Hali ni mbaya tumwombee Lunyamila anapumulia mashine mwananyamala

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,277
Reaction score
8,860
WINGA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Edibily Lunyamila leo hii asubuhi amekimbizwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kusumbuliwa na kifua na sasa anapumua kwa msaada wa mashine.


Mtandao huu ulifanikiwa kufika hospitalini hapo muda mfupi baada ya winga huyo kukimbizwa hospitalini hapo baada ya kuzidiwa tangu jana usiku akiwa nyumbani kwake Mbezi jijini Dar es Salaam.



Shaffihdauda.com imemshuhudia Lunyamila akiwa amelala kitandani katika wodi ya wanaume namba 5 kitanda namba 16 katika hospitali hiyo ya rufaa ya Kinondoni.





Daktari Madirisha Pascal anayemuhudumia winga huyo wa zamani, Lunyamila anasumbuliwa na tatizo la kifua ambalo linamfanya ashindwe kupumua vizuri.



“Kama mnavyomuona anapumua kwa msaada wa mashine na bado tunaendelea kumfanyia uchunguzi ili kubaini nini kinachomsumbua zaidi,” alisema Pascal.



Mmoja wa ndugu wa Lunyamila, Lameck John alisema kwamba, mchezaji huyo wa zamani alianza kujisikia vibaya jana Jumapili na leo asubuhi hali yake ilibadilika ndipo walipomkimbiza hospitali.




Lunyamila alivyokuwa enzi anaichezea Yanga..

“Alianza kulalamika hawezi kupumua na kifua kinamsumbua pia mbavu zilikuwa zikimuuma, baada ya majibu ya vipimo tutajua kinachomsumbua zaidi,” alisema Lameck.


Kutokana na hali iliyoonekana hospitalini hapo, Lunyamila anahitaji huduma ya haraka ili kuweza kuokoa uhai wake kwani anapumulia mashine akiwa katika sehemu yenye joto kali hivyo anapambana na vitu vingi kwa wakati mmoja.Taarifa za kiuchunguzi zilizofanywa na mwandishi wetu zimebaini Lunyamila anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo.


''Nilikuja jana hospitali ya mwananyaala ikagundulika moyo wangu umekuwa mkubwa,hivi sasa naenda muhimbili kwa ajili ya vipimo zaidi nikifika na kukutana na daktari nitakujulisha ''ilipofika mchana wa leo mwandishi alipokea simu kutoka kwa Lunyamila akimwambia ameambiwa arejee tena hospitali ya Mwananyamala.
 
Apone haraka lakini viongozi wa.Yanga na Serikali kupitia(Wizara ya Michezo,Habari na Utamaduni). Wamsaidie mchezaji huyo

Thamani ya mtu isiwe pale anapotumika tu.
Anapoumwa anatelekezwa namna hii.

"""Mungu ni MwemA"""
 

...Mungu Aponye haraka.
 
Wapi wapenda soka. Inatakiwa tuoneshe mapenzi yetu ya mpira kwa ndugu yetu lunyamila.
 

 
Get-Well Soon Jembe langu,Winga Teleza.

Hapo Beki 2 anakaba Kassongo Athuman.
4 na 5 wanamaliza Mustafa Hoza na George Masatu,

Winga teleza wako alikua hapiti kwenye huu ukuta. !!
 
Daah....enzi za Lunyamila, Sanifu Lazaro"Tingisha", Said Mwamba Kizota, Athuman China na Issa Athuman yanga ilikuwa inatisha. Get well soon Edibily.
1. Mohammed Mwameja
2. Kassongo Athuman
3. Deo Mkuki
4. Mustafa Joza
5. George Masatu
6. Hussein Marshall
7. Abdul Mashine
8. Ramadhan Lenny
9. Nteze John
10. Malota Soma
11. Dua Said
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…