Hakuna kama Mayele Tanzania

Smart codetz

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2023
Posts
218
Reaction score
875
🚨HAKUNA KAMA FISTON MAYELE
FISTON MAYELE tangu alipojiunga Yanga amecheza michezo 35 na kufunga mabao 43 katika michuano yote yakiushindani

Tangu MAYELE alipotua Tanzania hakuna mchezaji aliyefunga mabao mengi kumzidi yeye.Mayele amefunga mabao mengi kuliko mechi alizocheza.
 
Mayele anajua sio siri nina rafiki yangu ni simba damu damu ila anakuambia mayele analijua goli. Sina ushabiki lakini kwa kusikiliza redio tu nimemjua mayele ni mfungaji mzuri naamini kwa wanaojua mpira na sio washabiki maandazi lazima wamkubali mayele amefanya vizuri sana na anajua mpira.
 
Kwaio mayele amesha vunja rekodi zote za yanga?
1.Mohamed Hussein (mmachinga)
2.Henry Morris

Pale YANGA Kuna magwiji ya soka yamewai kupiga mwingi kuliko mayele....
Yanga wamewai kua klabu bingwa afrika mashariki na kati mara kadhaa....

Tunaomba ufafanuzi plz...
 
Hawa waandika record waache uongo jamani, mkiwa manokoteza virecord huko muwe mnatumikisha Kwanza Akili kabla ya kuokota tu mbio mbio mwisho wa siku unaonekana KIAZI

wote tunajua kuwa mayele ni mchezaji mzuri sana na anafunga sana tu ila hakuna haja ya kupika Data za uongo uongo ili tu tuzidi kumpaisha, anachofanya bado ni kizuri bila ata uongo

Msimu uliopita ambao mayele alikuwa mfugaji Bora namba 2 katika ligi kuu bara, alikuwa na Goli 16 katika mechi 30, je msimu huu kacheza mechi ngapi hadi hivi sasa kwenye ligi Kuu Peke yake tupo mechi ya 24?

Sasa iweje leo iwe kacheza mechi 35? Let's say mwaka jana kwenye ligi Peke yake amecheza mechi 30, bado michuano ya kimataifa na ya ndani

msimu huu tufanye kacheza mechi 15 japokuwa amecheza zaidi ya hizo, hayq jumlisha mechi za CAF champions League,CAF confederation cup,Azam confederation cup
 
Past tense...kwasasa gumzo la nchi ni Baleke
 
Msimu huu kacheza 36 mpaka sasa......
Ligi 21+FA 3 + Mabingwa 12.
Ila watu wanaongea vitu vya ajabu hapa.
 
Past tense...kwasasa gumzo la nchi ni Baleke
Sasa si Bora ata ingekuwa ni kweli mkuu, Record za kubumba bumba tu ilimradi waendelee kumpamba

Wanasahau kuwa msimu uliopita jamaa kacheza mechi 30 za ligi Kuu Pekee, sasa iweje leo awe kacheza mechi 35 tangu atue Tanzania?

Kiuhalisia jamaa amecheza zaidi ya mechi 60 tangu atue Tanzania tukianza na ligi Kuu msimu uliopita na huu, michuano ya kimataifa ya msimu uliopita na huu, michuano ya Azam confederation msimu uliopita na huu

Jamaa ni mchezaji mzuri sana ila too much hype, kwakuwa Yanga haikuwa na mfugaji mzuri karibia miaka 4 nyuma, jamaa angefanya aliyokuwa anafanya kagere sijui ingekuaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…