, ingawaje ni jambo zuri kijamii
 
...Nursery School yenyewe ni Madarasa ya Awali ya Shule za Serikali, ipo Town, siyo International School. Mshikaji wangu ni Dereva Taxi wa kuajiriwa...." Ninadhani Mshikaji wako, hata kama ni Dereva Taxi wa kuajiriwa, amekosea kuomba ushauri wa suala hili kutoka kwako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…