Grow and fly big books series (Utangulizi, Sehemu ya 1&2)

Grow and fly big books series (Utangulizi, Sehemu ya 1&2)

Thomas Lazaro

Member
Joined
Jul 28, 2020
Posts
5
Reaction score
1
UTANGULIZI

Kutokana na kukua kwa tatizo kubwa la ajira miongoni mwa vijana na familia nyingi duniani, imepelekea watu kuchanganyikiwa ni nini cha kufanya. Watu wote siku hizi wanahaha kutafuta ajira ambayo imekua adimu sana na hivyo kuwafanya watu ambao akili zao na mawazo yao yameelekezwa kwenye kuajiriwa kupata msongo wa mawazo na hata kupata matatizo ya kiafya inayosababishwa na stress

Miongoni mwa waathirika wakubwa wa tatizo hili la ajira ni pamoja na wahitimu wa shule na vyuo mbali mbali duniani. Tatizo la ajira ni janga la kimataifa katika kizazi cha sasa kwani wanafunzi mashuleni na vyuoni wameandaliwa kuwa waajiriwa badala ya kuwa watengeneza ajira

Kitabu hiki kimelenga kuwafungua watu kutoka kwenye kifungo cha ajira kama njia pekee ya kupata kipato na inafundisha mbinu na njia nyingine ya kupata kipato ya kuanzisha biashara na uwekezaji

Pia kitabu hiki kimelenga kuwaandaa matajiri wakubwa ambao watakuwa waandaa ajira kwa watu wengine. Niamini baada ya kukisoma kitabu hiki na kuweka ulichojifunza kwenye matendo hakika utaishi kujua njia nyingine mpya ambayo ndio chanzo kikubwa cha utajiri na utakuwa suluhisho la ajira kwa wengine pia.

Elimu na ufahamu utakao upata kwenye kitabu hiki utakufanya ugundue kuwa utajiri unao wewe mwenyewe kwenye mikono yako na wala hauitaji kuwa na mtaji mkubwa sana kuanza biashara na uwekezaji utakao kufanya kuwa tajiri. Vile vile kwa wale ambao wameajiriwa watajikuta wanaanza kupata njia sahihi ya kuwa tajiri badala ya kutegemea njia moja ya ajira kuwa chanzo pekee cha kupata kipato.

Waajiriwa watagundua pia kuwa ajira ni sehemu ya kujifunzia kufanya kazi za uwekezaji na biashara. Badala ya kugombana na mabosi wao kila mara kuhusu kuongezewa mishara, kutegemea promotion za kazini, kufanya ufisadi na rushwa kama njia ya kujiongezea kipato, watajifunza kujiongezea mishahara na kujipa promotion wao wenyewe kupitia biashara na uwekezaji wao wenyewe.

Miongoni mwa chanzo cha kupotea kwa ajira nyingi duniani ni pamoja na kukua kwa sayansi na teknolojia ambayo kwa upande mwingine ungeweza kutumika kuwa jukwaa zuri la kutatua tatizo la ajira. Ebu jiulize; je unajua fursa zinazopatikana kutokana na uwepo wa sayansi na teknolojia ikiwa ni pamoja na ukuaji wa mitandao ya kijamii?

Je, huwa unaitumiaje mitandao ya kijamii, kwa kuchati au, kwa kutangaza biashara yako?

Mitandaoni kuna fursa nyingi ambazo hazijawahi kuwapo na ni fursa kwa watu wote bila upendeleo wala ubaguzi wa kipato hata kama hauna kipato kabisa unaweza kuanza biashara kupitia mtandao na ukawa tajiri. Ebu endelea kujifunza kupitia kitabu hiki.

MAFUNZO ONLINE.jpg
 
Kitabu hicho kinatoa na mitaji? Maana hiyo ndio ajenda kuu ya vijana wasio na ajira.
 
Kitabu hicho kinatoa na mitaji? Maana hiyo ndio ajenda kuu ya vijana wasio na ajira.
mtaji wa kwanza ni elimu juu ya fedha maana unaweza kupata fedha alafu bado ukashindwa kutoka kimaisha vile vile. you better invest in education first and the money will be following the course
 

swahili front PAGE..jpg

SEHEMU YA KWANZA

SURA YA KWANZA

ANZISHA, SIMAMIA NA KUENDELEZA BIASHARA YAKO

MAANA YA BIASHARA

Biashara; Ni shughuli yoyote inayofanywa kwa makusudi ya kupata faida, inaweza kuwa uuzaji wa bidhaa, au uuzaji wa huduma. Mfano wa bidhaa ni kama magari, simu, nguo, vyakula, nk huduma; ni kama shule, huduma za kifedha, huduma za kiafya, dalali, uuzaji wa huduma za mitandao, nk.

NGUZO ZA MSINGI ZA KUANZA BIASHARA

Kuanza biashara kunatokana na maono tofauti, na mahitaji ya kikundi fulani cha watu wanaotaka huduma au bidhaa fulani. Ili Kuanza biashara zingatia kanuni zifuatazo;-

Wazo la biashara; Fikiria wazo la biashara unayopenda na ulio na shauku nayo ambayo unaweza kupitia maisha yako kujenga mfumo bora wa biashara. Wazo linaweza kutoka kwenye vyanzo tofauti kama vile;- kutoka kwako mwenyewe marafiki, wafanyakazi wenzako mahitaji ya watu au jamii Fulani n.k.

Soko; Tambua watumiaji wako kwa idadi, kwa umri, na kwa kiwango cha uchumi ambao unatarajia kuwauzia bidhaa au huduma hiyo; hii itatoa kidokezo cha bidhaa gani na yenye ubora gani wanayohitaji.

Eneo; Unapaswa kujua ni eneo gani waliko wateja wako. Hii inafafanua ni wapi unataka kuanzisha biashara yako, njia gani ya usambazaji na usafirishaji wabidhaa, na ni kwa kipindi gani utawasambazia bidhaa hiyo, ikiwa ni kwa msimu au muda wote.

Upatikanaji wa huduma ya bidhaa unayotaka kutoa; kuangalia upatikanaji wa bidhaa au huduma unayotaka kutoa ni muhimu kuamua ikiwa ni ya msimu au inapatikana mwaka mzima. Usimamizi wa biashara yako; kusimamia biashara yako ni kipimo cha akili yako, hii ni pamoja na wakati wa kufungua, wakati wa kufunga, na usimamizi wa fedha.

Ukaguzi; ni muhimu sana kuangalia ikiwa unakua au unaingia katika hasara ya kupoteza fedha, rasilimali na muda, na darubini ya kujua hayo ni kupitia ukaguzi wa mara kwa mara.

Uhalali au usajili wa biashara; hii ni pamoja na malipo ya leseni ya kampuni na malipo ya ushuru ili kuepusha adhabu na faini zitokanazo na ukwepaji wa kodi.
 
swahili front PAGE..jpg
swahili front PAGE..jpg
SEHEMU YA PILI

MIKAKATI YA KUKUZA BIASHARA



Biashara yoyote yenye afya hupimwa kwa viwango vya ukuaji na unahitaji kujumuisha mikakati ifuatayo ili kuhakikisha kuwa biashara yako inakua;

Ongeza thamani; kudumisha thamani ya bidhaa na huduma, wateja wataendelea kununua bidhaa na huduma zako zikiwa ni bora. Wakati thamani inapoongezwa kwenye bidhaa ndipo na wateja wanaongezeka pia. Jifunze jinsi ya kuongeza thamani kwenye biashara yako, inaweza kuwa usafirishaji rahisi, bei nafuu, ufungaji mzuri, usafi, n.k.

Upana wa soko: bidhaa yako inahitaji wateja wengi kuwafikia wahitaji wengi kadri uwezavyo. Kupanua huduma zako na soko lako ndio mkakati bora wa kuelekea kufikia malengo yako ya biashara.

Kiwango cha Uwekezaji: Usitumie faida zote zinazoingia kutoka kwenye biashara yako, angalau asiliomia 15% ya faida ya biashara yako uweke akiba. Hii itasaidia katika kukuza biashara yako na uwekezaji katika wazo jipya la biashara.

Matangazo:
hakikisha unatumia njia zote zinazofaa za kutangaza biashara yako kuongeza wateja zaidi kwa kutumia vyanzo vinavyopatikana kama vile; wavuti, media za kijamii kama whatsapp, Facebook, YouTube, redio, magazeti,TV nk

Upangaji wa mipango imara ya biashara: hii itakusaidia kutambua malengo ya biashara yako na itakusaidia pia kushinda changamoto na kutoa mwelekeo wa biashara yako.

Epuka mawazo mengi ya biashara kwa wakati mmoja. Hii inaweza kukusaidia Kukupa utaalam na inakupa nafasi zaidi ya kupata maarifa ya kile unachofanya na kuongeza thamani yako, na ufanisi wako binafsi. Chagua wazo moja na ufanyie kazi ili kufikia malengo yako.

Kuendelea kujifunza katika maisha yako yote;
vyanzo vya kujifunza vinaweza kupatikana kupitia;- ushauri, utendaji kwa vitendo, uzoefu kutokana na kushindwa mara kadhaa, kupitia semina, media, nk Hakikisha unafanya kitu kila siku ambacho kitakusaidia kufikia malengo yako.

Habari sahihi: pata habari sahihi juu ya kile unachotaka kufanya? Jinsi gani ya kufanya? Je! Unataka kufanya wapi? Na jiulize swali hili "Je! Nina habari sahihi juu ya usimamizi wa biashara yangu?"
 
Back
Top Bottom