GTV: Ndio tumekula hasara au?

To me it doesnot make any difference, wote tu DsTv na GTV wanatukamua tena afadhali hata GTV maana nilkuwa natafakari kujiunga nao kwa kuwa gharama zao ni nafuu.

Nadhani ngekuwa bora kama Wafanyabiashara wetu wazawa wangeanzisha Makampuni ya aina hiyo, ingetuwezesha watzanania wengi kumudu gharama za kuona entertainment channels mbalimbali kwa bei nafuu. Laiti kama ITV, Channel, TEN au TBC1 wangenunua haki ya kurusha matangazo ya hizo entertainment channels na kuztuuzia kwa bei nafuu (naamini inawezekana mbona GTV waliuza kwa bei rahisi kuliko DsTv?) naamini Watanzania wengi tungeweza kufaidika
 
Mkuu pole sana,umechemsha vibaya sana,fanya utafiti kabla ya kupost!!!!!!!!
 
Mhh tuache utani jamaa amechemsha big time na hataki hata kurudi kuomba radhi kwa kubeba taarifa juu juu bila hata kuifanyia uchunguzi na kujiridhisha kidogo.DStv na GTV wapi na wapi? nakubaliana na mkulu aliyesema watanzania tuna tabia ya kufanya makosa ya aina hii kama kwetu huko TV walikuwa wanaita ITV na simu ya mkononi wanaita Mobitel!
 
Nafikiri ingekuwa vyema watanzania wangejua huyo mtanzania mwenye asilimia 50 ni nani. Baada ya hapo mamlaka husika can go after his bank account(s) na mali yote anayomiliki. Kwani hapa siri ni nini??? Kama KAGODA inajulikana ni mali ya nani, hii GTV ndiyo iwe siri????!!!
 
Sorry na samahani ni GTV na si DSTV. Na nimekubali nimechemsha au nimeropoka. Samahani kwa usumbufu ulijitokeza naomba kusahihisha meseji yangu kwamba ilihusu GTV na si DSTV.
 
Nimekubaliana na yote mliyosema kuhusu kuchemsha kwa habari niliyoitoa kwenye jamii forums yenye kichwa cha habari "DSTV yaingia mtini kinyemela", naomba kusahihisha habari hiyo na kusema "GTV ndio imeingia mtini". Wengi wa wachangiaji wamesema nimeropoka, nimetokea wapi na sikufanya utafiti wa kutosha na mengi yenye mtazamo huo. Nashukuru kwa kuliona hilo na kunipa mawazo ili niwe makini. Kilichonifurahisha zaidi ni kwamba wengi wetu tupo makini, hasa kugundua makosa. Pia nimefurahi kwani kwa muda mfupi wachangiaji wamekuwa wengi sana. Tuendelee na moyo huo wa kuelimishana.
 
noma tupu!! ramifications za credit crunch hatimaye sasa imeanza kutuingia wabongo directly

....na waziri wetu mmoja (sijui chizi) alisimama hadharani na kutudanganya eti msukosuko wa fedha duniani hautatuathiri watanzania akidai hatuna mfumo wa pesa kama wa magharibi! Wenye kujua tukaelewa ni kawaida ya siasa zao, kutudanganya tu kwa porojo. Thanks to Lipumba aliyempinga waziri huyu hadharani na kusema lazima tutaathirika. Na ndio kweli.

Ningekuwa rais, waziri huyu ningemfuta kazi wenzie wajifunze kuwa makini. Lakini mkuu wetu huyu ziiiiiiiiiiiiiiii kabisa. Amelala tu. Yeye na Mugabe tofauti ndogo
 

Ni waziri yupi huyo mkuu,kama vp mtaje tu tumjue
 
Mzee umeropoka, sio DStv ni GTV (General Television)

Mkulu General Television ni nyingine na si GTV tunayoizungumzia hapa,General Television yenyewe ipo Melbourne,Australia na inamilikiwa na Nine Network...Tunayoizungumzia hapa ni GTV inayomilikiwa na Gateway Broadcast Services...GTV ni jina tu ambalo hata Ghana Broadcasting Corporation(GBC) wanacho kituo chao cha televisheni kiitwacho GTV(Ghana Television),,,ni hayo tu mkulu....Be blessed
 
Goood news, Supersports wamenunua rights zilizobakia za kuonyesha mechi zote za EPL. Wao walikuwa na Package B (20%) na GTV walikuwa na Package A (80%) kwa ajili ya kuonyesha nchi za Sub Saharan Africa lakini kwa sasa wamerudisha Package A kwa mechi zilizobakia na pia mechi zote za msimu ujao. This is good news maana weekend hii mechi zote (the usual 8 live games) zitakuwa Supersports.
 
Kwa wale wateja wote wa GTV, DSTv watawapunguzia gharama na pia mtaweza kutumia Dish zenu zile zile. Mechi za weekend hii, 3 on Saturday na nafikiri 2 on Sunday (but not sure).
 
Mechi zitakuwa kwenye Supersport 7 kwa weekend hii... Pre and Post Coverage itakuwa ni ile ile kama ilivyokuwa ya misimu ya nyuma. Premier league rights zimeanza kuuzwa tena hapa Uingereza (huwa zinauzwa kwa misimu 3) na hivyo basi kunaweza kukawa na provider mwingine kuanzia msimu wa 2010/2011 but lets wait and see. Kwa sasa naomba niishie hapa, tutaonana tena jioni. Siku njema watanzania wenzangu.
 
This is bad news for all football suporters especially in Africa and across the globe in general. We hope that DSTV will secure 100% of the rights so we can continue to watch and suport "our" England teams, and especially my Arsenal. Go gunners!

Mimi mwenyewe ni mpenzi mkubwa wa Arsenal na ningependa kukwambia kwamba kwa sasa utaweza kuona mechi zote za Arsenal as it is a top team and hence DStv gives it a preferential treatment when it comes to live games.
 
Nadhani zitauzwa kwenye liquidation hiyo, ndo mwanzo wa DSTV kurudi kwenye monopoly.

Nadhani hawa jamaa wataendelea kuwa na monopolistic powers when it comes to EPL maana sidhani kama AU wana sheria zinazozuia kampuni moja kuwa na haki zote za kuonyesha michuano mikubwa kama huu.

Hapa UK, EU wanasheria zinazozuia kampuni moja kuwa na rights zote za kuonyesha mpira na hivyo kuna kampuni mbili kwa sasa (Skysports na Setanta) ambazo zinagawana mechi kama ilivyokuwa hapo nyumbani. Hivyo basi ukiwa hapa inabidi uwe na kampuni hizo zote mbili ili uweze kuona mechi (kawaida ni mechi 4 live per weekend).
 
Kwa wale wateja wote wa GTV, DSTv watawapunguzia gharama na pia mtaweza kutumia Dish zenu zile zile. Mechi za weekend hii, 3 on Saturday na nafikiri 2 on Sunday (but not sure).

nimeongea na jamaa wa DSTV wanasema inabidi ubadilishe decoder na card kwenye hiyo package ya GTV (kama ulikuwa nayo) na dish inabidi liwe adjusted in terms of direction.
 

DSTV wameuziwa rights za 3yrs kuonyesha EPL
 
Hilo la kurudishiwa hela naona msahau, kwenye liquidation ya kampuni wateja mtakua watu wa mwisho kabisa kufikiriwa. Kuna creditors kibao, walichukua zaidi ya $200 mill kuanzisha kampuni, mpaka zirudishwe hizo kwanza.
 
SuperSport brings England to Africa!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…