Haji Manara ni Mswahili anayecheza na akili za Waswahili wenzake

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,537
Reaction score
8,824
Sio uongo vilabu vya Simba au hata Yanga vina Waswahili wengi sana ambao % kubwa shule ni zero na wanacho penda ni kusikia wakikandiana, na kutambiana wachezaji, kutambiana makocha, ndo maana vijiwe vya mashabiki wa Simba na Yanga ambavyo almost asilimia 100 huwa ni waswahili swahili pale huwa ni kukandiana tu hakuna kingine wanacho jua na huwezi wakuta wanajadili hata Uwekezsji kwenye virabu vyao make hizo ni maada ambazo kamwe hawawezi hata ziongea kwa sekunde 7.

Mo ndo maana anawa buruza kwa sababu anajua mashabiki asilimia kubwa ni waswahili ambao shule ni hakuna.

Huyu sasa msemaji wa Simba ni Mtu mjanja mjanja mswahili anacheza na akili za waswahili wenzake, haiwezekani msemaji wa Clabu yeye kila siku ni mipasho kwa timu pinzani yaani huwezi kuta post zake zinazungumzia maendeleo ya Mpira wa Simba hapana yeye ni mipasho kwa Yanga, post zake kwenye page yake zimejaa mipasho tu. Huyu ndo MO anawataka wa aina hii waswahili, klabu za wenzetu huwezu kuta msemaji wa Clabu A anahangaika na mambo ya Clabu B make hayamuhusu ila huku Bonho kwa sababu ya aina ya mashabiki tulio nao uswahili ndo unaonekana dili.

Maendeleo ya soko hapa Tanzania yanarudiswa nyuma na aina za Mashabiki wa hizi virabu vikongwe, mashabiki waswahili ambao wanacho jua ni kufungana basi hawajui kingine. Ndo maana unakuta Mechi ya Simba lets say na JKT Oljoro utajuta Jezi zinazo uzwa pale ni za Yanga na Simba unajiuliza kulikoni?

Mashabiki wa Simba na Yanga ndo wanao rudisha nyuma soka la Tanzania, mashabiki waswahili vichwani zero kabisa.
 
Yaana huyo.Haji na manukato yake yaliyododa ndo anaharibu soka Mikia fc
Huyo popoma Haji ndo shida.
 
Kwa asili ya soka la Tanzania, Simba na yanga ndiyo nguzo za ligi yetu, tuna derby moja tu, bila kuongeza ushwahili mwingi Kama wa haji manara hakutakuwa na ushindani.

Jiulize utawashawishi vipi watu wajaze uwanja wa taifa (60,000+) bila uswahili na matani ya kutambiana?

Usije ukalinganisha soka la Ulaya na Tanzania, hatutawafikia waliko ila wacha na sisi tuburudike.


Haji manara atabaki kuwa mswahili mwenye ushawishi mkubwa Sana katika soka la Tanzania kwani anasaidia Sana Simba kupata mapato na kuongeza mashabiki.

Big up Bugatti, Haji S. Manara
 
Yes Uswahili
Sisi hatuigi sijui club za nje, sisi ni sisi uswahili watz ndio jadi yetu.. Usilete habari za watu wengine siyo kila kitu lazma tuige tunaweza kuwa na utaratibu wetu na wengne wakaiga pia
 
halafu
Sisi hatuigi sijui club za nje, sisi ni sisi uswahili watz ndio jadi yetu.. Usilete habari za watu wengine siyo kila kitu lazma tuige tunaweza kuwa na utaratibu wetu na wengne wakaiga pia
unakuta jinga kama hilo limepanga tandale hata masaki halijawahi fika nalo lishajiona lizungu..... hizi ndo jadi zetu ugomvi wa mbuzi tunauza ng'ombe
 
kwa kifupi,mtu mwenye tabia za β€œkiswahili” huwa wana mambo ya ajabu sana
 
halafu

unakuta jinga kama hilo limepanga tandale hata masaki halijawahi fika nalo lishajiona lizungu..... hizi ndo jadi zetu ugomvi wa mbuzi tunauza ng'ombe
Where is Tandale and where is Masaki fool?
 
Sisi hatuigi sijui club za nje, sisi ni sisi uswahili watz ndio jadi yetu.. Usilete habari za watu wengine siyo kila kitu lazma tuige tunaweza kuwa na utaratibu wetu na wengne wakaiga pia
Ili jibu ni mubashara kabisa.
 
Mswahili ni mtu yeyote mwenye asili ya mwambao wa afrika mashariki na siku hizi ni maana ya mswahili ni mtanzania anayeongea lugha ya kiswahili, hivyo basi tunajivunia kuwa waswahili
 
Wewe una mtizamo kama wangu. Ni kweli kabisa washabiki wa timu hizi wanaendekeza sana mipasho kuliko maendeleo ya vilabu. Weledi na ubunifu ni zero kabisa kwa viongozi
 
Mwalimu wa madrasa kawashika akili mbumbumbu
 
halafu

unakuta jinga kama hilo limepanga tandale hata masaki halijawahi fika nalo lishajiona lizungu..... hizi ndo jadi zetu ugomvi wa mbuzi tunauza ng'ombe
πŸ˜ƒπŸ€£πŸ˜ƒπŸ˜‚
 
Haji Manara hana ushawishi wowote kwenye klabu ya Simba au mpira wa Tanzania, Kinacho isaidia Simba ni MO kwakua ameweka fedha kwenye timu na timu inapata matokeo.
Mashabiki wa Simba na Yanga wanachotaka matokeo mazuri uwanjani. Timu Yao ikiwa inapata matokeo uwanjani watakuja kwa wingi mbaka utashangaa. Waulize mashabiki wa African sports na Cost pale Tanga wakati timu zao zikiwa kwenye ushindani hali ya Uwanja wa mkwakwani ilikuaje.
waulize mashabiki wa Tukuyu na Mecco za Mbeya hali ilikua inakuaje zikikutana pale Sokoine, Uliza Wana Tp lindanda wakati mtangazaji Marehemu Dominic Chilambo anakuelezea Hali ya Uwanja wa CCM kirumba wakati Pamba na Malindi wanakinukisha kutafuta bingwa wa Muungano,Angalia Mbeya City wakati inapata matokeo msimuwake wa kwanza pale Sokoine.
Mashabiki watakuja na watasafiri na timu inayo shinda tu.
Haji Manara alikua akiuza pafyum unajua Nini kilimtokea!! Anakesi ya Wizi wa kuaminika na pafyumu ziligoma kununuliwa. Kama ingekua ana ushawishi angeanza na pafyum zake kwanza. Angalia juzi aliposhindwa ku ujaza Uwanja na alidai watajaza viwanja viwili.
Simba na Yanga hazi itaji mpiga debe iyo hatua zilisha ivuka kitambo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…