Guardiola aamua kumpiga Benchi Joe hart .

Guardiola aamua kumpiga Benchi Joe hart .

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Mzee wa Mabifu Guardiola ameamua Joe Hart awe kipa wa chaguo la pili , baada ya leo tena kumchomesha mahindi kwenye benchi .

Ikumbukwe kwamba hata ule mchezo wa kirafiki dhidi ya Arsenal hali ilikuwa hivihivi , swali ni je Joe Hart atakubali kuchomeshwa mahindi na kupoteza namba kwenye timu ya Taifa ?

Yetu macho .
 
Mimi huwa naona Caballero yuko vizuri tu. Kama Caballero hatafanya makosa ya kizembe itabidi tu Joe Hart atafute timu ingine
 
Ni yapi makosa ya Joe Hart ?

.. ni just a dip in form siku za karibuni. Ila nafikiri ni makosa aliyoyafanya akiwa anachezea England ndiyo hasa yanamgarimu. Kumbuka lile goli alilofungwa na Bale; na lile lingine la Iceland .. media & pundits wengi walimuelekezea vidole
 
mkuu mtoa mada JOE HART NI KIPA MZURI sasa huyu kocha anasema hivi anapenda golikipa anayeUNGANA NA MABEKI KUOKOA MPIRA kwa mfano unakumbuka mechi ya kombe la dunia baina ya Argentina na Ujerumani ilitokea shambulizi langoni mwa Ujerumani kijana HIGUANI aliingia ndani ya 18 huku walinzi wa Ujerumani wakiwa wameduwaa yule golikipa wao NEUVER alijitoa muhanga kwa kutoka golini kwenda kupambana na Higuani matokeo yake golikipa alifanikiwa kuzima ndoto za Higuani kupata goli hapa makipa ambao angetamani apate ni kama kipa wa Atletico ,kipa wa manchester.
 
mkuu mtoa mada JOE HART NI KIPA MZURI sasa huyu kocha anasema hivi anapenda golikipa anayeUNGANA NA MABEKI KUOKOA MPIRA kwa mfano unakumbuka mechi ya kombe la dunia baina ya Argentina na Ujerumani ilitokea shambulizi langoni mwa Ujerumani kijana HIGUANI aliingia ndani ya 18 huku walinzi wa Ujerumani wakiwa wameduwaa yule golikipa wao NEUVER alijitoa muhanga kwa kutoka golini kwenda kupambana na Higuani matokeo yake golikipa alifanikiwa kuzima ndoto za Higuani kupata goli hapa makipa ambao angetamani apate ni kama kipa wa Atletico ,kipa wa manchester.
Guardiola anafahamika kwa mabifu yasiyo na kichwa wala miguu , kama hakumtaka Hart si angemwambia atafute timu tu ?
 
Guardiola anafahamika kwa mabifu yasiyo na kichwa wala miguu , kama hakumtaka Hart si angemwambia atafute timu tu ?
mkuu hawa ni binadamu sio malaika hivi fikiria mtu kama JOSE kwa maneno anayompa Juani Mata unawaza huyu anamatatizo gani kichwani.
 
Back
Top Bottom