Haji Manara anapaswa kumuachia Ally Kamwe kuwa msemaji mkuu wa Yanga sc, kwa maana wakati wake umeisha (umepita)

Haji Manara anapaswa kumuachia Ally Kamwe kuwa msemaji mkuu wa Yanga sc, kwa maana wakati wake umeisha (umepita)

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Kila kitabu na zama zake , Haji Manara alikua moto sana kipindi anashindana na Murro wakati Haji akiwa Simba sc na Muro akiwa msemaji wa Yanga hakika nilishuhudia na kusikia maneno yenye mbwembwe na kejeli humo humo ndani yake hakika gemu ilichangamka mno tena mno na hiyo yote kwa kua walikua wanaendana.

Kwa sasa Manara karudi ni kama vile Leonel Mess arudi laliga bila ya Ronaldo kisha aanze kushindana mwenywe pasipo kuwa na upinzani huo ni mfano simaanishi kuwa Manara ni mkali sana la hasha bali nasema Manara zama zake zimepita sasa atafute shughuli zingine pale Yanga mambo ya usemaji amuachie Ally Kamwe.

Naambatanisha sababu kuu maalumu za kusema kuwa Haji Manara apumnzike na kumuachia Ally Kamwe

(1) Wakati wake umekwisha, nilimtazama Manara mwananchi day kwa jicho la tatu niligundua jamaa anafosi tu lakini hakuna kitu, Ally Kamwe alishawaandaa mashabiki na tayari wamemuelewa kurudi kwa Manara ni kama vile kaja kuanza kutengeneza upya .

Mbwembwe za Ahmedy Ally na Ally Kamwe zimeendana na ndiyo kitabu kipya kwenye soka la bongo na siyo haji Manara kuja kubishana na Ahmedy Ally ni vitu viwili tofauti kwa ufupi Manara kitabu chake kimepita amuachie Alli Kamwe.

(2) Manara anafanya kazi kwa kisasi, hili lipo wazi jamaa anafanya kazi kwa kulipiza kisasi tena mambo yake binafsi anayoyajua mwenyewe huko alikotoka sasa hii siyo nzuri katika taasisi kubwa kama Yanga akiropoka neno ni kama yanga ndiyo imeropoka na inakua haileti picha nzuri kwa viongozi wa yanga na taasisi nzima, kwa hili amuachie bwana mdogo tu halina ubishi.

(3) Anapiga dili binafsi za kipuuzi na kitoto kupitia platform ya Yanga, labda mjinga tu ndiyo hakuelewa kwa nini hamisa alitajwa sana pale jukwaani na kuitwa apande juu avalishwe jezi ya yanga na azizi k hiyo ni biashara kati ya Hamisa na Haji na ndiyo maana Azam waliikata hawakutaka kuonesha upuuzi kama huo usiokuwa na faida kwao, kiufupi huo ni ujinga wa hali ya juu kufanyika kwenye jukwaa kubwa kama lile kisa tu mtu kabeba pesa ya maji ya kunywa ili amtaje taje mtu.

Natumia jukwaa hili kubwa la wanamichezo kufikisha ujumbe huu kwa viongozi wa Yanga sc kuwa wamtafutie Haji Manara kazi nyingine ya kufanya usemaji wamuache bwana mdogo Ally kamwe aendeleze gurudumu la kutuburudisha wanayanga kwani tunahitaji damu changa na vijana wabunifu kama Ally Kamwe.
 
Kuna mmoja ni Afisa Habari wa Yanga na mwingine ni Msemaji wa Yanga sasa sijui unaelewa tofauti ya majukumu yao au napo itatulazimu kukuelewesha zaidi?

Kwamba management ya Yanga ni wajinga kuweka hivi vyeo vyenye majukumu tofauti?
 
hizo ni mbwembwe tu mzeee
Hapana, mbwembwe za nini wakati unapoajiri inatokana na Organisation Chart ya kampuni ambayo ndio imecreate hizo post na kuweka majukumu kwa kila post plus mshahara na kila kitu?

Huwezi kuajiri mtu pasi na organisational chart. Hata kama hamumpendi Manara i think uongozi unamhitaji kwa sababu wanazozijua wao kulingana na KPI anazopewa na labda anazidikia vizuri.
 
Kuna mmoja ni Afisa Habari wa Yanga na mwingine ni Msemaji wa Yanga sasa sijui unaelewa tofauti ya majukumu yao au napo itatulazimu kukuelewesha zaidi?

Kwamba management ya Yanga ni wajinga kuweka hivi vyeo vyenye majukumu tofauti?
Wakati haji yupo selo nani alikuwa akifanya majukumu yake?
 
Kuna mmoja ni Afisa Habari wa Yanga na mwingine ni Msemaji wa Yanga sasa sijui unaelewa tofauti ya majukumu yao au napo itatulazimu kukuelewesha zaidi?

Kwamba management ya Yanga ni wajinga kuweka hivi vyeo vyenye majukumu tofauti?
Manara anayaelewa kweli hata majukumu yake na mipaka ya majukumu yake?maana tunaona anafanya mpaka majukumu ya Rais wa yanga mpaka ya mdhamini mkuu pia anayafanya.
Kwa kifupi Manara hafai kuwa na cheo chochote kwenye taasisi kubwa kama yanga.
 
Mambo ya riziki sometimes you don't need to take this life too seriously

Manara anatafuta riziki na Ally kamwe the same .

So it is better kuwaacha wote waumege mkate.

Ikiwa the big boss Gsm anawakubali wote Sisi ni nani
 
Manara is in denial. Alichotarajia kukipata kimapokezi ni kinyume kabisa na alichokutana nacho.

Miaka 2 ya kukaa nje ya game yamedhihirishia game kuwa haikuwa ikimuhitaji Manara.

Manara had been obsolete for long lakini mazingira hayakumpa wasaa wakudhihirika u obsolesce wake mpaka pale alipofungiwa.

Manara yupo jopo moja na kina Mzee Magoma, hawataki kukubali kuwa wakati umebadilika na hawahitajiki tena.
 
... viongozi wa Yanga sc kuwa wamtafutie Haji Manara kazi nyingine ya kufanya usemaji wamuache bwana mdogo Ally kamwe aendeleze gurudumu la kutuburudisha wanayanga kwani tunahitaji damu changa na vijana wabunifu kama Ally Kamwe.
Anayelipia ngoma ndiye anayechagua wimbo

1723783370857.png
 
Kila kitabu na zama zake , Haji Manara alikua moto sana kipindi anashindana na Murro wakati Haji akiwa Simba sc na Muro akiwa msemaji wa Yanga hakika nilishuhudia na kusikia maneno yenye mbwembwe na kejeli humo humo ndani yake hakika gemu ilichangamka mno tena mno na hiyo yote kwa kua walikua wanaendana.

Kwa sasa Manara karudi ni kama vile Leonel Mess arudi laliga bila ya Ronaldo kisha aanze kushindana mwenywe pasipo kuwa na upinzani huo ni mfano simaanishi kuwa Manara ni mkali sana la hasha bali nasema Manara zama zake zimepita sasa atafute shughuli zingine pale Yanga mambo ya usemaji amuachie Ally Kamwe.

Naambatanisha sababu kuu maalumu za kusema kuwa Haji Manara apumnzike na kumuachia Ally Kamwe

(1) Wakati wake umekwisha, nilimtazama Manara mwananchi day kwa jicho la tatu niligundua jamaa anafosi tu lakini hakuna kitu, Ally Kamwe alishawaandaa mashabiki na tayari wamemuelewa kurudi kwa Manara ni kama vile kaja kuanza kutengeneza upya .

Mbwembwe za Ahmedy Ally na Ally Kamwe zimeendana na ndiyo kitabu kipya kwenye soka la bongo na siyo haji Manara kuja kubishana na Ahmedy Ally ni vitu viwili tofauti kwa ufupi Manara kitabu chake kimepita amuachie Alli Kamwe.

(2) Manara anafanya kazi kwa kisasi, hili lipo wazi jamaa anafanya kazi kwa kulipiza kisasi tena mambo yake binafsi anayoyajua mwenyewe huko alikotoka sasa hii siyo nzuri katika taasisi kubwa kama Yanga akiropoka neno ni kama yanga ndiyo imeropoka na inakua haileti picha nzuri kwa viongozi wa yanga na taasisi nzima, kwa hili amuachie bwana mdogo tu halina ubishi.

(3) Anapiga dili binafsi za kipuuzi na kitoto kupitia platform ya Yanga, labda mjinga tu ndiyo hakuelewa kwa nini hamisa alitajwa sana pale jukwaani na kuitwa apande juu avalishwe jezi ya yanga na azizi k hiyo ni biashara kati ya Hamisa na Haji na ndiyo maana Azam waliikata hawakutaka kuonesha upuuzi kama huo usiokuwa na faida kwao, kiufupi huo ni ujinga wa hali ya juu kufanyika kwenye jukwaa kubwa kama lile kisa tu mtu kabeba pesa ya maji ya kunywa ili amtaje taje mtu.

Natumia jukwaa hili kubwa la wanamichezo kufikisha ujumbe huu kwa viongozi wa Yanga sc kuwa wamtafutie Haji Manara kazi nyingine ya kufanya usemaji wamuache bwana mdogo Ally kamwe aendeleze gurudumu la kutuburudisha wanayanga kwani tunahitaji damu changa na vijana wabunifu kama Ally Kamwe.


Umedadavua vema...!

Na Kwakua Kila atakayekuja kuchangia hii hoja atasema namuunga mkono mtoa Mada.!


Naomba huu Uzi mods Wauhifadhi Kwa Marejeo, Waugonge Muhuri halafu Waufunge!

Kuna Nyakati Wana Yanga Akili huwa zinawarudia ee.! Sio kama alivyosema Manara kuwa Walibakiaga Wawili tu Wenyenazo.!
 
Mbona kazi ya Afisa habari na Msemaji ni tofauti kabisa.
Afisa habari haiishii kuisemea Clabu kwa mdomo tu.
Ni Bosi wa Habari zote za kwenye majarida na mitandaoni.

Msemaji ni muongeaji tu chini ya Afisa habari.
 
Back
Top Bottom