Hali si shwari Mabibo Hostel - UDSM

Mngendalyasota

Senior Member
Joined
Jan 22, 2011
Posts
171
Reaction score
48
WanaJF,
Kwa siku ya nne (4) hostel za Mabibo hazijafanyiwa usafi na watoa huduma wa kampuni mojawapo iliyoingia mkataba na chuo kikuu cha Dar es Salaam kufanya hivyo.Taarifa zilizozagaa ni kwamba wafanyakazi hao (vibarua) wapo kwenye mgomo dhidi ya mwajiri wao wakiwa na madai mbalimbali mojawapo likiwa la kutokulipwa mshahara wao wa Januari hadi sasa. Sasa kutokana na hali hiyo hali ya corridor na vyoo ni mbaya sana. Kuanzia jana wanachuo walianza kujimobilize na kutaka waonane na uongozi wa chuo juu ya mstakabali wa afya zao.
 
Mmh tartibu.. Manake wakuu wetu busara hamna wasije Sema wametumwa name Chadema
 
na mabibo kulivyo na shida ya maji.. na mnavyokaa wengi.. i can imagine hali ipoje
 
Hii Taarifa ingependeza zaidi jukwaa la Habari Mchanganyiko, By the Way Poleni sana,inabidi Mchukue hatua Mapema Maana Viongozi wetu kwa sasa ni utamaduni Wao kua Kuwajibika ni mpaka Washinikizwe ,Suala la Afya si la Mzaha hata Kidogo.
 
Usomi ni kufanya vitu kwa vitendo, acheni utoto. Fanyeni usafi. Tatizo lenu ubishoo mwingi ukizingatia ishu za pale block G
 
Mhhh! Ni hatari maana wanalala wengi sana katika room moja approximately eight students angalau Block F. Mishahara yao nimidogo na pia wanafanya kazi ktk mazingira magumu xana. Wapeni mpunga wao japo ni kidogo warejee kazini.
 
wale ni wasomi mkuu hawawezi kufagia.

Usomi wao utakuwa hauna maana wakishindwa kutatua tatizo hili japo kwa muda wakisubiri hatma yake. Wajikusanye dk 15 wafanye usafi, ni kitu kinawezekana mbona, si wana viongozi wao!!!?
 
Pamoja na kujimobilize vijana wa mabibo ni watu wazima wanaoweza kufanya usafi wa maeneo yao kwa kupanga ratiba zao mpaka tatizo litakapotatuliwa.
 
Usomi ni kufanya vitu kwa vitendo, acheni utoto. Fanyeni usafi. Tatizo lenu ubishoo mwingi ukizingatia ishu za pale block G

Hee..na wewe unajua kuwa kuna Block G pale chini ya tank ?
 
Mnaonaje mkijitolea japo kwa siku mbili kufanya usafi ili muwe salama kutoka kwa magonjwa hatarishi!

hahaha! Waanze tu na vipedo vyao na makeup usoni washike ufyagio wa chooni pyaaa ! Pyaaa!! Ni balaaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…