Hali tete: Suluhisho la synovial fluid au ukosefu wa ute kwenye miguu

Hali tete: Suluhisho la synovial fluid au ukosefu wa ute kwenye miguu

kakamgeni

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2018
Posts
241
Reaction score
201
Habari za jioni ndugu zangu wapendwa wa mtandao huu wa JF kupitia Jukwaa hili mahsusi la Jamii Health. Naamini tuko hapa kwa ajili ya kuelimishana na kuongeza ufahamu wa mambo mbalimbali kwenye vichwa vyetu - Yote ni katika kukabiliana na changamoto za kila siku za kimaisha. basi bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye kile kilichonileta hapa nikihitaji ushauri mzuri kutoka kwenU utakaoweza kuleta matokeo chanya.

Kwa ufupi ni kwamba, mama yangu mzazi anasumbuliwa na tatizo la kiafya ambalo kitaalamu linafahamika kama SYNOVIAL FLUID au KUPUNGUKIWA NA UTE KWENYE MAUNGIO YA MAGOTI. Hadi Sasa ameshafanya vipimo vingi ikiwemo cha MRI Scan ambacho kilimtaka afanyiwe operesheni ya miguu yote miwili, hali iliyopelekea kumnyima raha hasa ukizingatia yupo above 50+. Sasa kuna mzee m1 jirani yetu alitoa ushuhuda kwamba aliwahi kuumwa na kufikia hatua kama yake.

Akasema kwamba kuna shirika moja hapa mjini linaitwa WEST INTERNATIONAL walimuagizia virutubisho kutoka Ujerumani vinavyoitwa EDGE ambavyo vilimgharimu takribu Tzs 1.2M za kitanzania hadi kumfikia na hadi sasa anaendelea vizuri. Kitu kilichonipa wasiwasi ni kwamba nilipojaribu kumuambia anielekeze ofisi zao alidai kwamba ni muda mrefu umepita wamehama na hana mawasiliano yao ila kama tunahitaji anaweza akafanya namna akatuletea kwani kuna package moja imepaki. Binafsi sikulihafiki hilo ndio kupelekea hadi kuja hapa kuomba ushauri kutoka kwenu.

kwa yeyote anayefahamu dawa, tiba, au virutubisho vitakavyoweza kusaidia kupona hili tatizo basi asisite kunishauri - kwani waswahili wanakwambia ugonjwa usikie kwa mwenzako na ombea usikufike. Nina imani kubwa ya kupata ufumbuzi kupitia jukwaa hili kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu. Niwatakie Jioni Njema Wote.

NAWASILISHA
 
Pole sana kwa mama mkuu, tiba nyingi ya magonjwa ipo katika vyakula vyetu hivi kama akizingatia vizuri unaweza ukasahau hbr ya dawa

Some foods are very good for your joints, such as:

Dark, leafy vegetables. ( cabbage, spinach)

Omega-3 fatty acids (found in salmon, mackerel, and flaxseeds)

Anti-inflammatory foods that have curcumin in them (a compound found in turmeric)

High antioxidant foods (onions, garlic, green tea, and berries)

Nuts and seeds.
 
Pole sana kwa mama mkuu, tiba nyingi ya magonjwa ipo katika vyakula vyetu hivi kama akizingatia vizuri unaweza ukasahau hbr ya dawa

Some foods are very good for your joints, such as...
Shukrani Sana Kwa Ushauri Wako Mkuu. Hakika Tutaufanyia Kazi
 
Shukrani Sana Kwa Ushauri Wako Mkuu. Hakika Tutaufanyia Kazi
Mkuu fuata ushauri wa mkuu aliyekupa, ikisihindikana nione mimi kwa wakati wako ili nipate kumtibia mama yako mzazi kwa upungufu wa ute kwenye Magoti.

Ushauri wangu musije mukampeleka hospitali akafanyiwe operesheni kwani mukifanya operesheni miguu yake haitaweza tena kupinda na atakuwa anatembea kwa kutumia magongo mutakuwa mumesha mtia kilema cha maisha hawezi tena kurudi hali yake ya kawaida.

Kuna mtu nilimpa ushauri wangu akadharau matokeo yake anatembea kwa bakora mguu mmoja ulipunguwa ute hakutaka kutumia dawa za asili matokeo yake walimuweka chuma katika magoti hakuweza tena mguu kukunja . Na ameshafariki huyo niliye mshauri Mungu amalaze mahali pema.
 
Habari za jioni ndugu zangu wapendwa wa mtandao huu wa JF kupitia Jukwaa hili mahsusi la Jamii Health. Naamini tuko hapa kwa ajili ya kuelimishana na kuongeza ufahamu wa mambo mbalimbali kwenye vichwa vyetu - Yote ni katika kukabiliana na changamoto za kila siku za kimaisha. basi bila kupoteza muda ningependa kwenda moja kwa moja kwenye kile kilichonileta hapa nikihitaji ushauri mzuri kutoka kwenU utakaoweza kuleta matokeo chanya.

Kwa ufupi ni kwamba, mama yangu mzazi anasumbuliwa na tatizo la kiafya ambalo kitaalamu linafahamika kama SYNOVIAL FLUID au KUPUNGUKIWA NA UTE KWENYE MAUNGIO YA MAGOTI. Hadi Sasa ameshafanya vipimo vingi ikiwemo cha MRI Scan ambacho kilimtaka afanyiwe operesheni ya miguu yote miwili, hali iliyopelekea kumnyima raha hasa ukizingatia yupo above 50+. Sasa kuna mzee m1 jirani yetu alitoa ushuhuda kwamba aliwahi kuumwa na kufikia hatua kama yake.

Akasema kwamba kuna shirika moja hapa mjini linaitwa WEST INTERNATIONAL walimuagizia virutubisho kutoka Ujerumani vinavyoitwa EDGE ambavyo vilimgharimu takribu Tzs 1.2M za kitanzania hadi kumfikia na hadi sasa anaendelea vizuri. Kitu kilichonipa wasiwasi ni kwamba nilipojaribu kumuambia anielekeze ofisi zao alidai kwamba ni muda mrefu umepita wamehama na hana mawasiliano yao ila kama tunahitaji anaweza akafanya namna akatuletea kwani kuna package moja imepaki. Binafsi sikulihafiki hilo ndio kupelekea hadi kuja hapa kuomba ushauri kutoka kwenu.

kwa yeyote anayefahamu dawa, tiba, au virutubisho vitakavyoweza kusaidia kupona hili tatizo basi asisite kunishauri - kwani waswahili wanakwambia ugonjwa usikie kwa mwenzako na ombea usikufike. Nina imani kubwa ya kupata ufumbuzi kupitia jukwaa hili kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu. Niwatakie Jioni Njema Wote.

NAWASILISHA
Gombeyehealthcare.
Tunatoa huduma zifuatazo÷>
1. Matatizo ya Mifupa.
2. Matatizo ya Mfumo wa uzazi, kwa jinsia zote.
3. Matatizo ya Mmengonyo wa Chakula.
4. Matatizo yanayo ambatana na mfumo wa damu.
Nikutoe hofu tatizo hilo la mgonjwa litaisha kwani huduma zetu Ni Bora.
Tupigie kwa namba ÷
+255 678 211 747
+ 255 733 482 038
Tunapatikana Dar es salaam ILALA.
 
Back
Top Bottom