Sina nia ya kuharibu biashara ya mtu bali najaribu kuiokoa jamii ya Watanzania wenzangu na hasa watoto. Nimevumilia kwa muda mrefu kero ya tangazo hili la "Hakatwi Mtu Hapa"! tatizo langu ni pale ambapo unaonyeshwa wizi na utapeli wa wazi na kisha inaonekana kama ni jambo la kufurahisha na yule mama anaona mwenzake akiibiwa mkate na hachukui hatua zaidi ya kumaka tu "unaona?....", kwa kweli mimi sioni kama tangazo lile lina mantiki zaidi ya kufundisha na kushabikia wizi na utapeli. Kwani tumekosa ubunifu wa kutengeza matangazo yanayoashiria mambo positive ili kufikisha ujumbe? AG kazi yake kushupalia waandishi tu lakini hawa wengine wanabofoa wala hapeleki bill Bungeni! TCRA mpo?