Leo tuna Hadith mpya
DONDA LA WIVU
👇
LEO MCHANA.
“Ni lazima niitishe kikao cha wazee wa Mila, ni lazima nipange siku moja maalumu kuwakomoa firauni hawa, wajinga na wapuuzi wanao yachezea maisha yangu ………… Nakwambieni Ally mpuuzi wewe nitakukomesha. Mwaka huu nitakukomoa ili uione dunia chungu, kama uchungu wa nyanya chungu, Ng’ombe we!” Mzee Jamali aliwaza yeye na moyo wake, amekasirika sana siku ya leo, hajapata kuwa na hasira kama alizonazo leo, kamwe hajapata kukasirika kama alivyokasirika leo, leo Shetani kamwingia, tena huyo Shetani kamshawishi afanye hima hima apate kumkomoa Ally mwanawe wa kumzaa.
“Ninatamani kumwaga damu, damu ya makafiri wapuuzi, wajinga, mafirauni nyie mnanihujumu mapenzi yangu.” Macho ya mzee Jamali yaliiva kwa hasira. kujibanza kwake nyuma ya kijumba nyasi haikutosha kuipunguza jaziba aliyokua nayo, hasira zilimpanda pale akimuona mkewe mpenzi Tunu binti mashallah! Amesimama na Ally mwanawe wa kumzaa, kila ikiwa leo hawana jambo la muhimu kujadili zaidi ya kutizamana machoni kama Ndege wawili mapenzini.
Hawana jambo lolote lile muhimu zaidi ya kunena nena vijimaneno ambavyo Mzee Jamali Mzee mwenye umri wa miaka sabini na ushee anahisi ndani ya fikara zake kuwa wawili hawa wanaongea juu ya mapenzi, mapenzi yao wenyewe, japo kwa usiri mkubwa ambao si Tunu wala si Ally aliyekua tayari kumweleza Mzee Jamali
“Tunu nilikutoa Kijijini kwenu ukiwa umeoza, unanuka, umeharibika. Miguu yako yote miwili ilikua imeoza na kuharibiwa na Funza, ambao kwa mikono yangu hii miwili nilikua radhi kuwachezea chezea hao Funza na kuwatoa miguuni kwako, ulikuja kijijini kwangu ukiwa umekonda haswa, umekonda kama gofu lililoachwa na Mkoloni, umekonda na kudhoofika, umekonda mifupa mifupa, umekonda kama Mnazi uliokosa mbolea ya Samadi. Macho yamejaa tongo tongo kama usaha,” Aliwaza.
“Nikachukua jukumu la kukulisha, kukupaka mafuta ya kukunenepesha na kunawilisha mwili wako. Leo hii unang’ara kama Jua, leo hii umenenepa kama Tembo, leo hii umeukacha ule ushamba wako wa Porini, ajabu! Taaratibu taaratibu unanisusa kisiri siri, umeona wacha unisaliti, umeona sio mbaya kuwa na mtu mwingine pembeni, umefikia hatua ya kunitema mfano wa bigi ji inayotemwa kwa maonjesho ya utamu wa karanga,”
“No way, sikubali wala sikubaliani na matendo ambayo umefikia hatua ya kunifanyia. Kwa pupa zako wataka mie niamini maneno ya wahenga waliposema heri kumfadhiri mbuzi atakupa nyama, kuliko kumfadhiri binadamu atakaye kutia aibu na fedhea. Sawa, Sina mengi ya kuongeza nilazima nitawakomesha ili mjue kuwa sihitaji michezo iliyopitwa na wakati.”
Mawazo yalimsumbua Mzee wa watu, mawazo yalimsumbua usiku na mchana, yalimsumbua asitake kumwambia Tunu au mwanae Ally juu ya donda linalo muumiza, donda linalo geuza geuza akili zake, akachomoka kutoka kwenye pembe ya kijumba nyasi chake, ameshikilia mkongojo, Koti lake lenye rangi nyeusi ametupia juu ya mabega, kanzu yake chakavu mwilini imeambatana na baraka shea yake chakavu kichwani, akajikongoja kongoja, akawapita hawa wawili waliokua ndani ya bustani ya mboga mboga, wamesimama wana ongea kwa raha zao .
Tunu na Ally walimwona Mzee Jamali akichomoza pale alipojibanza akielekea ndani ya kijumba nyasi chao.Tunu alieleka kumpokea mumewe riziki aliyokuja nayo siku ile, Ally kijana wa pekee kwa Mzee Jamali, aliendelea kupalilia mboga mboga bustanini.
Ally ana umri wa miaka ishirini na mitano, wakati Tunu ambaye kwa sasa ndie ***** Ally, mama wakufikia, mama wa kambo. Anakaribiana kidogo na umri wa Ally, yeye ana umri wa miaka ishirini na mitatu bado angali ni binti mdogo mwenye wingi wa furaha na tabasamu, tabasamu lake zuri kama Mauaridi, macho yake makubwa mazuri kama mtoto mdogo mwenye umri wa miaka mitano, nywele za huyu binti ni nywele za asili ndefu, nzuri, zimechanua mfano wa Ua Jasimini.
“Habari za kazi mume wangu?” Tunu alimsabahi Mzee Jamali, tayari Keisha kumpokea ile riziki ya siku ile.
“Salama mama Ally, nina furaha kubwa kuwakuta mkiwa salama salimini.” Mzee Jamali alijibu akilazimisha tabasamu la kinafiki limtoke mdomoni mwake akijua kwamba bado ni mwenye hasira juu ya ule uhusiano ambao yeye anahisi kuwa Tunu na mwanae Ally wameujenga.
“Pole sana baba Ally, pole mume wangu, pole kwa majukumu mazito ya kila siku.” Tunu alimfariji mumewe wakati huo huo Tunu amekwisha kuchukua kitenge chake alichojifunika kiunoni akalifuta jasho lililokuwa limesheheni juu ya paji la uso wa mumewe kwisha kumaliza kumfuta jasho lilosheheni juu ya paji la uso wa mumewe Tunu akaikamata miguu ya mumewe akaifuta futa vumbi kwa kile kitenge chake, kwisha kuhakikisha kuwa mumewe ni safi Tunu akalichukua koti la mumewe kwa lengo la kwenda kulihifadhi chumbani kwao kwa heshima zote Tunu alilitundika lile koti juu ya Msumari uliopo ndani ya chumba cha yeye na mumewe.
Akaelekea Jikoni, akakitwaa kibuyu kidogo kilicho jaa asali, tena akakitwaa kingine kilicho na maziwa fresh, akaeleka pale alipoketi mumewe. Tunu akafanya kumimina ile asali juu ya miguu ya mumewe, kulikua na beseni ambalo limemiminiwa maziwa. Basi Tunu akaanza kuiosha miguu ya mumewe kwa kuchanganya changanya ile asali na maziwa, kwisha kumaliza ile kazi Tunu alimfuta futa miguu mumewe, alimfuta futa kwa kile kitenge chake. Alihakikisha kuwa mumewe ni safi salama, Tunu alilitoa lile beseni akaenenda jahani kuumwaga ule mchanganyo wa maziwa na asali na baada ya hayo yote Tunu akaeleka Mekoni kumwandalia mumewe mlo wa mchana ule.
DONDA LA WIVU
👇
LEO MCHANA.
“Ni lazima niitishe kikao cha wazee wa Mila, ni lazima nipange siku moja maalumu kuwakomoa firauni hawa, wajinga na wapuuzi wanao yachezea maisha yangu ………… Nakwambieni Ally mpuuzi wewe nitakukomesha. Mwaka huu nitakukomoa ili uione dunia chungu, kama uchungu wa nyanya chungu, Ng’ombe we!” Mzee Jamali aliwaza yeye na moyo wake, amekasirika sana siku ya leo, hajapata kuwa na hasira kama alizonazo leo, kamwe hajapata kukasirika kama alivyokasirika leo, leo Shetani kamwingia, tena huyo Shetani kamshawishi afanye hima hima apate kumkomoa Ally mwanawe wa kumzaa.
“Ninatamani kumwaga damu, damu ya makafiri wapuuzi, wajinga, mafirauni nyie mnanihujumu mapenzi yangu.” Macho ya mzee Jamali yaliiva kwa hasira. kujibanza kwake nyuma ya kijumba nyasi haikutosha kuipunguza jaziba aliyokua nayo, hasira zilimpanda pale akimuona mkewe mpenzi Tunu binti mashallah! Amesimama na Ally mwanawe wa kumzaa, kila ikiwa leo hawana jambo la muhimu kujadili zaidi ya kutizamana machoni kama Ndege wawili mapenzini.
Hawana jambo lolote lile muhimu zaidi ya kunena nena vijimaneno ambavyo Mzee Jamali Mzee mwenye umri wa miaka sabini na ushee anahisi ndani ya fikara zake kuwa wawili hawa wanaongea juu ya mapenzi, mapenzi yao wenyewe, japo kwa usiri mkubwa ambao si Tunu wala si Ally aliyekua tayari kumweleza Mzee Jamali
“Tunu nilikutoa Kijijini kwenu ukiwa umeoza, unanuka, umeharibika. Miguu yako yote miwili ilikua imeoza na kuharibiwa na Funza, ambao kwa mikono yangu hii miwili nilikua radhi kuwachezea chezea hao Funza na kuwatoa miguuni kwako, ulikuja kijijini kwangu ukiwa umekonda haswa, umekonda kama gofu lililoachwa na Mkoloni, umekonda na kudhoofika, umekonda mifupa mifupa, umekonda kama Mnazi uliokosa mbolea ya Samadi. Macho yamejaa tongo tongo kama usaha,” Aliwaza.
“Nikachukua jukumu la kukulisha, kukupaka mafuta ya kukunenepesha na kunawilisha mwili wako. Leo hii unang’ara kama Jua, leo hii umenenepa kama Tembo, leo hii umeukacha ule ushamba wako wa Porini, ajabu! Taaratibu taaratibu unanisusa kisiri siri, umeona wacha unisaliti, umeona sio mbaya kuwa na mtu mwingine pembeni, umefikia hatua ya kunitema mfano wa bigi ji inayotemwa kwa maonjesho ya utamu wa karanga,”
“No way, sikubali wala sikubaliani na matendo ambayo umefikia hatua ya kunifanyia. Kwa pupa zako wataka mie niamini maneno ya wahenga waliposema heri kumfadhiri mbuzi atakupa nyama, kuliko kumfadhiri binadamu atakaye kutia aibu na fedhea. Sawa, Sina mengi ya kuongeza nilazima nitawakomesha ili mjue kuwa sihitaji michezo iliyopitwa na wakati.”
Mawazo yalimsumbua Mzee wa watu, mawazo yalimsumbua usiku na mchana, yalimsumbua asitake kumwambia Tunu au mwanae Ally juu ya donda linalo muumiza, donda linalo geuza geuza akili zake, akachomoka kutoka kwenye pembe ya kijumba nyasi chake, ameshikilia mkongojo, Koti lake lenye rangi nyeusi ametupia juu ya mabega, kanzu yake chakavu mwilini imeambatana na baraka shea yake chakavu kichwani, akajikongoja kongoja, akawapita hawa wawili waliokua ndani ya bustani ya mboga mboga, wamesimama wana ongea kwa raha zao .
Tunu na Ally walimwona Mzee Jamali akichomoza pale alipojibanza akielekea ndani ya kijumba nyasi chao.Tunu alieleka kumpokea mumewe riziki aliyokuja nayo siku ile, Ally kijana wa pekee kwa Mzee Jamali, aliendelea kupalilia mboga mboga bustanini.
Ally ana umri wa miaka ishirini na mitano, wakati Tunu ambaye kwa sasa ndie ***** Ally, mama wakufikia, mama wa kambo. Anakaribiana kidogo na umri wa Ally, yeye ana umri wa miaka ishirini na mitatu bado angali ni binti mdogo mwenye wingi wa furaha na tabasamu, tabasamu lake zuri kama Mauaridi, macho yake makubwa mazuri kama mtoto mdogo mwenye umri wa miaka mitano, nywele za huyu binti ni nywele za asili ndefu, nzuri, zimechanua mfano wa Ua Jasimini.
“Habari za kazi mume wangu?” Tunu alimsabahi Mzee Jamali, tayari Keisha kumpokea ile riziki ya siku ile.
“Salama mama Ally, nina furaha kubwa kuwakuta mkiwa salama salimini.” Mzee Jamali alijibu akilazimisha tabasamu la kinafiki limtoke mdomoni mwake akijua kwamba bado ni mwenye hasira juu ya ule uhusiano ambao yeye anahisi kuwa Tunu na mwanae Ally wameujenga.
“Pole sana baba Ally, pole mume wangu, pole kwa majukumu mazito ya kila siku.” Tunu alimfariji mumewe wakati huo huo Tunu amekwisha kuchukua kitenge chake alichojifunika kiunoni akalifuta jasho lililokuwa limesheheni juu ya paji la uso wa mumewe kwisha kumaliza kumfuta jasho lilosheheni juu ya paji la uso wa mumewe Tunu akaikamata miguu ya mumewe akaifuta futa vumbi kwa kile kitenge chake, kwisha kuhakikisha kuwa mumewe ni safi Tunu akalichukua koti la mumewe kwa lengo la kwenda kulihifadhi chumbani kwao kwa heshima zote Tunu alilitundika lile koti juu ya Msumari uliopo ndani ya chumba cha yeye na mumewe.
Akaelekea Jikoni, akakitwaa kibuyu kidogo kilicho jaa asali, tena akakitwaa kingine kilicho na maziwa fresh, akaeleka pale alipoketi mumewe. Tunu akafanya kumimina ile asali juu ya miguu ya mumewe, kulikua na beseni ambalo limemiminiwa maziwa. Basi Tunu akaanza kuiosha miguu ya mumewe kwa kuchanganya changanya ile asali na maziwa, kwisha kumaliza ile kazi Tunu alimfuta futa miguu mumewe, alimfuta futa kwa kile kitenge chake. Alihakikisha kuwa mumewe ni safi salama, Tunu alilitoa lile beseni akaenenda jahani kuumwaga ule mchanganyo wa maziwa na asali na baada ya hayo yote Tunu akaeleka Mekoni kumwandalia mumewe mlo wa mchana ule.