Haki ya Mwanamke(msichana) na uhuru wake ambao anatakiwa aupate/aipate


IVUGA, sikukusudia wanaojiuza moja kwa moja, hawa kwa upande mmoja ninawaheshimu kwani angalau wanapambana na maisha; na kwa upande mwengine ninawahurumia kwani wengi wao hawafanyi hivi kwa kupenda, kama wakiwezeshwa kielimu na kimahitaji wanawacha.

Lakini niliowakusudia ni wale ambao ama peke yao au kwa kushirikiana na wanaume wanaendesha biashara ya ukahaba. Hawa wanakuwa "middle woman" au mameneja, wanamiliki maduka ya ngono na "wanasukuma" wasichana wadogo kuingia katika ukahaba. Sijui hili ninalozungumzia hapa litakuwa na ukweli kiasi gani kwa Tanzania, na nitafurahi kusikia kama bado halijafika, pia tujiandae kulizuwia. Huwa ninawaona wasichana wa Kiafrika hasa kutoka Afrika ya Kaskazini na Magharibi, Ulaya ya Mashariki, Asia na Amerika ya Kusini wakiwa wameingizwa bila ya ridhaa yao katika ukahaba. Wanalazimishwa kila siku walipe kiasi gani na wasipolipa wanachezea mkong'oto.
 

Mamamia hawa watu wa aina hii nawafahamu sana tu na hata mimi nishawahi kuwaona sana nilipokuwa ughaibuni ,na kwa hapa bongo nina uhakika wapo na ndio wanaoanzisha madanguro , sasa hawa wanawatumia hawa mabinti zetu ambao hawana means of income kwenye biashara yaani wao wameshidwa kuanzisha biashara nyingine zaidi ya madanguro. tatizo bado linakuja hapa kuwa tungemwelimisha mwanamke watua kama hawa wasingepata wasichana wa kwenda kuwauza na biashara ya ukahaba ingebakia kama interest ya mtu tu
 

tuko pamoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…