Hakuna mtu atakae kuambia fanya hiki au fanya kile utajirike kama yeye hatapata chochote kile kutoka kwako

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
Huu ndo ukweli ambao hutakaa uambiwe ila ni ukweli mtupu na iko hivyo.

Hakuna mtu atakae kuambia fanya hiki au fanya kile UTAJIRIKE au KINALIPA kama yeye hatapata chochote kile kutoka kwako.

Mimi nikija kukuhamasisha kufuga kuku jua nitauza vifaranga hilo ndo lengo kuu hiyo tajirika ni entry point tu.

Nikikuambia panda miti ya mbao utajirike baso jua nitakuuzia miche ya hiyo miti na mimi nitafaidika hapo.

Katika mazingira ya Kawaida sio rahisi mtu akuambie fanya kile utajirike kama yeye hatanufaika.

Ukiona anakuambia fanya kile utatoka na yeye hakifanyagi basi jua ana wrong information au alisha jaribu akapata hasara sasa anatafuta wafuasi au anataka kukutanguliza ili ajifunzie kwako.

Mengi hata siku moja kwenye mikutano yake ya kuhamasisha vijana wajiajiri huwezi sikia anakuambia anzisha kiwanda cha maji, anzisha kituo cha Radio au anzisha Gazeti.

AZAM hata siku moja hawezi kukuambia fungua kiwanda cha Juice au pika mandazi au mikate au anzisha biashara ya kupack maji.

Wengi huwa wanavutiwa na maneno mawili tu TAJIRIKA na INALIPA.

Watu wa Network Marketing huwa ni mabingwa wa kutumia TAJIRIKA ila sasa anaye kuamboa tajirika unakuta shati limepauka vibaya mno ila anakuhubilia tajirika. Ukiona hivyo jua yeye kuna namna atafaidika na wewe kuingia.
 
Tajirika na Inalipa huwa ni Urimbo wa kukamatia ndege. unaweka urimbo sasa unangojea ndege waje kutua ukamate
 
ndio formula ya maishamkuu,
''UKITAKA KULA LAIMA NA WEWE ULIWE'' Jk,mbona ni vitu reasonable kabisa mkuu,hivi ukiliwa moja ukala hamsini kuna tatizo gani? kawaida tuu kwenye ulimwengu wa fursa
 
Mtu anaandaa semina ya kulipia ya kufuga kuku wakati yeye hana kuku na hajawahi kufuga kuku.
Anaandaa semina ya kulipia ya kutengeneza sabuni wakati hajawahi kuteneza sabuni.
Hawa wazungumzaji(motivational speakers)na hivi sasa kila mtu utasikia ni mzungumzaji mimi ndio wananiacha hoi kabisa mtu hana hata biashara yoyote lakini anaandaa semina anafundisha watu jinsi ya kufanikiwa kwa kufanya biashara,kilimo ufugaji nk.
Na wengi wanaoibiwa fedha zao ni wasomi au wanafunzi wa elimu ya juu.
Kila siku yanaibuka madude ya ajabu ajabu kama bitcoin,forex nk.
 
ndio formula ya maishamkuu,
''UKITAKA KULA LAIMA NA WEWE ULIWE'' Jk,mbona ni vitu reasonable kabisa mkuu,hivi ukiliwa moja ukala hamsini kuna tatizo gani? kawaida tuu kwenye ulimwengu wa fursa
Sijui kama umenielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…