LGE2024 Hakuna umuhimu Wagombea kuwachezesha vigoma Dada zetu mnapoenda kuchukua au kurejesha fomu. Huu ni udhalilishaji

LGE2024 Hakuna umuhimu Wagombea kuwachezesha vigoma Dada zetu mnapoenda kuchukua au kurejesha fomu. Huu ni udhalilishaji

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Salaam,

Hivi sasa, imekuwa kama desturi katika maeneo ya Uswahilini ndani ya jiji la Dar es Salaam, ambapo baadhi ya wagombea huwalipa wanawake na vikundi vya ngoma ili waje kucheza kiholela na kuvua utu wao, kwa lengo la kuvutia umati na kupata wafuasi wengi.

Wanawake hawa wanapomsindikiza mgombea, hucheza kwa namna isiyofaa, wakionyesha sehemu za siri, na baada ya shughuli, mgombea huwachukua kuwapelekea kwenye vinywaji. Hali hii inaonyesha jinsi ambavyo wagombea wameacha kuzingatia sera bora na kujikita katika kutumia vikundi vya burudani ili kujipatia umaarufu.

Ni wakati jamii iamke, kwani kukubaliana na hali hii kutaendeleza mwenendo huu wa kutumiwa kirahisi.
 
..vyama vya siasa hutumia wasanii kulingana na uwezo wa KIFEDHA wa chama husika.

..Ccm wanapokea BILLION 3.2 kila mwezi hivyo hutumia wasanii wakubwa na maarufu nchini.

..tusilaumu wasanii wadogo wadogo wanaotumika na vyama vya upinzani.

..hiyo ni nafasi ya kuonekana, na huenda Ccm wakazipenda kazi zao, na hivyo kuwatumia kwa malipo makubwa siku za mbeleni.
 
Ccm wanapokea BILLION 3.2 kila mwezi hivyo hutumia wasanii wakubwa na maarufu nchini.
Aiseee, nadhani ruzuku ingekua inatolewa kwa vyama vidogo ili vijiendeshe au ingeangalia proportionality ya namba ya wanachama sio viti vya uwakilishi.

Sasa wachukue 3 B bado za ufisadi na miradi lukuki ya umma waliyohodhi kutoka enzi za chama kimoja.

Hata USA nimeshangaa sana how money buys democracy, yaani hauna pesa huwezi endesha kampeni yoyote.
 
Bora wanaowachezesha vigoma kuliko wale "wanaowachapa" kabisa.
 
Back
Top Bottom