Halima Bulembo: Mikopo ya kausha damu inawakausha kwelikweli wanawake na kuwadhalilisha. Asema ukikopa elfu 50 unalipa jumla 85

Halima Bulembo: Mikopo ya kausha damu inawakausha kwelikweli wanawake na kuwadhalilisha. Asema ukikopa elfu 50 unalipa jumla 85

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Halima Bulembo amesema mikopo ya kausha damu pamoja na urahisi wake wake wa kupatikana ina gharama kubwa. Akitolea mfano, amesema mtu akikopa 50,000 anakatwa 5,000 ya fomu, 5,000 nauli ya mkaguzi kuja kukagua mali zako na marejesho ya jumla ya 75,000 hivyo jumla kufanya matumizi ya 85,000 kwenye mkopo.

Akiongea na wanawake wa Kigamboni, amesema mikopo hiyo inawakausha na kuwafedhehesha. Bulembo amesema kila siku wahusika wanatakiwa kupeleka 2000.

Bulembo amewataka wanawake wakakope kwenye mikopo ya halmashauri kwani ipo na inatolewa. Halima amesema kuanzia sasa, wahusika wakitaka kutoa mikopo wafike kwa Mkurugenzi ikapitishiwe huko ikithibitika ina namna nzuri na bora kwa kina mama japo Bulembo amesema asingependa iendelee kabisa.

Kwa msaada wa Mwananchi
 
Analalamika kana kwamba hao wakopeshaji wametoka Jehanamu vile! Kumbe wamesajiliwa kihalali kabisa na mamlaka husika! Na wanalipa kodi serikalini.

Angesema serikali iangalie namna ya kupunguza riba za kwenye mabenki na taasisi nyingine za kifedha, ningemuelewa.

Maana hao kausha damu wengi wao nao wanakopa fedha kwenye mabenki kwa riba kubwa, na kuja kuzizungusha kwa hao wakopaji wadogo! Hivyo lazima na wenyewe wafidie kwa wakopeshaji wao, ili na wenyewe wapate faida.

Na kuhusu mikopo ya Halmashauri, kimsingi imejaa urasimu kupitiliza. Kuna kujuana kwingi, inatolewa kimya kimya! Kwa hali hiyo, watu wanaona bora wakaumie tu kwa hao kausha damu.
 
Analalamika kana kwamba hao wakopeshaji wametoka Jehanamu vile! Kumbe wamesajiliwa kihalali kabisa na mamlaka husika! Na wanalipa kodi serikalini.

Angesema serikali iangalie namna ya kupunguza riba za kwenye mabenki na taasisi nyingine za kifedha, ningemuelewa.

Maana hao kausha damu wengi wao nao wanakopa fedha kwenye mabenki kwa riba kubwa, na kuja kuzizungusha kwa hao wakopaji wadogo! Hivyo lazima na wenyewe wafidie kwa wakopeshaji wao, ili na wenyewe wapate faida.

Na kuhusu mikopo ya Halmashauri, kimsingi imejaa urasimu kupitiliza. Kuna kujuana kwingi, inatolewa kimya kimya! Kwa hali hiyo, watu wanaona bora wakaumie tu kwa hao kausha damu.
Pia hiyo mikopo ya halmashauri, Rais si alisema isitishwe watu wakakope benki sababu ya ubadhilifu na urasimu unaofanyika.
 
Back
Top Bottom