Halima Mdee kwa uchungu mbele ya Rais amzungumzia Dkt. Faustine Ndugulile, "Hakuwa mnafiki, alipata ajali kadhaa za kisiasa kwasababu ya kweli yake"

Halima Mdee kwa uchungu mbele ya Rais amzungumzia Dkt. Faustine Ndugulile, "Hakuwa mnafiki, alipata ajali kadhaa za kisiasa kwasababu ya kweli yake"

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwakilishi wa wabunge wachache bungeni, Halima Mdee, amesema Dk Faustine Ndugulile, aliyekuwa mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, alisimama kidete kwa wananchi wake na Taifa, kusema kweli bila kujali gharama.

"Dkt. Faustine Ndugulile alikuwa siyo mnafiki kama akiwa na jambo lake, alikuwa ni aina ya kiongozi ambaye alitumia muda wake mwingi katika kuwawakilisha Wananchi wa Kigamboni lakini kwa kazi zake za Kitaifa, alikuwa anasema kweli tupu pasipo kujali itamgharimu nini"

“Kama jambo ni nyeupe atasema nyeupe, na kama ni bluu atasema bluu, alipambana kwa ajili ya kile alichokiamini, jambo lililomletea changamoto kadhaa, lakini lilimpa heshima kubwa, inawezekana hatukumuelewa kipindi kile, lakini tumekuja kumuelewa. Taifa lilimuamini na kumchagua kuwa mwakilishi wa Tanzania katika WHO Kanda ya Afrika, na akashinda,” amesema Mdee.

Ameongeza kuwa Dk Ndugulile alikuwa mtu wa ‘moto’ aliyepaswa kuigwa na wote, akisisitiza umuhimu wa kuwa na msimamo ili kusaidia kuinua Taifa. “Watu wengi tunakuwa baridi au vuguvugu ambao ni unafiki, lakini yeye alikuwa wa moto,” amesema Mdee.

 
Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA, Halima akishiriki kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Kigambonio na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ukanda wa Afrika Dkt. Faustine Ndugulile, leo tarehe 02 Disemba, 2024 amesema:

"Dkt. Faustine Ndugulile alikuwa siyo mnafiki kama akiwa na jambo lake, alikuwa ni aina ya kiongozi ambaye alitumia muda wake mwingi katika kuwawakilisha Wananchi wa Kigamboni lakini kwa kazi zake za Kitaifa, alikuwa anasema kweli tupu pasipo kujali itamgharimu nini"
Hata yeye siku akifa, watasema sio mnafiki, Wala hawatasema ni Mbunge alieapishwa gereji na Mr Ndugai.

Faustine Kesha lala, mapambio hayasaidii kitu, kubwa tumuombee Dua njema.
 
Back
Top Bottom