Halima Mdee na Wenzake 18 wamejimaliza kisiasa

Halima Mdee na Wenzake 18 wamejimaliza kisiasa

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
HALIMA MDEE NA MWENZAKE 18 WAMEJIMALIZA KISIASA.

Habari za siku za mwisho wa wiki Wajumbe wa JF,

Hakikaki katika kitu ambacho hua naamini kwenye maisha yangu ni kwamba njia ya mkato kwenye maisha huleta mafanikio ya muda na hatimaye baadae kuacha katika matatizo makubwa sana.

Ndugu Halima Mdee na kundi lake la Wanawake 18 ambao wengi wao bado ni wanasiasa vijana miaka 30-45, bila kupima maumivu ya baadae kwenye kesho yao wamejitia kiburi kujimaliza kisiasa pasipo kujali maelekezo ya waliokua viongozi wao. Wanaenda kujimaliza kisiasa mapema ikiwa bado siasa zinawahitaji sana leo na kesho.

NI VIPI KINAMAMA HAWA WANAJIMALIZA KISIASA?

Ikumbukwe kwamba kinamama hawa bado wanahitaji maisha marefu ya kisiasa. Hawataweza kupata umaarufu katika chama chochote kwa sasa na hata baada ya 2025 jambo walikua nao wakiwa CHADEMA.

Waliota ndevu kwa kudhani kwamba wana jasho lako kubwa katika chama hicho wakidhani walikosea hawawezi kuguswa wakasau kua chama hicho kimekuwa taasisi kubwa yenye wanachama na wafuasi wengi nchi nzima.

Mdee na kundi lake wanachoweza kuambulia kwa sasa ni ubunge wao wa kulindana walioahidiwa na Ndungai ambaye hajali katiba ya nchi kwajitamba na vikanuni vyake vya bunge. Baada ya 2025 hawa kinamama hata walihamia CCM kwenda kufanya siasa mpya kwa kugombea kwenye majimbo haitowezekana kwa vile majimbo yote yote bado yapo chini ya CCM, hivyo kumtoa mbunge wa ccm aliyepo kwenye jimbo si rahisi.

Kwenda kugombea viti maalum ndani ya CCM si rahisi kwa maana zile nafasi zinahitaji uzoefu wa ndani ya chama muda mrefu wajumbe wakuzoee.

Wanachoweza kupata zaidi kwa mapenzi ya Rais ajaye ndani ya CCM labda kuu wa Wilaya, Mkoa, Ukatibu tawala au Ukurugenzi na Ubalozi ambapo bado itategemea na mapenzi ya Rais ajaye kupitia CCM kwenye demokrasia ya nchi Maana si wanaccm wote wanafurahia hawa na anayofanya Magufuli.

LABDA WANAWEZA KUHAMIA VYAMA VIINGINE VVYA UPINZANI?

Si rahisi sana kwa kinamama hawa kwenda kupata umaarufu kwenye vyama vipya vya upinzani kama ilivyokua kwa CHADEMA ambacho kiko kwenye Consistency ya Upinzani imara kwa miaka 20 sasa. Hivi vyama viingine vya upinzani bado vinahitaji kujengwa haviwezi kumpa mtu umaarufu wa haraka hivyo.Kwahiyo si rahisi sana kwenda kuwika kwenye vyama vingine vya siasa mapema hivyo, inahitaji kwanza muda kujijenga upya.

Kwa sasa watapambwa na kuchonganishwa sana na wanaccm maana wanatamani CHADEMA ife leo, wanaccm hawawaonei huruma kinamama hawa, nia yao ni kutaka kuona upinzani wa kughushi bungeni ili mambo yao yaendelee hasa kwenye mashinikizo yaliyopo hivi sasa ya jumuiya za kimataifa.

NINI CHA PEKEE WAFANYE ILI WAJINUSURU NA HALI HII?

Mimi kama mwanasiasa mkongwe, mwandishi na mchambuzi wa siasa ndani ya nchi yangu, njia pekee ya kinamama hawa kurudi kwenye siasa ni kuandika barua kwa viongozi wao wa zamani wa CHADEMA wakiwaomba radhi na wajiondoe kwenye nafasi hizi za ubunge wa muda ambao lengo lake ni kuinufaisha serikali ya CCM na Chama chenyewe. Faida ya kufanya hivi ni kubwa kuliko kwenda kuanza maisha mapya kwenye vyama vipya.

Asiogope kua wanachama watakosa imani nao, wao ni wakongwe kwanza ndio wataibua furaha kubwa kwa wanachadema kwa ujasiri wa kuomba radhi maana hakuna asiyekosea.Kwa kufanya hivi maisha yanasonga mbele na nyota zao za kisiasa zitazidi kung'ara zaidi. Kama wewe ni mwanachama ni mwanachama tu haijalishi ukikosea kiasi gani.

Kama hawaamini katika hili wawaulize Mama Sophia Simba wa CCM aliyefukuzwa uanachama CCM na kisha baadaye kuomba radhi na leo hii ni mbunge tena. Watazame kina Nape Nnauye na Makamba maisha yanaendelea na siasa zao zinaendelea haijalishi walikosea kiasi gani.
 
HALIMA MDEE NA MWENZAKE 18 WAMEJIMALIZA KISIASA.


Habari za siku za mwisho wa wiki Wajumbe wa JF!

Hakikaki katika kitu ambacho hua naamini kwenye maisha yangu ni kwamba njia ya mkato kwenye maisha huleta mafanikio ya muda na hatimaye baadae kuacha katika matatizo makubwa sana.

Ndugu Halima Mdee na kundi lake la wanawake 18 ambao wengi wao bado ni wanasiasa vijana miaka 30-45, bila kupima maumivu ya baadae kwenye kesho yao wamejitia kiburi kujimaliza kisiasa pasipo kujali maelekezo ya waliokua viongozi wao. Wanaenda kujimaliza kisiasa mapema ikiwa bado siasa zinawahitaji sana leo na kesho.

NI VIPI KINAMAMA HAWA WANAJIMALIZA KISIASA?
Ikumbukwe kwamba kinamama hawa bado wanahitaji maisha marefu ya kisiasa. Hawataweza kupata umaarufu katika chama chochote kwa sasa na hata baada ya 2025 jambo walikua nao wakiwa CHADEMA. Waliota ndevu kwa kudhani kwamba wana jasho lako kubwa katika chama hicho wakidhani walikosea hawawezi kuguswa wakasau kua chama hicho kimekuwa taasisi kubwa yenye wanachama na wafuasi wengi nchi nzima.

Mdee na kundi lake wanachoweza kuambulia kwa sasa ni ubunge wao wa kulindana walioahidiwa na Ndungai ambaye hajali katiba ya nchi kwajitamba na vikanuni vyake vya bunge. Baada ya 2025 hawa kinamama hata walihamia CCM kwenda kufanya siasa mpya kwa kugombea kwenye majimbo haitowezekana kwa vile majimbo yote yote bado yapo chini ya CCM, hivyo kumtoa mbunge wa ccm aliyepo kwenye jimbo si rahisi. Kwenda kugombea viti maalum ndani ya CCM si rahisi kwa maana zile nafasi zinahitaji uzoefu wa ndani ya chama muda mrefu wajumbe wakuzoee.

Wanachoweza kupata zaidi kwa mapenzi ya Rais ajaye ndani ya CCM labda kuu wa Wilaya,Mkoa,Ukatibu tawala au Ukurugenzi na ubalozi ambapo bado itategemea na mapenzi ya Rais ajaye kupitia ccm kwenye demokrasia ya nchi Maana si wanaccm wote wanafurahia hawa na anayofanya Magufuli.

LABDA WANAWEZA KUHAMIA VYAMA VIINGINE VVYA UPINZANI?
Si rahisi sana kwa kinamama hawa kwenda kupata umaarufu kwenye vyama vipya vya upinzani kama ilivyokua kwa CHADEMA ambacho kiko kwenye Consistency ya Upinzani imara kwa miaka 20 sasa. Hivi vyama viingine vya upinzani bado vinahitaji kujengwa haviwezi kumpa mtu umaarufu wa haraka hivyo.Kwahiyo si rahisi sana kwenda kuwika kwenye vyama vingine vya siasa mapema hivyo, inahitaji kwanza muda kujijenga upya.
Kwa sasa watapambwa na kuchonganishwa sana na wanaccm maana wanatamani CHADEMA ife leo, wanaccm hawawaonei huruma kinamama hawa, nia yao ni kutaka kuona upinzani wa kughushi bungeni ili mambo yao yaendelee hasa kwenye mashinikizo yaliyopo hivi sasa ya jumuiya za kimataifa.


NINI CHA PEKEE WAFANYE ILI WAJINUSURU NA HALI HII?
Mimi kama mwanasiasa mkongwe, mwandishi na mchambuzi wa siasa ndani ya nchi yangu, njia pekee ya kinamama hawa kurudi kwenye siasa ni kuandika barua kwa viongozi wao wa zamani wa CHADEMA wakiwaomba radhi na wajiondoe kwenye nafasi hizi za ubunge wa muda ambao lengo lake ni kuinufaisha serikali ya CCM na Chama chenyewe. Faida ya kufanya hivi ni kubwa kuliko kwenda kuanza maisha mapya kwenye vyama vipya. Asiogope kua wanachama watakosa imani nao, wao ni wakongwe kwanza ndio wataibua furaha kubwa kwa wanachadema kwa ujasiri wa kuomba radhi maana hakuna asiyekosea.Kwa kufanya hivi maisha yanasonga mbele na nyota zao za kisiasa zitazidi kung'ara zaidi. Kama wewe ni mwanachama ni mwanachama tu haijalishi ukikosea kiasi gani.


Kama hawaamini katika hili wawaulize Mama Sophia Simba wa CCM aliyefukuzwa uanachama CCM na kisha baadaye kuomba radhi na leo hii ni mbunge tena. Watazame kina Nape Nnauye na Makamba maisha yanaendelea na siasa zao zinaendelea haijalishi walikosea kiasi gani.
Huu ndo uhalisia lakini sidhani kama akili hii wanayo.
 
Kweli kabisa,,Wameteleza issue ni kuomba msamaha maisha yanaendelea. Wasije wakajichanganya kwa hili.
 
100% naunga mkono!
Wote tunajua walishinda ubunge wa majimbo wakaibiwa hivyo wana hasira. Kwa hiyo wakiomba msamaha bila shaka wanachama wao watawaelewa! Hiyo team kwanza haipaswi kuwa katika viti maalumu. Hao wote ni wabunge wa majimbo. Iweje leo warudi nyuma. Hila za wenyewe zimewadanganya maskini.
Hawakujua Bawacha ingewatupa!
Halima chama bado kinakupenda! Omba msamaha!
Mbona watu wakubwa sana wakina Kinana na Makamba wanaomba msamaha????
 
Sio wote 19 watakaopotea, kuna baadhi wakihamia CCM baada ya huu ubunge watatoboa vizuri tu, mfano Ester Bulaya, Kunti na Matiko. Hii ni kwasababu wananchi kwenye majimbo yao wanaimani nao na wale waliopitishwa kwenye majimbo hayo hawakubaliki.
 
halima mdee na wenzake wameenda ccm sio kwa7bu wanaipenda ccm. ila ni kwaajili ya tamaa ya pesa tu.
Na sababu iliyo wapeleka ccm ndio itakayo amua ni muda gani watakaa ccm.
 
Tatizo watakuwa tayari kuacha pesa waje wapigike mtaani kwa miaka mitano?
 
Namkumbuka aliyewahi kutoka upinzani na kwenda ccm - Shujaa wa Manzese marehemu Lamwai, alipewa hadi ubunge wa kuteuliwa, kipindi kilipoisha ikawa ndiyo mwisho wake Angejua akabaki upinzani labda mambo yangekuwa mazuri (Namuona Mrema aliyeamua kukomaa na TLP yake)
 
Back
Top Bottom