Hakika nimepoteza nguvu zangu bure

shirima Mathias

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2017
Posts
451
Reaction score
1,333
Zamani nilidanganywa kwa kuambiwa kuwa ukiwa na pesa utapata kila kitu, kweli nikapambana na nikafanikiwa kwa kiasi chake.

Ki ufupi nimewekeza kwenye biashara zisizofilisika. Na kwa siku napata laki nane hadi tisa (hiyo ni faida kwa kila siku).

Ila kinachonishangaza nimejikalia tuu nyumbani nacheza na kuku,mabata mzinga na kanga.

Kuna saa naweza kubeba milioni kama ishirini hivi nikazirusha zikasambaa chumbani ili angalau nipate kazi ya kuziokota na kuanza kuzihesabu tena.

Eti naweza kuwa nimelogwa? Au ni kawaida
 
[emoji28][emoji28][emoji28] aisee nimecheka saaaaana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…