Guéhi aibua gumzo EPL baada ya kuandika 'I Love Jesus' kwenye kitambaa cha unahodha chenye rangi za upinde/LGBTQ+

Guéhi aibua gumzo EPL baada ya kuandika 'I Love Jesus' kwenye kitambaa cha unahodha chenye rangi za upinde/LGBTQ+

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Beki wa kati wa Crystal Palace na England, Marc Guéhi huenda akachukuliwa hatua za kinidhamu na Shirikisho la Soka la Uingereza (FA) baada ya kuandika “I LOVE JESUS” kwenye kitambaa chake cha unahodha wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Newcastle mchezo uliomalizika kwa sare ya 1-1 jumamosi ya Novemba 30.
1733227491831.png
Vitambaa vya unahodha vyenye rangi ya upinde viligawiwa kwa vilabu vyote 20 vya Ligi Kuu kwaajili ya kusaidia jumuiya ya LGBTQ+, hivyo uamuzi wa Guéhi wa kuongeza ujumbe wake binafsi unaohusu dini unaweza kuchukuliwa kuwa ni ukiukaji wa Sheria za Mchezo kwani vitambaa hivyo haviruhisiwi kuandikwa kitu chochote cha kibinafsi.

Soma, Pia: Nahodha wa Ipswich Town, Sam Morsy agomea kuvaa kitambaa cha Unahodha chenye Upinde kwa sababu za Kidini
 
BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE ALITUTAJIA MAADUI.

1. UMASIKINI
2.UJINGA.
3. MARADHI.

Akasema Hawa ni maadui wa kweli kweli katika hili Taifa.

LEO 2024 BAADA YA MIAKA 60 TUMEKUWA NA MAADUI WENGI ZAIDI.

2024 maadui wameongeseka Zaidi kuliko wale watatu wa 1961.

1.Umasikini na ufukara.
2.Ujinga na upumbavu.
3.Magonwa na Maradhi.

4.Mmomonyoko wa Maadili.
ushoga, usagaji Kamali, sugar mamy, sugar Dady mashangazi
AJIRA.
5. Rushwa na Upendelo

6. USimba na u yanga.
7. Mitandao ya kijamii Tiktok, x, nk
8. Manabii wa uongo na Mashehe Uchwara.
9. Ajali nyingi mno.
10. Gharama kubwa za maisha, ujenzi holela nk

MAMBO NI MENGI SANA VIJANA WA KITANZANIA WANAWAZA MAMBO YA HOVYO SANA SIMBA NA YANGA ZINATAWALA MIKEKA NK.

OKOENI TAIFA LENU LEO.
MKIFIKA MBINGUNI MTAHOJIWA NA MUNGU MLILIFANYIA NINI TAIFA LENU NIMEMALIZA.
 
I LOVE JESUS, huo ujumbe una ubaya gani? labda kama una ubaya ni kuandika ujumbe huo kwenye huo utepe wenye rangi ya pendera ya kusapoti wapenzi wa jinsia moja. manahodha wengine nao wataandika yao kama vile free palestine, na mengine mengi
 
Kwani si alipaswa tu kukataa kuivaa hiyo arm band ya akina James delicious na kuivaa ile ya Jesus wa Nazareth.
 
Walimu waliotufundisha mbinu za kukabiliana na maisha ikiwa Ni pamoja na tabia njema na maadili wameangushwa na viongozi wa juu. Inatufanya kuwaona waongo pindi tunapomaliza masomo na kukuta uhalisia Ni tofauti na kile walichopigia kelele shuleni.
 
Mnafiki tu huyo. Unavaa arm band ya ushoga halafu unaandika Yesu. Mnafiki wa Hali ya juu
 
kuna mahala shetani huitwa mungu wa dunia hii "mungu" inayoanzwa kwa herufi ndogo.
2Kor 4:4

JESUS IS LORD&SAVIOR
Ndio ni mungu lakini ni kwa wale tu ambao wamepokea ajenda zake yaan ni kwa wale walimwengu walio mpokea
 
Siku zijazo wataweka rangi zao kwenye jezi hawa wakuda
 
I LOVE JESUS, huo ujumbe una ubaya gani? labda kama una ubaya ni kuandika ujumbe huo kwenye huo utepe wenye rangi ya pendera ya kusapoti wapenzi wa jinsia moja. manahodha wengine nao wataandika yao kama vile free palestine, na mengine mengi
Huo ujumbe huo,, I love Jesus una nguvu kubwa sana kwa sababu ushoga ni pepo na Jesus hufukuza mapepo, kwa ujumbe huo, umewatisha mapepo ya ushoga.
 
Back
Top Bottom