Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amesema Serikali kwa kushirikiana na Wadau itahakikisha inapaza sauti kuhusu mchezo wa Gofu ili umma upate uelewa kuhusu umuhimu wa mchezo huo Kitaifa na Kimataifa.
Amesema hayo Machi 26, 2023 Dar es Salaam katika hafla ya Gofu NBC Lugalo Open 2023.