H. Polepole, Profesa Kabudi na Bashiru Ally juu ya Katiba Mpya na Muungano

H. Polepole, Profesa Kabudi na Bashiru Ally juu ya Katiba Mpya na Muungano

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Profesa Kabudi alisema wazi, kuwa kwenye ishu ya muungano, wazanzibar mambo yao yako mezani, yako well documented isipokuwa yale ya Tanganyika. Akasema anaogopa siku watanganyika watakaponyanyuka na kudai mambo yao

Humphrey Polepole akasema, Katiba ya Sasa inampa Rais wa sasa madaraka makubwa mno yakiwemo ya teuzi za kila namna hadi kuanzia mawaziri hadi wakurugenzi na akasema Makatibu wakuu wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar wanataka serikali tatu na hata makatibu wakuu wa Serikali ya Muungano walitaka Serikali mbili lakini mambo ya muungano yaongezwe, akaendelea kusema kuwa hata kamati ya Makatibu wakuu wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar walitaka mambo ya Muungano yapunguzwe, Ofisi ya waziri mkuu ilitaka serikali tatu na ofisi ya makamu wa wa rais ambayo ilikuwa na dhamana ya mambo ya kujadili kero za mambo ya muungano ilitaka serikali tatu

Bashiru Ally yeye akasema Katiba ya sasa ya mwaka 1977 haiendani na mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi.

Kwa hiyo ninashangaa wale wanaomshambulia Lissu juu ya muungano na kutaka kutengeneza muungano mzuri zaidi usio wa manung'uniko kutoka pande zote mbili

Hata rasimu ya Warioba ilisena wazi kuwa Kwa Muundo wa sasa wa Muungano, mambo hayako clear, je Tanganyika ndo Tanzania yenyewe au ni kitu gani?

Kuna njia moja tu inayoweza kuulinda Muungano, njia yenyewe ni:

Tusiwaingilie wazanzibar mambo yao ya ndani, namna hii watatuheshimu na hawatatuona wakoloni. Ila hii tabia ya kuwachagulia viongozi Dodoma na kuwapandikiza ipo siku zanzibar itarevolt, na ikirevolt itavunja muungano.

Iwapo chuki yao dhidi ya Muungano itakuwa kubwa kuliko chuki yao ya upemba na uunguja, huu muungano hauna future.
Na hii chuki dhidi ya Muungano itasababishwa na tabia zetu za kudhulumu sauti za wananchi wa Zanzibar kwenye kujichagulia viongozi wao wenyewe!

1: Humphrey Polepole



2: Profesa Kabudi

 
Kwa hiyo matamshi au misimamo au kauri za Polepole, Bashiru,Kabudi wakati ule zilikuwa zimejazwa na roho mtakatifu,je za sasa zimejazwa na nini?
 
Aisee. Hawa jamaa nikikumbuka walichokuwa wanakisimamia kwenye mchakato wa katiba mpya..

Ukiwalinganisha na sasa. Ilibidi wawe wanazomewa kila siku wanapopita. Lakini leo ndiyo mashujaa na wanaaminika kweli kweli.
 
Mchawi mpe mwanao akulelee!
NB: Tuache kuwa ving'ang'anizi kujaribu kumuenzi baba wa Taifa hata alipokosea! ... tukianza kufikiri namna hii matatizo mengi aliyotuachia yatatatulika, nayeye atapumzika kwa amani!
 
ukishajiunga CCM unakabidhi ubongo wako pale reception ya Lumumba, unaupitia siku ukiihama.
 
Kabudi wa 2013 akikutana na Kabudi wa sasa lazima zipigwe ngumi kali sana, ni watu wawili tofauti!
Teh teh teh .... Kuna msemo unasema "siyo vizuri kuongea wakati wa kula"....teh teh teh..

Kuhusu uwepo serikali ya Tanganyika ni kuwa serikali hiyo ipo ila imevaa koti la serikali ya muungano.

Yaani serikali ya Tanganyika ndio hiyo hiyo serikali ya Tanzania ndio maana wengine wanaonea aibu jina Tanganyika hivyo wameibatiza jina jipya "Tanzania bara".
 
Sasa hivi wako kwenye V8 za kijani ukiwapelekea hizo clips watakuchapa makofi. Kama kuna kitu cha msingi duniani ni kukumbushana. Ahsante mleta mada kwa kuwakumbusha hawa “wanafiki wa taifa”
 
Dah, hii mada inahuzunisha sana, inaonyesha jinsi watu walivyo wakiwa hawana vyeo na wakati wakipata vyeo wanavyokuwa wanafiki.

Watu kama hawa ni wa kupuuzwa tu kwani ni wachumia tumbo tu.
 
Back
Top Bottom