Halima Mdee: Namkubali sana Roma Mkatoliki, sio Alikiba wala sio Diamond

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506


Mbunge wa Kawe Halima Mdee amefunguka na kusema kuwa katika wasanii wa bongo anamkubali zaidi Roma Mkatoliki kuliko Diamond na Alikiba kwa kuwa wawili hao wote ni waimba mapenzi tu pamoja na umaarufu wao na siku zote mapenzi wanayoimba hayasaidii nchi.

“Nampenda Roma Mkatoliki kwasababu anaimba hali halisi, unajua wasanii ni vioo vya jamii sasa inategemea msanii anataka atumike vipi, atumike kibiashara peke yake ama atumike katika kuelimisha jamii mambo yanayoendelea katika nchi yake,” Mdee aliamuambia mtangazaji wa kipindi cha Hot Stage cha Jembe FM, Jay Jay.

“Kwahiyo Roma above all, yaani wasanii wote, si Diamond, si Alikiba wote wanaimba mapenzi, ni wasanii maarufu wanapendwa lakini mwisho wa siku wanaimba mapenzi na mapenzi hayasaidii nchi, kinachosaidia nchi ni wewe kuangalia namna gani unaweza kutumia taalum yako kama kioo cha jamii.

Watu wanakusikiliza ili kuweza kupeleka meseji, sio kupeleka meseji ya uchochezi bali ya uelewa, kucreate awareness kwa wananchi ambao wanawasikiliza wasanii kwa kiasi kikubwa. Kwahiyo kwangu Roma Mkatoliki amekuwa akifanya kazi nzuri kutumia sanaa kama kuburudisha lakini at the same time kuelimisha.”
 

Viva Roma!!!!! Viva Roma!!!!!!!!!
 
Nakubaliana na wewe Halima. Mimi si mshabiki kabisa wa nyimbo za vijana, lakini nyimbo za huyu kijana zina ujumbe mahususi kwa nchi yetu na vizazi vijavyo!
 
Tatizo anataka kila mtu awe wakala wa CHADEMA, diamond na ali kiba wanatafuta pesa na sio harakati za siasa, labda tu wanapohitajiwa kwa kulipwa, yeye anawachukia hao jamaa kwa sababu hawakuwa upande wao kwenye kampeni.
Aache kulazimisha kila mtu kuwa mwanasiasa, mapenzi yaimbwe maana nayo yapo kwenye jamii
 
Dr Mwaka ana dawa ya kutibu ugonjwa wa kukurupuka,dawa hiyo pia itakusaidia kuongeza umakini katika kuelewa topic na content zake. Tafadhali fanya followup.....
 
Mie siipendi kabisa CCM lakini namkubali Diamond. Ulichanganya siasa kwenye kila jambo unaweza ukamchukia hata mtoto wako mwenyewe
 
Kwasababu za kisiasa (na si kuimba mapenzi) hawezi kuwakubali hao wengine wakati walikuwa mstari wa mbele kuwarudisha CCM madarakani mwaka jana..

...yeye katoa sababu yake halafu wewe unaleta ya kwako,amekwambia "mapenzi hayawezi kuisaidia nchi",labda kuongeza mimba zisizotarajiwa!, wewe unaleta habari ya CCM!
 
Bibi anachanganya siasa na entertainment...she's narrow-minded...yeye kila kitu ni siasa tu
Entertainment gani inayobomoa jamii badala ya kujenga? Mdee yuko sahihi kabisa, hao vijana wawili wanasaka pesa sawa ila wabaharibu jamii.
 
Politics is who gets what, when and how. (nmesahamu reference)
 
Hip hop hailipi......japo ina ujumbe mzuriiiii.

Mashabiki wanapendaa nyimbo za mapenzi
 
mbona mkuu unajitoa ufahamu tumia akili yako sio tumbo likuongoze halima hajasema anawachukia diamond, kiba bali alichosema hapendezwi na nyimbo zao yeye anapenda nyimbo za roma sasa wewe porojo zako au ndo nyie magufuli sijui anawaitaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…