Gsan wa X-Plastaz: Msanii wa kwanza Tanzania kushiriki Tuzo za BET mwaka 2009

Gsan wa X-Plastaz: Msanii wa kwanza Tanzania kushiriki Tuzo za BET mwaka 2009

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Gsan.jpg

Rapa Gsan wa kundi la X Plastaz kutoka Arusha
Rapa Gsan wa kundi la X Plastaz kutoka Arusha, Tanzania, aliiwakilisha Afrika katika toleo la mwaka 2009 la BET Hip Hop Awards cypher, zilizorushwa Oktoba 27 kupitia chaneli ya BET huko Marekani. Huyu ndiye Mtanzania wa kwanza kushiriki katika tuzo hizi.

BET Cypher, kama inavyojulikana na wengi, ni sehemu ya BET Hip Hop Awards ambayo husubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa Hip Hop duniani kwani huwahusisha miamba wa muziki huo kutoka maeneo mbalimbali duniani. Gsan alishiriki akiwa pamoja na magwiji kama Eminem na KRS One, lakini pia Nipsey Hussle, aliyekuwa akiibukia katika ulingo wa Hip Hop wakati huo.

Gsan KRS One Premier.jpg

Gsan (katikati) akiwa na KRS One (kulia) pamoja na DJ Premier (kushoto)
Ushiriki wa X Plastaz kupitia Gsan katika BET Hip Hop Awards ni baada ya BET kuona video ya wimbo wao ulioitwa Nini Dhambi kwa Mwenye Dhiki kupitia YouTube. Wimbo huo uliokuwa umeangaliwa mara 400,000 ulikuwa ni moja ya nyimbo za Afrika Mashariki zilizotazamwa zaidi YouTube kwa wakati huo.

Na hivyo ndivyo Gsan alipata fursa ya kukwea pipa kuelekea Brooklyn, New York kurekodi cypher na baadaye kuhudhuria kilele cha tuzo hizo Jijini Atlanta, Georgia.

Ingawa Hip Hop kwa Kiswahili lilikuwa suala geni, lakini magwiji wa muziki huo kutoka Marekani, KRS One aka Teacha pamoja na DJ Premier walikoshwa sana na vionjo hivyo vya Kiafrika. Gsan hakufanya ajizi kuipeperusha bendera ya Tanzania.


Tazama video hii kumuona Gsan akiwakilisha Tanzania miongoni mwa magwiji wa Hip Hop duniani

“Kwangu ilikuwa kitu kikubwa sana kuwepo sehemu moja na watu kama Eminem, KRS One, huku DJ Premier akipiga midundo na mimi nikionesha kile nilicho nacho. Wengi walifurahishwa na nilichofanya na kuniuliza kwanini nili-rap kwa Kiswahili kwani walitaka kuelewa nichowasilisha. Niliwaambia Kiingereza si lugha yangu ya kwanza ingawa naizungumza na ninapenda”, alisema Gsan katika mahojiano baada ya uwakilishi huo.
“Kulikuwa na emcees kutoka duniani kote kwenye eneo moja na nilifurahi kuiwakilisha Afrika. Sikupigwa na butwaa kuwepo pale na wasanii wakubwa duniani, bali nilifurahi kuonesha uwezo wangu mbele ya marapa wenzangu.”

gsan-niki-sm.jpg

Gsan akiwa na rapa Nicki Minaj wakati wa BET Hip Hop Music Awards mwaka 2009 Atlanta, Georgia. Kabla ya hapa Nicki na Gsan walikuwa tayari wameshakutana katika Cypher Brooklyn, New York.
 
G san kwa cypher; noma sana hi cypher, hizi ndo cypher zilizokimbiza enzi hizi, sasa hivi sidhani kama zipo tena.
 
Kwani dablyusibi hawajauona huu Uzi watoe pongezi kwa gsan kumfungulia mond njia
 
Ni bahati mbaya mitandao yetu hii ilikuwa bado haijashika kasi. Hii 2009 nicki ndio alikuwa mpya mpya kwenye game?

Nakumbuka nicki nilimuona mara ya kwanza kwenye kundi jipya la young money na drake n.k. kama sikosei ni miaka hiyo hiyo 2009.

Aisee watu wameanza kupasua anga kitambo.
 
Back
Top Bottom