GSM anafanya atakalo Yanga

wajibisha

Member
Joined
May 16, 2021
Posts
90
Reaction score
215
Sasa ni rasmi klabu ya Yanga ipo mikononi mwa GSM na cha ajabu viongozi wako kimya kabisa.

Hawa wote wameletwa na GSM

1. Engineer Hersi
2. Karibu Mkuu Haji Mfikirwa
3. CEO Senzo
4. Haji Manara

Cha ajabu GSM yupo yanga kwa kofia mbili tu.

kwanza kama mzalishaji na msambazaji wa jezi za Yanga.

Pili, kama mdhamini katika masuala ya usajili ingawa wachezaji wanaoletwa wengi ni wa mkopo.

Kwa kofia hizo mbili dhaifu ni makosa makubwa kwa viongozi wa kuchaguliwa kama Mwenyekiti na Makamu wake kukubali GSM kuhodhi uendeshaji wa klabu kwa kujaza watu wake.

Kwanza hili la kumleta Manara ni aibu kubwa sana.

Viongozi wa Yanga amkeni.
 
" 2: karibu mkuu haji mkifirwa"

Nalog off [emoji125][emoji125]
 
Ongezea na nugaz vile vile kaletwa na GSM.

Yani pale asiyekuwa mtu wa GSM ni msolla, mwakalebela na bumbuli.

Lkn wao wamekalia kumsema Barbara mchepuko wa mo ndio mana kamuweka pale.

Je na huyo manara je kaletwa na nani pale?
 
Mpira unahitaji pesa, itakuwaje mtu atoe hela zake kisha asijipangie masharti?

Kama masharti yake huyapendi jiondoe Yanga
 
Bahati mbaya utopolo hawaoni ulichoandika hapa, wao wanamuangalia Mo tu.
 
Hakika mkuu, inasemekana Mwenyekiti Msolla kama kasusa. Kwa hali ilivyo inasemekana kuna pande mbili na PANAFUKUTA hasa, ni swala la muda tu.
 
Hakika mkuu, inasemekana Mwenyekiti Msolla kama kasusa. Kwa hali ilivyo inasemekana kuna pande mbili na PANAFUKUTA hasa, ni swala la muda tu.
Naomba sana Mungu ajalie Yanga wavurunde ili nione ngumi za Twaha Kiduku za ulingoni zikinafanyaje kazi kwenye vurugu ya patashika nguo kuchanika[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…