NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Kila kitabu na zama zake , Haji Manara alikua moto sana kipindi anashindana na Murro wakati Haji akiwa Simba sc na Muro akiwa msemaji wa Yanga hakika nilishuhudia na kusikia maneno yenye mbwembwe na kejeli humo humo ndani yake hakika gemu ilichangamka mno tena mno na hiyo yote kwa kua walikua wanaendana.
Kwa sasa Manara karudi ni kama vile Leonel Mess arudi laliga bila ya Ronaldo kisha aanze kushindana mwenywe pasipo kuwa na upinzani huo ni mfano simaanishi kuwa Manara ni mkali sana la hasha bali nasema Manara zama zake zimepita sasa atafute shughuli zingine pale Yanga mambo ya usemaji amuachie Ally Kamwe.
Naambatanisha sababu kuu maalumu za kusema kuwa Haji Manara apumnzike na kumuachia Ally Kamwe
(1) Wakati wake umekwisha, nilimtazama Manara mwananchi day kwa jicho la tatu niligundua jamaa anafosi tu lakini hakuna kitu, Ally Kamwe alishawaandaa mashabiki na tayari wamemuelewa kurudi kwa Manara ni kama vile kaja kuanza kutengeneza upya .
Mbwembwe za Ahmedy Ally na Ally Kamwe zimeendana na ndiyo kitabu kipya kwenye soka la bongo na siyo haji Manara kuja kubishana na Ahmedy Ally ni vitu viwili tofauti kwa ufupi Manara kitabu chake kimepita amuachie Alli Kamwe.
(2) Manara anafanya kazi kwa kisasi, hili lipo wazi jamaa anafanya kazi kwa kulipiza kisasi tena mambo yake binafsi anayoyajua mwenyewe huko alikotoka sasa hii siyo nzuri katika taasisi kubwa kama Yanga akiropoka neno ni kama yanga ndiyo imeropoka na inakua haileti picha nzuri kwa viongozi wa yanga na taasisi nzima, kwa hili amuachie bwana mdogo tu halina ubishi.
(3) Anapiga dili binafsi za kipuuzi na kitoto kupitia platform ya Yanga, labda mjinga tu ndiyo hakuelewa kwa nini hamisa alitajwa sana pale jukwaani na kuitwa apande juu avalishwe jezi ya yanga na azizi k hiyo ni biashara kati ya Hamisa na Haji na ndiyo maana Azam waliikata hawakutaka kuonesha upuuzi kama huo usiokuwa na faida kwao, kiufupi huo ni ujinga wa hali ya juu kufanyika kwenye jukwaa kubwa kama lile kisa tu mtu kabeba pesa ya maji ya kunywa ili amtaje taje mtu.
Natumia jukwaa hili kubwa la wanamichezo kufikisha ujumbe huu kwa viongozi wa Yanga sc kuwa wamtafutie Haji Manara kazi nyingine ya kufanya usemaji wamuache bwana mdogo Ally kamwe aendeleze gurudumu la kutuburudisha wanayanga kwani tunahitaji damu changa na vijana wabunifu kama Ally Kamwe.
Kwa sasa Manara karudi ni kama vile Leonel Mess arudi laliga bila ya Ronaldo kisha aanze kushindana mwenywe pasipo kuwa na upinzani huo ni mfano simaanishi kuwa Manara ni mkali sana la hasha bali nasema Manara zama zake zimepita sasa atafute shughuli zingine pale Yanga mambo ya usemaji amuachie Ally Kamwe.
Naambatanisha sababu kuu maalumu za kusema kuwa Haji Manara apumnzike na kumuachia Ally Kamwe
(1) Wakati wake umekwisha, nilimtazama Manara mwananchi day kwa jicho la tatu niligundua jamaa anafosi tu lakini hakuna kitu, Ally Kamwe alishawaandaa mashabiki na tayari wamemuelewa kurudi kwa Manara ni kama vile kaja kuanza kutengeneza upya .
Mbwembwe za Ahmedy Ally na Ally Kamwe zimeendana na ndiyo kitabu kipya kwenye soka la bongo na siyo haji Manara kuja kubishana na Ahmedy Ally ni vitu viwili tofauti kwa ufupi Manara kitabu chake kimepita amuachie Alli Kamwe.
(2) Manara anafanya kazi kwa kisasi, hili lipo wazi jamaa anafanya kazi kwa kulipiza kisasi tena mambo yake binafsi anayoyajua mwenyewe huko alikotoka sasa hii siyo nzuri katika taasisi kubwa kama Yanga akiropoka neno ni kama yanga ndiyo imeropoka na inakua haileti picha nzuri kwa viongozi wa yanga na taasisi nzima, kwa hili amuachie bwana mdogo tu halina ubishi.
(3) Anapiga dili binafsi za kipuuzi na kitoto kupitia platform ya Yanga, labda mjinga tu ndiyo hakuelewa kwa nini hamisa alitajwa sana pale jukwaani na kuitwa apande juu avalishwe jezi ya yanga na azizi k hiyo ni biashara kati ya Hamisa na Haji na ndiyo maana Azam waliikata hawakutaka kuonesha upuuzi kama huo usiokuwa na faida kwao, kiufupi huo ni ujinga wa hali ya juu kufanyika kwenye jukwaa kubwa kama lile kisa tu mtu kabeba pesa ya maji ya kunywa ili amtaje taje mtu.
Natumia jukwaa hili kubwa la wanamichezo kufikisha ujumbe huu kwa viongozi wa Yanga sc kuwa wamtafutie Haji Manara kazi nyingine ya kufanya usemaji wamuache bwana mdogo Ally kamwe aendeleze gurudumu la kutuburudisha wanayanga kwani tunahitaji damu changa na vijana wabunifu kama Ally Kamwe.