Haiwezekani Wasabato kuhubiri neno la Mungu bila kutaja Kanisa Katoliki? Au ni mafunuo? au mbinu za kupata na kutunza wafuasi?

Alafu hata hawajibiwi.

Inauma sana ukijipanga kwa vita kwa silaha kibao alafu adui yako anakudharau.
Unajibu nini takataka? Kanisa lina experience ya kupingwa kwa kila aina ya hoja tangu linaanza 33 A.D mpaka leo, limepitia kila kipindi, hao ni wadogo sana, limepangua hoja kibao za maana, mfano Utatu Mtakatifu, Umungu wa Yesu, Bikira Maria kuwa mama wa Mungu, kuhukumiwa na tawala ya Rumi, leo ndio vinuka mkojo vya 1800 na kitu vitusumbue kweli? Tunafocus kwenye mambo yetu ya msingi yanayotujenga kiroho na kimwili sio upupu huo.
 
Ukweli ni kwa sababu mosi,wakatoliki wengi hawana uelewa na dini,pili ni ngumu kutetea ukatoliki kwa kutumia bible, ukatoliki kwenye bible wamemchukua yesu tu na mama yake mengine wamebuni nje ya bible
 
Kuna wanaojitekenya wenyewe kuwa Kanisa lao ni la Mitume!

Neno “Katoliki” linatokana na neno la Kiyunani katholikos, linalomaanisha "ulimwengu mzima" au "wa wote." Lilitumika kwa mara ya kwanza na Mtakatifu Ignatius wa Antiokia mwanzoni mwa karne ya 2 (takriban mwaka 110 BK) kuelezea Kanisa la Kikristo kwa ujumla wake. Hii inaonyesha kwamba hata katika kipindi hicho, kulikuwa na hisia ya Kanisa kama jamii moja iliyoungana, inayowakilisha waamini wote.

Ingawa Kanisa Katoliki la Roma kama taasisi lilianza kuwa na muundo wa kikanuni baada ya Konstantino kuhalalisha Ukristo mwaka 313 BK (Tamko la Milan).

Usabato bila Ukatoliki hauwezi kuwepo maana yote yanayofanyika yalianzishwa na Katoliki..
 
Katika Wasabato Mchungaji ambaye anahubiri angalau waweza muelewa ni Pastor Mbaga pekee,huyu anamhubiri Kristo hana muda wa kukashfu wengine.
 
Maelezo marefu bila kujibu hoja ya Msingi

Hata hivyo Kanisa Katoliki haijawahi kutamka kuwa Sabato ni Jumapili hata siku moja na haijawahi Fanya juhudi kuhadaa ulimwengu

RC wao wameamua kuabudu Jumapili kwani ni siku alipofufuka Kristo mwana wa Mungu aliye hai

Nyie endeleeni kuabudu sabato yenu hakuna aliyewazuia


Kuhusu watakatifu wapo wa kutosha duniani:

Salamu kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu.[a] Mimi ni mtume kwa sababu Mungu mwenyewe alitaka.

Kwa watakatifu wa Mungu walioko katika mji wa Efeso, waamini walio wa Kristo Yesu

Zab 16:3

Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.

1 Wakorintho 1:1-11:13
Neno: Bibilia Takatifu
1 Kutoka kwa Paulo, aliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Yesu Kristo, na Sosthene ndugu yetu.

2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wote waliota kaswa katika Kristo Yesu, wakaitwa wawe watakatifu, pamoja na wengine wote ambao kila mahali wanalikiri jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wao na Bwana wetu. 3 Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
 
Siku ya saba ni Jumamosi,kwa mujibu wa Mungu au Kalenda? Au Mungu alianza kuumba dunia siku gani? What if alipumzika Jumatatu, Jumanne,Jumatano au Alhamisi inamaana wao wanakosea? Maana wakati dunia imeumbwa kulikuwa hamna kalenda.
 
Huwezi kuelewa hayo Kwa sababu bichwa lako limeegemea kwenye miujuza.

Dhehebu pekee hapa Duniani lililofanikiwa kuijua Siri ya unabii ya vitabu VYA Ufunguo na Daniel, ni Wasabato.

RC viongozi wanaujua huo unabii ila wanajitoa ufahamu tu
Nasadiki kwa Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume", period

Na ndiyo dini ya ukweli ya Ukristu ambayo ilianzishwa na Mtume Petro alipokabidhiwa kondoo awachunge na Bwana Yesu Kristu (Mathayo 16:18). Wengine wote ni waprotestanti na wapinga kristo.

Wasabato siyo DHEHEBU LA KIKRISTU bali ni CULT (Itikadi) iliyoanza baada ya Nabii wa Uwongo kushindwa utabiri wake juu ya mwisho wa Dunia kuwa ni mwaka 1844
 
Wewe umechanganyikiwa. Hakuna unalolojua.

Dhehebu la SDA kwa sababu lilianzishwa kwa ulaghai, hiyo laana ya ulaghai ndiyo itakayoliongoza dhehebu hilo.

SDA ilianzishwa mwaka 1863 na watu watatu Joseph Bates, James White na mkewe Hellen White, baada ya unabii wa William Miller. kuwa eti mwisho wa Dunia ungekuwa October 22 mwaka 1844, kutokutokea.

Mwisho wa Dunia Ilipokosa kutokea, wakawadanganya wafuasi wajinga kuwa eti mmojawapo ametokewa na malaika njiani wakati anaenda shambani, na malaika huyo akamwambia kuwa eti ile siku waliyotegemea ungetokea mwisho wa Dunia, Yesu alienda mbingu ya 7. Toka hapo ikawa ni ulaghai mtupu mpaka leo.

SDA imeanza mwaka 1863, kama wao tu ndiyo wapo sahihi, ina maana hata mitume waliokuwa wanasali siku ya BWANA, siku ya kumega mikate, hawakuwa wanamwabudu Mungu wa kweli???
 
Siku ya saba ni Jumamosi,kwa mujibu wa Mungu au Kalenda? Au Mungu alianza kuumba dunia siku gani? What if alipumzika Jumatatu, Jumanne,Jumatano au Alhamisi inamaana wao wanakosea? Maana wakati dunia imeumbwa kulikuwa hamna kalenda.
Kama Bado hujui hata siku ya Saba ni lini hili inathibitisha hata ukatoliki wenyewe umeubaka tu yaani hujui.


Kila mwaka tunaazimisha pasaka na pasaka lazima iwe jpili ukisoma injili ya mathayo,Marko na Luka inasema wazi jpili ni siku ya kwanza ya juma.

Sasa Anza kuhesabu kuanzia jpili Hadi jmos utapata jibu.


Sisi tunataka kujifunza nimewahi muuliza paroko Tena sio mmoja alinijibu vzr tu kuwa kanisa lilibadiisha utukufu wa jmos na kuleta jpili kwenye mithali Ile mikubwa imeandikwa hii ukurasa wa372 kama sijakosea.

Kanisa liliona ibada iwe siku aliyo fufuka yesu.
 
Nipe hilo neno Jumapili siku ya kwanza ya juma? Je nakuuliza Mungu alianza kuumba dunia Jumapili...... na imeandikwa wapi.... hujanijibu mpaka sasa.

Huyo Paroko umemuuliza peke yako,si wengine tunao kwenye familia zetu.

Achana na Paroko nipe andiko linalosema Mungu kaanza kuumba dunia Jumapili...... Mimi nikisoma Mwanzo ,Mungu aliumba dunia na siku ya Saba akapumzika........ hawajasema alianza kuumba lini.

Halafu hivi kwa mfano mtu akiamua siku ya kufanya ibada kwake iwe jumatano, huku akiizishika na kuziishi amri za Mungu,vipi huyu hato muona Mungu.
 
Kwenye akili Yako toa neno jpili weke siku ya kwanza,pili,tatu nk.

Baada hapo kabishane na familia yako. Kwa mujibu wa biblia siku ya kwanza ya juma ni jpili.


Sasa ni rasmi kabishane na mke wako.
 
Kwenye akili Yako toa neno jpili weke siku ya kwanza,pili,tatu nk.

Baada hapo kabishane na familia yako. Kwa mujibu wa biblia siku ya kwanza ya juma ni jpili.


Sasa ni rasmi kabishane na mke wako.
Yameandikwa wapi siku ya kwanza ni Jumapili au labda nyie mna biblia ya kwenu peke yenu.

Sasa mbona mkali weka reference na sio kuzusha na kuungaunga.Mara ohooo kuna Paroko na ongea nao sasa ukiongea nao ndio inakuwaje,si wengine tumesoma nao.......... Mara ohooo mimi mkatoliki mbarikiwa kwa hiyo ukiwa mkatoliki then what.......

Halafu hivi kwa mfano mtu akiamua siku ya kufanya ibada kwake iwe jumatano, huku akiizishika na kuziishi amri za Mungu,vipi huyu hato muona Mungu.
 
Maandiko siyo Simba na yanga kuwa ni ushabiki tu kusoma nao sio issue hata sisi tumesoma nao vilevile.

Msabato Hana biblia Wala hatungi biblia .Biblia zote zinatungwa na katoriki wao wananunua tu.

24 Siku ya Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake wali chukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa wakaenda kaburini. 2 Wakakuta jiwe limeondolewa kwenye mlango wa kaburi. 3 Lakini walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu. 4 Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hilo, ghafla, watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayong’aa sana, wakasimama karibu nao

Soma Kwa biblia Yako
 
Mbona unakuwa kituko,Okay Kuna sehemu uliyo andika inasema Mungu alipumzika siku ya Saba (Jumamosi),kuna sehemu inaonyesha tunatakiwa kusali na kupumzika hiyo Jumamosi ya Sabato au kuna sehemu kwenye hicho ulicho kiandika kinasema Jumapili ni siku ya kwanza ambayo Mungu alianza uumbaji.

Halafu biblia haikutungwa na Katoliki, yaani unaendelea kutoa maboko. Bali Wakatoliki walikusanya hivyo vitabu vilivyo andikwa na mitume na manabii wa Mungu na kuvipangilia kwenye mtiririko. Ila hamna mkatoliki aliye tunga biblia,biblia ni ujumbe wa Mungu kupitia kwa Manabii na Mitume ili uwafikie watu wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…