Haji Manara azimia mara mbili baada ya kipigo kutoka kwa Kaizer Chiefs

Haji Manara azimia mara mbili baada ya kipigo kutoka kwa Kaizer Chiefs

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Gazeti la Mwananchi limeripoti muda mfupi uliopita kuwa Msemaji wa Klabu Simba Haji Manara alizimia mara kufuatia kipigo cha bao 4 kwa bila kutoka kwa Klabu ya Kaizer Chief ya Africa Kusini

Inaarifiwa kuwa Msemaji huyo maarufu wa Wekundu wa Msimbazi hakuamini kuwa timu yake inaweza kufungwa kwa magoli mengi hivyo ukizingatia uimara na ubora wa kikosi cha Simba
===

ILIKUWA siku ngumu kwa Ofisa Habari wa Klabu ya Simba, Haji Sunday Manara baada ya kuzimia mara mbili katika hoteli ya Sky ambayo Simba ilikuwa imefikia jijini Johannesburg kufuatia kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa Kaizer Chiefs.

Manara alianza kujisikia vibaya mara baada ya kuwasili hotelini akitokea katika

Uwanja wa FNB ambako pambano hilo lilifanyika. Madaktari wa Simba walilazimika

kumpa huduma ya kwanza kwa saa zima msemaji huyo ambaye ni mtoto wa staa wa zamani wa Yanga, Sunday Manara

“Nimezimia mara mbili. Hali yangu ilikuwa mbaya nusura nife. Nina presha ya kushuka na mara nyingi huwa natumia chumvi kujiweka sawa. Hali yangu kwa sasa ni nzuri lakini huu mpira unaweza kutuua siku moja,” alisema Manara.

Simba ilikubali kichapo hicho na kujiweka katika mazingira magumu ya kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika huku pambano la marudiano likitazamiwa kufanyika Jumamosi kwenye Uwanja wa Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Advertisement
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Next time atakufa kabisaaa yaani [emoji38][emoji38]
 
Waliikimbia Yanga kwa mkapa, wakaenda kukutana na Yanga ya wazulu, dadeki 4g.
Kama kweli waliikimbia, basi game imepangwa kupigwa tena tarehe 03/07/2021 saa 11.00 jioni. Lazima mpira uchezwe uwanjani, hakuna kusingizia chochote eti kwa kuwa kuna wachezaji wamegomea kambi, kuna majeruhi wengi au kuna wenye kutumikia adhabu za kadi nyekundu na njano wengi. Game lazima lichezwe
 
Kama kweli waliikimbia, basi game imepangwa kupigwa tena tarehe 03/07/2021 saa 11.00 jioni. Lazima mpira uchezwe uwanjani, hakuna kusingizia chochote eti kwa kuwa kuna wachezaji wamegomea kambi, kuna majeruhi wengi au kuna wenye kutumikia adhabu za kadi nyekundu na njano wengi. Game lazima lichezwe
Sie hatuna tatizo na hilo ila tunawakumbusha tu Muda ni saa 11 jioni, sio ifike Muda huo halafu msiingize timu, muje muingize tena saa 1 jioni mtacheza na nyasi.
 
Sie hatuna tatizo na hilo ila tunawakumbusha tu Muda ni saa 11 jioni, sio ifike Muda huo halafu msiingize timu, muje muingize tena saa 1 jioni mtacheza na nyasi.
Inategemea na wenye mamlaka ya mpira. Ukienda muda ambao mamlaka haijakutaka na wala haijapeleka refarii, utacheza na nani, na mwamuzi atakuwa yupi?

Nani atahesabu muda wa kusubiri na kupuliza filimbi ya kumaliza game? Game ni tarehe 03/07/2021, hata kama kuna majeruhi na waliofukuzwa na waliosusia kambi, timu ije hivyo hivyo na waliobaki, hata kama wachezaji wa timu B, TFF inaruhusu, waje tu wacheze ili kuiokoa timu.

Heri kufungwa 6-0 kuliko kuteremshwa madaraja mawili
 
Mwandishi Eddo Kumwembe

IMG-20210517-WA0021.jpg
 
Hajji Manara ni Popoma tu kama yalivyo Mapopoma mengine pale mbumbumbu fc!

Akijifanya kuzimia tena, wasimmwagie maji! Badala yake wamcharaze tu viboko vya kutosha kwenye makalio yake! Halafu atazinduka tu. Shenzi kabisa yule.
 
Back
Top Bottom