Haba na haba hujaza kibaba au kibubu?

Haba na haba hujaza kibaba au kibubu?

Jospina

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2013
Posts
2,421
Reaction score
1,395
Naomba mnisaidie kuwarekebisha jamaa hawa. Wahenga walisema HABA NA HABA HUJAZA KIBABA. Kamwe, katu, katiti, abadan wahenga hawakusema "haba na haba hujaza KIBUBU". Hapana, tusiwalishe maneno wahenga wetu.Naomba waambieni hawa jamaa waseme hivi; "Wahenga walisema haba na haba hujaza KIBABA lakini sisi tunasema haba na haba hujaza KIBUBU". Watoto wetu shuleni wakiulizwa kujaza methali ya haba na haba.... kuna hatari wakajaza "hujaza kibubu" Baraza la Kiswahili la Taifa mko wapi?
 
Haba + Haba=Mahaba.

Wao (Voda M Pawa na CBA) ile wameiweka kibiashara, ni ubunifu tu.
 
Redio zinaua sana lugha ya Kiswahili na bakita wamelala usingizi wa pono
 
Hili liko kibiashara mkuu,ni ubunifu tu. Pia mtoto anafundishwa na kujibu kile alichofundishwa na mwalimu.

Kipindi tunakua tulikuwa tunafanya utani wa Methali mfano "Mga mgaa na upwa hali wali bila mchuzi" lakini hatukuwahi kujibu hivyo kwenye mtihani.
 
Naomba mnisaidie kuwarekebisha jamaa hawa. Wahenga walisema HABA NA HABA HUJAZA KIBABA. Kamwe, katu, katiti, abadan wahenga hawakusema "haba na haba hujaza KIBUBU". Hapana, tusiwalishe maneno wahenga wetu.Naomba waambieni hawa jamaa waseme hivi; "Wahenga walisema haba na haba hujaza KIBABA lakini sisi tunasema haba na haba hujaza KIBUBU". Watoto wetu shuleni wakiulizwa kujaza methali ya haba na haba.... kuna hatari wakajaza "hujaza kibubu" Baraza la Kiswahili la Taifa mko wapi?

hata mimi hili linanitatiza...naona matangazo ya vodacom eti 'haba na haba hujaza kibubu' wakati mimi nimesoma miaka yote nafumdishwa 'HABA NA HABA HUJAZA KIBABA"
 
Mi najua haba na haba hujaza kibaba hyo kibubu ni ya vodacom na cba tu haiwahusu wahenga sasa vodacom wasiseme wahenga walisema watafute namna nyngine
 
Hata me ninavyojua na nilivyosoma kwamba wahenga walinena"haba na haba hujaza kibaba" ,hayo mengine ya uzushi tu na pia ni njia ya kuidumaza lugha ya kiswahili na misamiati yake
 
Redio zinaua sana lugha ya Kiswahili na bakita wamelala usingizi wa pono

Kimsingi redio zimekuza sana lugha ya Kiswahili, kuongea kwa namna isiyobadilika ni dalili za lugha kufa. Kuongezeka kwa lugha ni kuongezeka kwa idadi ya wasemaji, uwanja wa matumizi na kukua kwa msamiati.

Kuhusu mada, naona kuwa Vodacom wako sawa, wahenga walisema vingine ndio. Lakini sio tatizo kwa lugha ya kibiashara kubadili utaratibu kwa minajili ya kunogesha. Kingine ni kuwa dhana ya kibubu imeeleweka sana kwa wateja waliolengwa kuliko kibaba ambacho ni wachache sana miongoni mwa wasemaji wa Kiswahili wa sasa wanaelewa.
 
Lugha yeyote inasifa ya kukua na kuimarika au Kufa.... Hivyo mabadiliko Hayo ya Methali hiyo Sio dhambi kwa mmahiri wa lugha.... Hivyo Neno lililotumiwa sana hapo awali KIBABA limepungua umaarufu kwa sababu ya.. Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.... Kwa ujio wa Mizani na Hivyo matumizi ya vifaa kama Ndonya au Kibaba, Sado na Makopo nk. Hivyo Kibubu ni neno Mtambuka lililokuja ambalo linamaana.... Kifaa maalum cha kuhifadhia... Zaidi fedha... Kidogo kidogo.. Kwa lengo la kujiwekea akiba.. Hivyo Vodacom wametumia fursa kusema Haba na Haba Hujaza Kibubu..... Yenye fasili... Kidogo kidogo hufanya vitu kuwa vingi au kusheheni
 
Back
Top Bottom