Hakuna sababu za ki "Demand & Supply" zinazosababisha bei ya kontena kupanda bandarini, tunapangwa?

Aramun

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2023
Posts
461
Reaction score
2,213
Ukiangalia supply and demand ya import and exports, utagundua wakati huu wa awamu ya 6 ambayo imeboresha mazingira ya uwekezaji, kama nchi tuna demand kubwa ya bidhaa kutoka nje.

Hivyo gharama za usafirishaji bidhaa kutoka nje zilitakiwa zishuke na siyo kupanda kwa sababu ndani kuna soko la uhakika, hivyo wanaoimport wana uhakika wa biashara na wanaleta mzigo wa kutosha.

Lakini maajabu ni kwamba tumeambiwa gharama za kusafirisha hizo kontena kuingia nchini zimeongeza mara 3 pale bandarini kutoka dola 3000 mpaka dola 9000.

Je, serikali kuna mahali inatupanga wananchi wake? Maana budget ya wizara ya fedha na mipango bado haijasomwa pale bungeni. Ni wanatafuta sababu ya kuleta makato mapya ama ni nini kinachopangwa na hawa wanasiasa wasiotujali sisi raia wa kawaida?

Your browser is not able to display this video.
 
Serikali haihusiki na usafirishaji uliopanda maana haimiliki meli, Kilichopanda NI freight charges ambazo hazihusiani na serikali,
 
Serikali haikupandisha bei yoyote, kilichopanda ni "freight" ambayo ni usafirishaji kutoka nje, yaani gharama za kusafirisha zimepanda kutoka nje. Tanzania haihusiki.

Wakulaumiwa na mazayuni, kimbembe wanachokifanya Wayemeni kuzuia meli za mazayuni kupita kando ya bahari yao maana yake meli zinazopita ni kidogo sana na makampuni ua bima yameziongezea bei, gharama siku zote zote zinarudi kwa mlaji.
 
Extremely dangerous indeed.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…