Mjasiria Akili
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 823
- 372
Katika hali ya kushangaza wakati timu ya Simba ikitaabishwa na Mbeya City uwanja wa taifa hapo jana afisa habari wa timu hiyo Haji Manara na meneja wa timu Musa Mgosi walikua bize na karibu kabisa na timu ya Mtibwa hapa mjini Morogoro.
Juzi mwandishi mmoja wa blog alisema Manara kaonekana hoteli moja na baadhi ya viongozi wa Mtibwa huku Musa Mgosi akionekana na baadhi ya wachezaji wa Mtibwa timu akiokua akiicheza hapo nyuma.
Mnyetishaji wetu alipowauliza wachezaji wa Mtibwa kuhusu kuonekana na Mgosi mchezaji mmoja mwandamizi wa timu hiyo alionekana kumshangaa Mgosi kujipendekeza kwao na kujifanya anawapa hamasa kuelekea mechi yao na Yanga wakati haimhusu.
Aidha alipotafutwa mchezaji mwingine alikiri Mgosi kuwafuata na kuwapa salamu kutoka uongozi wa Simba eti wakiizuia Yanga kupata point 3 kuna mlungula utawafikia, makubwa haya!
Nae Haji Manara alipoulizwa kunani Morogoro huku Simba wakidondosha point kwa Mbeya City alishangaa na kumuuliza mnyetishaji amejuaje uwepo wake Morogoro wakati ni siri kati yake na viongozi "simbamtibwa" ili kupanga mkakati wa kuizuia Yanga.
Juzi mwandishi mmoja wa blog alisema Manara kaonekana hoteli moja na baadhi ya viongozi wa Mtibwa huku Musa Mgosi akionekana na baadhi ya wachezaji wa Mtibwa timu akiokua akiicheza hapo nyuma.
Mnyetishaji wetu alipowauliza wachezaji wa Mtibwa kuhusu kuonekana na Mgosi mchezaji mmoja mwandamizi wa timu hiyo alionekana kumshangaa Mgosi kujipendekeza kwao na kujifanya anawapa hamasa kuelekea mechi yao na Yanga wakati haimhusu.
Aidha alipotafutwa mchezaji mwingine alikiri Mgosi kuwafuata na kuwapa salamu kutoka uongozi wa Simba eti wakiizuia Yanga kupata point 3 kuna mlungula utawafikia, makubwa haya!
Nae Haji Manara alipoulizwa kunani Morogoro huku Simba wakidondosha point kwa Mbeya City alishangaa na kumuuliza mnyetishaji amejuaje uwepo wake Morogoro wakati ni siri kati yake na viongozi "simbamtibwa" ili kupanga mkakati wa kuizuia Yanga.