capacity 0GB
Member
- Jul 6, 2020
- 43
- 52
ZIARA ZA GWAJIMA KWENYE MITAA NA KATA ZIMEONYESHA UDHAIFU MKUBWA WA HALIMA MDEE KATIKA KUWATUMIKIA WANANCHI.
Kawe, Dar es Salaam.
Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM ndugu Josephat Gwajima ameendelea na ziara zake kwenye mitaa na Kata za jimbo la Kawe ambapo amekua akishirikiana na wananchi katika kutatua kero zao za Msingi hasa zile za miundombinu ya maji taka.
Ziara hizi zinaacha alama mpya kwa Gwajima ambaye Kwa sasa amekua akitembea mtaa kwa mtaa na kubaini kero za Msingi za wananchi ambazo zimekuwa sugu katika kata kwa muda wa miaka kumi sasa chini ya Halima Mdee.
Ukubwa wa kero hizi unamfanya Halima Mdee kuonekana kama mgombea asiye na nafasi tena mbele ya wananchi Kwani zinaonyesha madhaifu yake kwa umma ambao umemchagua kwa miaka kumi sasa.
_“Wananchi wa Kawe wanahitaji muwakilishi ambaye atasimamia maslahi yao, Maendeleo yao na kuondoa kero zao kwa kushirikiana na serikali na sio Mbunge ambaye anapita kwetu na kutuona sisi ni Muhimu kila Baada ya miaka mitano, tunahitaji muwakilishi wa wananchi wa Kawe atakayetatua kero zetu wana Kawe na sio kwenda bungeni kujadili mambo ambayo sisi hatukumtuma kwenda kuwakilisha”_ Hassan Ramadhan Omary, mkazi Msasani.
Josephat Gwajima ni moja ya wagombea waliojiandaa na wanaotarajiwa kuwa na ajenda kubwa za mabadiliko kwa wananchi kwa miaka ya hivi karibuni, hii ni kutokana na aina yake ya siasa na kusimamia ukweli.
Mpaka sasa tayari Gwajima amefanikiwa kutembelea zaidi ya Kata 6 kati ya 10 za jimbo la Kawe akiendelea kubaini changamoto na mapungufu makubwa ya kiutendaji na kiuongozi yanayotokana na uongozi uliopita chini ya Halima Mdee ambaye aliwekeza muda mwingi kwenye Siasa za kitaifa na kusahau mambo ya msingi yanayohusu jimbo lake la uchaguzi na kero za msingi za wananchi.
Katika ziara yake inayoendelea katika Kata ya Msasani Alia mbaya na na Mgombea Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi ndugu Luca kwa pamoja wamehaidi kuboresha miundombinu ya maji taka ambayo imekua chanzo Kikubwa cha mafuriko Kwa wakazi wa Kata ya msasani.
_”nia yetu ni kuhakikisha tunawarudishia wananchi wa Kawe haki yao ya msingi ya uwakilishi sahihi ndani ya bunge ili kuweza kuwa na maendeleo yanayoendana na ukuaji wa Mji wa Dar es Salaam. Kukosekana kwa uwakilishi sahihi ndio kumekuwa sababu ya wananchi kuendelea kuteseka na kukosa Mbunge ambaye anaweza kusimamia Maendeleo ya jimbo ila kuwa na mbunge ambaye atatua kero za wananchi ikiwemo ujenzi wa miundombinu bora ya maji taka, barabara za mitaa zenye mitaro yenye uwezo na viwango na kusogeza zaidi huduma muhimu za afya Kwa wananchi na kazi hii Chama cha Mapinduzi inaiweza na sasa tumeamua kuhakikisha wananchi wanapata kile walichokuwa wanakikosa”_ Mzee Khalid, Kada wa CCM Kawe.
Josephat Gwajima anaendelea na ziara zake kwenye mitaa huku akiomba kura kwa wananchi kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi na kumchagua Rais Magufuli ili kuweza kurejesha hadhi ya Mji wa Kawe.
Husna Mkuza
Freelance Journalist
Kawe
Kawe, Dar es Salaam.
Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM ndugu Josephat Gwajima ameendelea na ziara zake kwenye mitaa na Kata za jimbo la Kawe ambapo amekua akishirikiana na wananchi katika kutatua kero zao za Msingi hasa zile za miundombinu ya maji taka.
Ziara hizi zinaacha alama mpya kwa Gwajima ambaye Kwa sasa amekua akitembea mtaa kwa mtaa na kubaini kero za Msingi za wananchi ambazo zimekuwa sugu katika kata kwa muda wa miaka kumi sasa chini ya Halima Mdee.
Ukubwa wa kero hizi unamfanya Halima Mdee kuonekana kama mgombea asiye na nafasi tena mbele ya wananchi Kwani zinaonyesha madhaifu yake kwa umma ambao umemchagua kwa miaka kumi sasa.
_“Wananchi wa Kawe wanahitaji muwakilishi ambaye atasimamia maslahi yao, Maendeleo yao na kuondoa kero zao kwa kushirikiana na serikali na sio Mbunge ambaye anapita kwetu na kutuona sisi ni Muhimu kila Baada ya miaka mitano, tunahitaji muwakilishi wa wananchi wa Kawe atakayetatua kero zetu wana Kawe na sio kwenda bungeni kujadili mambo ambayo sisi hatukumtuma kwenda kuwakilisha”_ Hassan Ramadhan Omary, mkazi Msasani.
Josephat Gwajima ni moja ya wagombea waliojiandaa na wanaotarajiwa kuwa na ajenda kubwa za mabadiliko kwa wananchi kwa miaka ya hivi karibuni, hii ni kutokana na aina yake ya siasa na kusimamia ukweli.
Mpaka sasa tayari Gwajima amefanikiwa kutembelea zaidi ya Kata 6 kati ya 10 za jimbo la Kawe akiendelea kubaini changamoto na mapungufu makubwa ya kiutendaji na kiuongozi yanayotokana na uongozi uliopita chini ya Halima Mdee ambaye aliwekeza muda mwingi kwenye Siasa za kitaifa na kusahau mambo ya msingi yanayohusu jimbo lake la uchaguzi na kero za msingi za wananchi.
Katika ziara yake inayoendelea katika Kata ya Msasani Alia mbaya na na Mgombea Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi ndugu Luca kwa pamoja wamehaidi kuboresha miundombinu ya maji taka ambayo imekua chanzo Kikubwa cha mafuriko Kwa wakazi wa Kata ya msasani.
_”nia yetu ni kuhakikisha tunawarudishia wananchi wa Kawe haki yao ya msingi ya uwakilishi sahihi ndani ya bunge ili kuweza kuwa na maendeleo yanayoendana na ukuaji wa Mji wa Dar es Salaam. Kukosekana kwa uwakilishi sahihi ndio kumekuwa sababu ya wananchi kuendelea kuteseka na kukosa Mbunge ambaye anaweza kusimamia Maendeleo ya jimbo ila kuwa na mbunge ambaye atatua kero za wananchi ikiwemo ujenzi wa miundombinu bora ya maji taka, barabara za mitaa zenye mitaro yenye uwezo na viwango na kusogeza zaidi huduma muhimu za afya Kwa wananchi na kazi hii Chama cha Mapinduzi inaiweza na sasa tumeamua kuhakikisha wananchi wanapata kile walichokuwa wanakikosa”_ Mzee Khalid, Kada wa CCM Kawe.
Josephat Gwajima anaendelea na ziara zake kwenye mitaa huku akiomba kura kwa wananchi kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi na kumchagua Rais Magufuli ili kuweza kurejesha hadhi ya Mji wa Kawe.
Husna Mkuza
Freelance Journalist
Kawe