KERO Hali ya Barabara Kwa Fundi Baiskeli (Kigamboni) ni mbaya, mkandarasi kaingia mitini, mwezi wa 6 sasa

KERO Hali ya Barabara Kwa Fundi Baiskeli (Kigamboni) ni mbaya, mkandarasi kaingia mitini, mwezi wa 6 sasa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kiga1.jpg
Hali ya Barabara Kwa Fundi Baiskeli (Kigamboni) ni mbaya, huu ni mwezi wa 6 tangu Bango la Mkandarasi liwekwe na hakuna kinachoendelea

JF tunaomba mtusaidie kupaza sauti kwa Serikali ya Kigamboni kuhusu changamoto ya barabara, kwa kweli ni mbovu sana hasa maeneo ya Kwa Fundi Baiskeli.
Kiga2.jpg

Kiga.jpg
Tangu zile mvua za Mwaka jana (2023) hadi leo hii (Septemba 2024) barabara zimeharibika na hazijarekebishwa vizuri, walipoona Wananchi tumelalamika sana wakaamua kuja kufunika mashimo kama wanavyofanya siku za nyuma.

Mvua zikinyesha baada ya hapo hayo mashimo waliyoyafunika yanarejea kama awali na wakati mwingine yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Kinachokera zaidi wameweka bango la Mkandarasi kuwa wanatengeneza Barabara tangu Aprili 2024 ila mpaka kufika leo hii, hiyo barabara inazidi kukatika na hakuna kinachoendelea.

Soma Pia: Mkandarasi wa barabara ya Majichumvi-Migombani anatutesa kwa zaidi ya Mwezi sasa


Barabara hiyo ina beba magari mazito ya mchanga, ni changamoto kwakweli na hapo bado mvua hazijaanza, zikianza hali ndio inaweza kuwa mbaya zaidi.

Watumiaji wote ikiwemo Bodaboda na watembea kwa miguu wote tunateseka kwa kiasi kikubwa sana. Serikali iangalie kinachoendelea huku, kama hilo bango la Mkandarasi limeweka kama pambo waje walitoe tu.
 
Serekali haina hela, toka wamebadikisha malipo kutoka kwa taasisi husika na kupeleka Hazina kwa Mgulu Mchemba
 
Hali ya Barabara Kwa Fundi Baiskeli (Kigamboni) ni mbaya, huu ni mwezi wa 6 tangu Bango la Mkandarasi liwekwe na hakuna kinachoendele...
Ubaya hiyo barabara haina destination ndomana haitiliwi maanani badala yake inatengenezwa kisiasa tu kwa kupitisha bull dozer

Pia laiti kipande cha kwa fund baskel Hadi mikwambe kungekuwa kuna foleni hiyo ingekuwa inatumika kama mchepuko/mbadala hivyo ingekuwa rahisi kuitengeneza
 
Sasa Fundi baiskeli barabara yanini?
 
Back
Top Bottom