Haka kamjengo kanaweza kugharimu shilingi Ngapi?

Kulingana na eneo ulilopo nadhani haizidi 2.5 million.
 
Hapo ni chumba na sebule, max ni tofali 1000 kuanzia msingi hadi juu, bati sita kila upande jumla 12, milango miwili, madirisha mawili, mbao 4×2 sita na 2×2 nane, mchanga Lori na kokoto nusu lori, cement mifuko 20, vitasa viwili, komeo mbili za ndani, misumari ya bati kilo2 na ya 4" kilo2, bawaba za milango 6, mafuta gharama yà kila kimoja hapo jumlisha usisahau hela ya fundi sijui vinasimamia ngapi vitu hivyo
 
Duuh
 
Tofali hapo ni 150-200 , mchanga lori 1 la tani 7, Cement mifuko 10, Bati 15-20 , mbao Laki 2 , misumari 15 000/- , milango na madirishana 120,000/- na ufundi 100,000/- . Ukijumlisha utajua ni Shs ngapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…