Haki za wafanyakazi zitazamwe upya

Haki za wafanyakazi zitazamwe upya

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,677
Kwa ufupi
"Hayo yalisemwa na Katibu wa kundi namba nne, Leokadia Vedastus huku akitaka katiba hiyo ijayo iongeze wigo wa haki za mfanyakazi ili aweze kulindwakikatiba."

Ukerewe. Wajumbe Baraza la Katiba Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, wamependekeza haki za wafanyakazi zitazamwe upya kwenye Katiba ijayo.
Hayo yalisemwa na Katibu wa kundi namba nne, Leokadia Vedastus huku akitaka katiba hiyo ijayo iongeze wigo wa haki za mfanyakazi ili aweze kulindwakikatiba.
Vedastus, alisema wamependekeza wigo wa haki za wafanyakazi uongezwe kwenye katiba kwa kutambua kuwa katiba ndio sheria mama ya nchi na sheria zote zinawajibika kwenye katiba hiyo.
Alisisitiza kuwa kwa haki hizo kuwepo kwenye Katiba kutaweza kumwongezea ulinzi mfanyakazi hivyo kuwafanya waweze kufanya kazi katika mazingira bora.
Alisema kwa muda mrefu haki nyingi za wafanyakazi zimekuwa hazitambuliki kikatiba hivyo kusababisha wafanyakazi wengi kunyimwa haki zao.
‘’Katiba Mpya ina wajibu wa kuongeza wigo wa haki za wafanyakazi, siyo kuishia kuwekahaki ya kufanya kazi pekee yake bila kuambatanisha haki zingine,’’alisema Vedastus.


Chanzo: MWANANCHI
 
Kwa ufupi
"Hayo yalisemwa na Katibu wa kundi namba nne, Leokadia Vedastus huku akitaka katiba hiyo ijayo iongeze wigo wa haki za mfanyakazi ili aweze kulindwakikatiba."

Ukerewe. Wajumbe Baraza la Katiba Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, wamependekeza haki za wafanyakazi zitazamwe upya kwenye Katiba ijayo.
Hayo yalisemwa na Katibu wa kundi namba nne, Leokadia Vedastus huku akitaka katiba hiyo ijayo iongeze wigo wa haki za mfanyakazi ili aweze kulindwakikatiba.
Vedastus, alisema wamependekeza wigo wa haki za wafanyakazi uongezwe kwenye katiba kwa kutambua kuwa katiba ndio sheria mama ya nchi na sheria zote zinawajibika kwenye katiba hiyo.
Alisisitiza kuwa kwa haki hizo kuwepo kwenye Katiba kutaweza kumwongezea ulinzi mfanyakazi hivyo kuwafanya waweze kufanya kazi katika mazingira bora.
Alisema kwa muda mrefu haki nyingi za wafanyakazi zimekuwa hazitambuliki kikatiba hivyo kusababisha wafanyakazi wengi kunyimwa haki zao.
‘’Katiba Mpya ina wajibu wa kuongeza wigo wa haki za wafanyakazi, siyo kuishia kuweka haki ya kufanya kazi pekee yake bila kuambatanisha haki zingine,’’ alisema Vedastus.

...nipitia RASIMU YA KATIBA MPYA, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977:
hii RASIMU YA KATIBA MPYA inamapungufu makubwa mno' walichofanya kwenye RASIMU ni ku- copy na ku-paste;
Haki ya kufanyakazi, na wafanyakazi na waajiri, sura ya nne, sehemu ya kwanza (34) na (35),
wameweka mambo ya CHAMA CHA WAFANYAKAZI yasiyo kuwa NA UMUHIMU wowote. Wakati KATIBA yetu YA MWAKA 77 ilikuwa imefafanua vizuri; Sura ya Kwanza, SEHEMU YA TATU (22) (23) (25)
...kwa maoni yangu; Kilichokuwa kinatakiwa ni kuhemu na kufuata maelekezo yaliyoko kwenye katiba yetu ya Mwaka 77, na kuboresha sheria mama na kanuni na haki za wafanyakazi, hasa zilezinazo husiana na wafanyakazi kwenye taasisi mbalimbali; kwa mfano
TRA (kuhusu % kiasi cha kodi na mambo ya matumizi ya TIN kwa wafanyakazi), mifuko ya hifadhi ya jamii, na sheria za kazi ziboreshwe, nk.
 
Back
Top Bottom