Habari njema - Arsenal yaanza mazungumzo na Massimiliano Allegri

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hatimaye ile timu mbovu na yenye mwenendo wa kuaibisha Arsenal , imepata maono mapya na taratibu imeanza kulivua limbwata ililopewa na kocha aliyechoka Arsene Wenger.

Vyombo mbalimbali vya habari za michezo vimeripoti kuanza mazungumzo ya kumpata kocha wa Juve , Allegri ambaye kwa Italy ni kama ameshinda kila kitu , huku akielekea kuivusha UEFA CHAMPIONS LEAGUE Juve dhidi ya Timu ya marefa ya Barcelona .

Kila la heri Arsenal .
 
Juve lazima achapwe wiki ijayo-watatoka 3-0 kisha kwenda dakika za nyongeza
Naiona nusu fainali ya barca na altetico madrid
 
Unakosea sana kusema Arsenal ni mbovu! Sasa Sunderland itakuaje??
 
Unakosea sana kusema Arsenal ni mbovu! Sasa Sunderland itakuaje??
Nakuhakikishia Sunderland itaitandika Arsenal gemu ya marudio , Arsenal sasa hivi ni sawa na shamba la kijiji , wala si shamba la bibi tena , maana shamba la bibi ni la ukoo tu .
 
hizi habari za kuanza mazungumzo zipo kila leo ..wamiliki watakapo ona hata makombe yanumuhimu pia pamoja na faida wanayoipata watafanya maamuzi.
Gunnerz till i die
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…