Habari njema kwa watanzania wote wenye ndoto za kusoma nje ya nchi

pide89

Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
41
Reaction score
3
Tunasaidia watu kupata admission, kupata passport na visa, tunasaidia pia kupata hostel au appartment ya kuishi unapokuwa masomoni kwa gharama nafuu!
Nchi tunazohusika nazo na tunaconnection nazo ni
-u.s.a(jimbo la calfonia)
-malaysia
-india
application zinaanza mwezi huu mpaka wa pili na masomo ya muhula wa kwanza yanaanza mwezi wa nne 2015
gharama za kupata admission ni $500 na tutakujulisha ada ya chuo
kwa mawasiliano zaidi tucheki kupitia +255764014285
 
HUDUMA GHARAMA
Ukienda uhamiaji gharama ya passport ni sh. 50,000= USD 29
Visa ya marekani ni USD 100
University application fee haizi USD 100
JUMLA USD 229

Ina maana wewe unatoza watu mara mbili zaidi ya gharama husika? hata kama ni kupata faida punguza tamaa mkuu

NB: Kuomba chuo popote pale duniani hakuhitaji connections, kama una vigezo utapata na kama huna hautapata, vyuo vyote vina website, msiwe wavivu ndugu wa kusoma kila kitu kipo mitandaoni, vyuo vizuri kuvijua ni rahisi tu ingia google utapata kila kitu kuanzia mwaka chuo kilipoanza mpaka mwisho. Kuhusu hostel hutolewa kwa foreigners kwa kulipa accomodation fee na sio mtu anakaa anabuni biashara za kihuni badala ya kwenda kulima
 
Sasa wewe unafikiri kuna kazi ya bure.

 

Mkuu pokea like zangu mia nane, wabongo wavivu sana wa kufikiri, hapa jamaa ndo kawaza mpaka bhasi then kaamua kuja na mradi wa kitapeli kama huu!
 
wakubwa wanasema busara ni kukaa kimya! sijaona kinachowafanya muandike hayo maneno! nafikiri ni kwa sababu ya maslahi yenu binafsi! huenda na nyinyi mmejaribu kufanya hvyo mmeshindwa! naomba mtuachie wenye vipaji vyetu! we ulikuja kupata huduma kwetu ukaona ni uhuni?
 
nchi hii haiwez kuendelea kama kila mtu atakuwa dalali, tunahitaji kuingia katika uzalishaji
Mkuu umemshukia!! Yaani kama Eagle! She.nzy type kabisa, eti tuna connections na nchi za usa, japan, sijui na wapi? Mimi nikafikri anatangazia watu scholarship kumbe kuomba chuo, kutafuta viza, kutafuta hostel! Sasa kuomba chuo nako mpaka upite kwa dalali? Kutafuta viza nayo mpaka dalali? Hopeless kabisa hili jamaa, bora litafute biashara nyingine kama limechoka kubeba maboksi!!

Sasa hivi udalali siyo deal tena maana vitu vingi viko kwenye mtandao ni kiasi cha ku-google tu vitu vinamwagika hapo!
 
Jamani msimshukie jamaa ki vilee. Kuna mahitaji ya hii biashara. Amin nawambieni kuna watu hawawezi kufanya kitu chochote wenyewe. Ni lazima wafanyiwe. Kuna wengine wanajidai wako busy na kuna wengine waoga tu na hhawajiamini.

Hata ulaya zipo hizi.
 
Jamani msimshukie jamaa ki vilee. Kuna mahitaji ya hii biashara. Amin nawambieni kuna watu hawawezi kufanya kitu chochote wenyewe. Ni lazima wafanyiwe. Kuna wengine wanajidai wako busy na kuna wengine waoga tu na hhawajiamini.

Hata ulaya zipo hizi.

Nisaidie kushangaa, wengine apa tunataka kusoma nje ila hatujui lugha ya malkia na wala hatujui nn cha kufanya mpaka tupate vyuo nje ya nchi, so hawa jamaa wapo sahihi, kama wewe unaelewa kila kitu ni wewe , tuache sie mamburula tutapeliwe sijui ndo kuliwa ilimrad tupate information sahihi
 

Mkuu BUKU JERO (Phd) hizo dolla 500 hazihusu gharama za visa,passport na admission fee,hiyo $500 ni yake kama ilivyo.
 
Last edited by a moderator:
Yani mtu akutafutie PASSPORT,VISA,HOSTEL kwa $500 unamuita tapel????
ama kweli watz tumerogwa.
 
Daka mtumba kaka naona yuko sahihi kabisa=passport+visa+hosteli kwa $500 hah mbona ok kabisa jamani kwani kuna agency watu wanalipa mpaka $980 na bado watu wanajazana ktk ofisi mhh watanzania tupunguze lawamaaaaa.....
 
Daka mtumba kaka naona yuko sahihi kabisa=passport+visa+hosteli kwa $500 hah mbona ok kabisa jamani kwani kuna agency watu wanalipa mpaka $980 na bado watu wanajazana ktk ofisi mhh watanzania tupunguze lawamaaaaa.....

Kuu naona hujamsoma fresh embu jaribu kusoma tena thread yake, emeandika tunafanya admission kwa $500,it means viza,passport utalipia na gharama nyingine yaani fees za chuo watakujulisha and utalipia.
Kwanini mtu usifanye mwenyewe, kwanza unakuwa na uhakika na jambo lako,unminimize cost zisizo na mpango na unapata kujua mambo mengi zaidi!
 
Kunajamaa yangu alienda kwa kampuni km hyo ilikua maeneo ya legho star, aligharamia karib laki tano, hadi leo ulaya anakisikia. Cjui hakua na sifa walimficha? Me nadhan ni km private hosptal wanakubambika magonjwa mengi ili ununue dawa nyingi
 
I dont think its right to discourage..the...business you are doing..keeep advertising no matter how people think about yu ...i know mnasaidia watu kupata elimu...nd at the same time..they have to pay yu back for your services ...nyc job pide 89 ....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…