Hali ya umeme yawa ya matumaini baada ya juhudi za Serikali pamoja na mvua kuanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini

Hali ya umeme yawa ya matumaini baada ya juhudi za Serikali pamoja na mvua kuanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu kwa Sasa Hali ya umeme inarejea katika Hali yake ya kawaida,kwa Sasa shughuli za kiuchumi zinazotegemea umeme zinakwenda vyema, Mioyo ya wananchi wajasiriamali na wafanyabiashara imeanza kuwa na Tabasamu na matumaini ya kufanya kazi muda wote,Taa ya Matumaini inawaka mioyoni mwa watu Sasa, Giza linazidi kusogezwa mbali, mitaa inazidi kuwa na mwanga na kuchangamka muda wote, sauti za manung'uniko ya umeme zinapungua na Kuisha.

Sasa Ni pongezi kwa serikali ya mh Rais Wetu mpendwa Dr Samia kwa juhudi zake kubwa za kukabiliana na tatizo hili pamoja Na shukurani kwa Mwenyezi Mungu kwa kutushushia Neema Na Baraka za Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mengi, ambapo hata hapa napoandika mvua kubwa inaendelea kunyesha huku niliko mkoani kwangu. Hakika serikali yetu imepambana,imejitahidi kwa nguvu zake zote, kwa nyenzo zote katika wakati wote ambao tulikuwa tunapitia katika kipindi Cha ukame wa mvua kulikopelekea kupungua kwa kina Cha maji katika mabwawa yetu ya kuzalisha umeme.

Hongera kwetu watanzania kwa mioyo yetu ya Subira uvumilivu na usikivu kwa serikali yetu kwa kipindi chote Cha changamoto hii ya umeme,kwa namna ambavyo tuliungana na kuielewa serikali yetu juu ya chanzo Cha changamoto hiyo ya umeme iliyokuwa imetokana na ukame mkubwa uliokuwa umeikumba nchi yetu.

Hata hivyo Inawezekana Kuna maeneo kukawa na kukatika kwa muda mfupi kwa umeme Jambo ambalo naamini haiwezi ikawa Kama awali,hivyo Tuwe wenye Subira na uvumilivu Kama awali huku tukiendelea kuiamini serikali yetu, maana Tumeona namna inavyo pambana pamoja na juhudi zake katika katika kukabiliana na changamoto ya aina yoyote inayojitokeza mbele yetu Kama Taifa.

Watanzania Hatuna budi Kuendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa upendo wake kwetu watanzania kwa kutupatia Baraka na Neema ya mvua katika kipindi hiki, zitakazo saidia kumaliza changamoto hii ya umeme,Hakika Mwenyezi Mungu anatupenda Sana watanzania, Tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu aendelee kulilinda Taifa letu na Wala Tusikubali mtu yeyote akatugawa kwa misingi ya udini,ukabila au ukanda. Tuwe wamoja na Tumuunge mkono Rais wetu mpendwa Dr Mama Samia Suluhu Hassan na serikali yake katika kututumikia watanzania.

Kazi iendeleee,mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
 
Acha utoto dogo, mvua sio jitihada za serikali, bali ni kudra za mwenyezi Mungu. Hata hayo maji mnayosema yamepatikana kwa 100% hapa mjini sio kweli. Yanapatikana bado kwa shida hata kama mgao umepungua, lakini ni huduma isiyoridhisha.
 
Acha utoto dogo, mvua sio jitihada za serikali, bali ni kudra za mwenyezi Mungu. Hata hayo maji mnayosema yamepatikana kwa 100% hapa mjini sio kweli. Yanapatikana bado kwa shida hata kama mgao umepungua, lakini ni huduma isiyoridhisha.
Kwanza nakushukuru Tindo kwa kukubali kuwa mgao umepungua,pili naomba nisema tena kuwa nimeipongeza serikali kwa juhudi zake katika kipindi chote Cha ukame,lakini pia kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia Neema ya mvua nchini.

Mwisho Asante kwa mchango wake
 
We mpuuzi nini watu tangu Jana hatujaona kombe la Dunia

USSR
Pole mkuu hata hivyo Hali kwa Sasa Ni ya Matumaini na faraja ukilinganisha na awali ,mgao siyo mjali Sana na naamini halini akwenda kuwa njema Sana siku chache zijazo kutokana na uwingi wa mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali
 
Hongera kwetu watanzania kwa mioyo yetu ya Subira uvumilivu na usikivu kwa serikali yetu kwa kipindi chote Cha changamoto hii ya umeme,kwa namna ambavyo tuliungana na kuielewa serikali yetu juu ya chanzo Cha changamoto hiyo ya umeme iliyokuwa imetokana na ukame mkubwa uliokuwa umeikumba nchi yetu.
Sisi sio waskivu Wala wavumilivu na Hilo mnalijua .... Hi shida haiwezi kuondoka Hadi muwe na akili na tunatarajia Hali Kama hii na zaidi kujitokeza Tena na Tena.
 
Ifike stage machawa kama hawa tuwe tunawabonda na mawe mpaka wafe. Mtu akishiba wali maharage anakuja kuandika upumbavu.
Hapana mkuu huwezi ukaua wote unaotofautina nao maana mwisho wa siku utakufa kwa msongo wa mawazo baada ya kugundua kuwa hata uliokuwa unawaamini nao hawakuamini Wala kukuunga mkono wakiwa pembeni, hivyo tuishi kwa kuvumiliana na kuheshimiana
 
Sisi sio waskivu Wala wavumilivu na Hilo mnalijua .... Hi shida haiwezi kuondoka Hadi muwe na akili na tunatarajia Hali Kama hii na zaidi kujitokeza Tena na Tena.
Hapana naamini Hali Kama hii haiwezi kujitokeza tena maana naamini serikali yetu utaweka mipango na mikakati ya kusaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika pamoja na maji ikiwa kutajitokeza Hali ya ukame.tuiamini serikali yetu na kuiunga mkono
 
Kwanza nakushukuru Tindo kwa kukubali kuwa mgao umepungua,pili naomba nisema tena kuwa nimeipongeza serikali kwa juhudi zake katika kipindi chote Cha ukame,lakini pia kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia Neema ya mvua nchini.

Mwisho Asante kwa mchango wake

Kwenye umeme tatizo bado lipo, jitihada za serikali ni bure tu. Mvua tuishukuru kwa mazingira lakini sio umeme.
 
Hapana mkuu huwezi ukaua wote unaotofautina nao maana mwisho wa siku utakufa kwa msongo wa mawazo baada ya kugundua kuwa hata uliokuwa unawaamini nao hawakuamini Wala kukuunga mkono wakiwa pembeni, hivyo tuishi kwa kuvumiliana na kuheshimiana

Mbondwe na mawe tu mfe, uchawa unazid hata ukiambiwa ushikwe makalio hukatai wewe
 
Kwenye umeme tatizo bado lipo, jitihada za serikali ni bure tu. Mvua tuishukuru kwa mazingira lakini sio umeme.
Umeme niliko Hali Ni njema Sana na ya kuleta matumaini.Hata huko uliko amini kuwa hali itatengemaa muda siyo mrefu hasa wakati huu ambao mvua zinaendelea kunyesha
 
Hapana naamini Hali Kama hii haiwezi kujitokeza tena maana naamini serikali yetu utaweka mipango na mikakati ya kusaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika pamoja na maji ikiwa kutajitokeza Hali ya ukame.tuiamini serikali yetu na kuiunga mkono
FB_IMG_16533992434679217.jpg

Mnalazimisha tuamini uongo😂
 
Ndugu zangu kwa Sasa Hali ya umeme inarejea katika Hali yake ya kawaida,kwa Sasa shughuli za kiuchumi zinazotegemea umeme zinakwenda vyema, Mioyo ya wananchi wajasiriamali na wafanyabiashara imeanza kuwa
na Tabasamu na matumaini ya kufanya kazi muda wote,Taa ya Matumaini inawaka mioyoni mwa watu Sasa, Giza linazidi kusogezwa mbali,mitaa inazidi kuwa na mwanga na kuchangamka muda wote, sauti za manung'uniko ya umeme zinapungua na Kuisha.
Unaota umejenga kasiri hewani
 
Back
Top Bottom