Haikuwa Rahisi Said Kastico Kupewa Mtaa

Haikuwa Rahisi Said Kastico Kupewa Mtaa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
HAIKUWA RAHISI SAID KASTICO KUPEWA MTAA...KAMA KAWAIDA

Mtendaji wa Mwenge hakuwa kafurahia sana Mzee Said Kastico kuadhimishwa.

Ugomvi ukatokea hadi ukafika kwa Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya.

Ukoo wa Mzee Kastico wala hawakuomba mzee wao apewe mtaa bali wananchi wenyewe katika mkutano walipendekeza Mzee Said Kastico apewe mtaa na wakachagua mtaa unaopita nyumbani kwake.

Wanae wakaombwa wachangie shilingi 320,000.00 na wakatoa fedha hizo.

Kilichofuatia baada ya kulipa hizo fedha ni Mtendaji kukaa kimya kwa wiki tatu na alipofuatwa kuulizwa kulikoni akajibu kuwa fedha zimekawia kulipwa na mtaa huo wa Said Kastico akapewa mtu mwigine jina lake Chilumba.

Baada ya kidonda ukafuatia msumari wa moto Mtendaji akasema kuwaambia watoto wa Said Kastico kuwa wanaweza kwenda kokote.

Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya akaomba ushahidi kuwa watoto wa Said Kastico hawakutoa ushirikiano wa kutosha kwa baba yao kuadhimishwa.

Ikaamuliwa Mzee Said Kastico apewe mtaa mwingine si ule wa kwanza pale mtaani kwake alipoishi.

Ikawa kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Said Kastico rafiki ya baba yangu akapata mtaa.

Screenshot_20220809-042422_WhatsApp.jpg
 
Vitu vingine vidogo sana ila tatizo ni kamati za maendeleo za kata, yani diwani, Afisa mtendaji kata na wenyeviti wa mitaa ya kata husika, tatizo liko hapo na si vinginevyo.
 
Huyu Said Kastico ni muislamu?

Na alinyimwa mtaa kwa sababu ya dini yake?
 
Vitu vingine vidogo sana ila tatizo ni kamati za maendeleo za kata, yani diwani, Afisa mtendaji kata na wenyeviti wa mitaa ya kata husika, tatizo liko hapo na si vinginevyo.
Ni kweli, jambo dogo kama hilo linaweza kukuzwa na kusababisha sintofahamu ambayo si ya msingi kabisa, tena likipata Watu wa kuupamba huo mvutano.
 
Huyu Said Kastico ni muislamu?
Na alinyimwa mtaa kwa sababu ya dini yake?
Bila...
Said Kastico ni Muislam.
Hakunyimwa mtaa wakazi wa mwenge walikubaliana kumpa mtaa hapo alipokuwa anaishi wakati wa uhai.

Wanae wakaambiwa wachangia fedha kukamilisha zoezi na wakatoa.
Ghafla pakawa kimya.

Walipokwenda kuuliza wakaambiwa na Mtendaji kuwa huo mtaa aliopewa baba yao kapewa mtu mwingine anaitwa Chilumba.
 
Ni kweli, jambo dogo kama hilo linaweza kukuzwa na kusababisha sintofahamu ambayo si ya msingi kabisa, tena likipata Watu wa kuupamba huo mvutano.
Plato...
Kuna watu ndani ya serikali wanadhani wao wana haki kuliko wenzao.
Linapokuja jambo ambalo litaakisi mathalan wenzao wao hawawezi kustahamili lazima watafanyia hujuma.

Hakuna mtu katika sisi tunaoijua historia ya Julius Nyerere ambae hajui uhusiano uliokuwapo baina ya Mshume Kiyate na Julius Nyerere.

Mzee Mshume alikuwa moja ya nguzo aliyoegemea Mwalimu Nyerere.
Katika miaka ya 1990s Mzee Mshume alipewa mtaa kwa mchango wake wa kupogania uhuru wa Tanganyika.

Hadi hii leo kibao hakijawekwa sasa zaidi ya miaka 30.

Huyo hapo chini Mshume Kiyate na Mwalimu Nyerere picha hii ilipigwa mwaka wa 1964 baada ya maasi ya Tanganyika Rifles.
1660054851963.jpeg
 
Plato...
Kuna watu ndani ya serikali wanadhani wao wana haki kuliko wenzao.
Linapokuja jambo ambalo litaakisi mathalan wenzao wao wao hawawezi ustahamili lazima wataifanyia hujuma.

Hakuna mtu katikasisi tunaoijua historia ya Julius Nyerere ambae hajui uhusiano uliokuwapo baina ya Mshume Kiyate na Julius Nyerere.

Mzee Mshume alikuwa moja ya nguzo aliyoegemea Mwalimu Nyerere.
Katika miaka ya 1990s Mzee Mshume alipewa mtaa.

Hadi hii leo kibao hakijawekwa sasa zaidi ya miaka 30.

Huyo hapo chini Mshume Kiyate na Mwalimu Nyerere picha hii ilipigwa mwaka wa 1964 baada ya maasi ya Tanganyika Rifles.
View attachment 2319218
Bado nafasi ipo Kwa viongozi kulifanyia kazi
 
Plato...
Kuna watu ndani ya serikali wanadhani wao wana haki kuliko wenzao.
Linapokuja jambo ambalo litaakisi mathalan wenzao wao hawawezi kustahamili lazima watafanyia hujuma.

Hakuna mtu katika sisi tunaoijua historia ya Julius Nyerere ambae hajui uhusiano uliokuwapo baina ya Mshume Kiyate na Julius Nyerere.

Mzee Mshume alikuwa moja ya nguzo aliyoegemea Mwalimu Nyerere.
Katika miaka ya 1990s Mzee Mshume alipewa mtaa kwa mchango wake wa kupogania uhuru wa Tanganyika.

Hadi hii leo kibao hakijawekwa sasa zaidi ya miaka 30.

Huyo hapo chini Mshume Kiyate na Mwalimu Nyerere picha hii ilipigwa mwaka wa 1964 baada ya maasi ya Tanganyika Rifles.
View attachment 2319218
Aisee!! Unafikiri Mzee kanyimwa jina la mtaa kwa sababu gani mahsusi?
Kwa sababu kuna Mzee maarufu sana mtaa mmoja Dodoma lakini mtaa amepewa Aboud Jumbe.
 
Aisee!! Unafikiri Mzee kanyimwa jina la mtaa kwa sababu gani mPlatousi?
Kwa sababu kuna Mzee maarufu sana mtaa mmoja Dodoma lakini mtaa amepewa Aboud Jumbe.
Plato...
Tujadili hili la Said Kastico wa Mwenge kwanza kisha tuingie la Dodoma.
Mtendaji kaeleza kuwa walichelewa lakini ikagundulikana kuwa si kweli.
 
HAIKUWA RAHISI SAID KASTICO KUPEWA MTAA...KAMA KAWAIDA

Mtendaji wa Mwenge hakuwa kafurahia sana Mzee Said Kastico kuadhimishwa.

Ugomvi ukatokea hadi ukafika kwa Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya.

Ukoo wa Mzee Kastico wala hawakuomba mzee wao apewe mtaa bali wananchi wenyewe katika mkutano walipendekeza Mzee Said Kastico apewe mtaa na wakachagua mtaa unaopita nyumbani kwake.

Wanae wakaombwa wachangie shilingi 320,000.00 na wakatoa fedha hizo.

Kilichofuatia baada ya kulipa hizo fedha ni Mtendaji kukaa kimya kwa wiki tatu na alipofuatwa kuulizwa kulikoni akajibu kuwa fedha zimekawia kulipwa na mtaa huo wa Said Kastico akapewa mtu mwigine jina lake Chilumba.

Baada ya kidonda ukafuatia msumari wa moto Mtendaji akasema kuwaambia watoto wa Said Kastico kuwa wanaweza kwenda kokote.

Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya akaomba ushahidi kuwa watoto wa Said Kastico hawakutoa ushirikiano wa kutosha kwa baba yao kuadhimishwa.

Ikaamuliwa Mzee Said Kastico apewe mtaa mwingine si ule wa kwanza pale mtaani kwake alipoishi.

Ikawa kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Said Kastico rafiki ya baba yangu akapata mtaa.

View attachment 2318640
Hiyo fedha waliyotoa Ni ya Nini ?
 
HAIKUWA RAHISI SAID KASTICO KUPEWA MTAA...KAMA KAWAIDA

Mtendaji wa Mwenge hakuwa kafurahia sana Mzee Said Kastico kuadhimishwa.

Ugomvi ukatokea hadi ukafika kwa Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya.

Ukoo wa Mzee Kastico wala hawakuomba mzee wao apewe mtaa bali wananchi wenyewe katika mkutano walipendekeza Mzee Said Kastico apewe mtaa na wakachagua mtaa unaopita nyumbani kwake.

Wanae wakaombwa wachangie shilingi 320,000.00 na wakatoa fedha hizo.

Kilichofuatia baada ya kulipa hizo fedha ni Mtendaji kukaa kimya kwa wiki tatu na alipofuatwa kuulizwa kulikoni akajibu kuwa fedha zimekawia kulipwa na mtaa huo wa Said Kastico akapewa mtu mwigine jina lake Chilumba.

Baada ya kidonda ukafuatia msumari wa moto Mtendaji akasema kuwaambia watoto wa Said Kastico kuwa wanaweza kwenda kokote.

Msaidizi wa Mkuu wa Wilaya akaomba ushahidi kuwa watoto wa Said Kastico hawakutoa ushirikiano wa kutosha kwa baba yao kuadhimishwa.

Ikaamuliwa Mzee Said Kastico apewe mtaa mwingine si ule wa kwanza pale mtaani kwake alipoishi.

Ikawa kheri nusu shari kuliko shari kamili.

Said Kastico rafiki ya baba yangu akapata mtaa.

View attachment 2318640
Samahani maalim, huyu marehemu kastico ana undungu na Maudline kastico wa CCM?
 
Vitu vingine vidogo sana ila tatizo ni kamati za maendeleo za kata, yani diwani, Afisa mtendaji kata na wenyeviti wa mitaa ya kata husika, tatizo liko hapo na si vinginevyo.
bi mkubwa wangu alipewa mtaa dah lilizuka zengwe hadi mkutano wakaitisha.familia waliokuwepo wakasusa kwenda ktk mkutano.jina likaondolewa
 
Ni kweli, jambo dogo kama hilo linaweza kukuzwa na kusababisha sintofahamu ambayo si ya msingi kabisa, tena likipata Watu wa kuupamba huo mvutano.
mkuu mie niliona mvutano wa bi mkubwa kupewa mtaa.lilizuka zengwe mtaani utadhani kodi wataanza kumpa bi mkubwa.
 
mkuu mie niliona mvutano wa bi mkubwa kupewa mtaa.lilizuka zengwe mtaani utadhani kodi wataanza kumpa bi mkubwa.
Kwa maelezo yako itakuwa ni suala la kimtaa tu. Anachojaribu kukieleza hapa Mzee MS ni kama aliyemtaja kanyimwa kwa sababu ya dini yake! Kama kila mtu akifungua uzi kuhusu flani kunyimwa jina la mtaa utaona itakuwa malalamiko mengi sana
 
Back
Top Bottom