Halmashauri bado hazijaanza utekelezaji wa agizo la Rais la kusamehe riba Kodi ya Pango

Halmashauri bado hazijaanza utekelezaji wa agizo la Rais la kusamehe riba Kodi ya Pango

Sir robby

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2022
Posts
2,396
Reaction score
4,080
Mh RAIS alitangaza kuwa Serikali yake imesamehe KODI ya PANGO kwa kuondoa RIBA kwa Wamiliki wa Viwanja wanaodaiwa KODI ya PANGO.

KODI iliyosamehewa ni ile ya ADHABU/RIBA kutokana na Kuchelewa kulipa KODI sahihi ya Kiwanja na Akatoa MUDA wa Miezi 6 Yaani kuanzia July 2022 mpaka Desemba 2022.

WAZIRI mwenye Dhamana Dkt. Mabula aliutangazia Umma juu ya Msamaha huo.Kitu cha Ajabu nimekwenda Ofisi ya Ardhi kutaka kulipa KODI ninazodaiwa nikitarajia nitafaidika na huo MSAMAHA nimeshangaa sana kuwakuta WATENDAJI hawajui kama kuna Huo MSAMAHA wa RIBA walichokifanya ni kunipigia Hesabu pamoja na Riba iliyosamehewa na MH.Rais.Nilipowadadisi zaidi Wakaniambia HAWAJAPATA WARAKA juu ya KUSAMEHE hizo KODI/RIBA

Ushauri kwa WAZIRI wa ARDHI ni Vema Akawatumia huo WARAKA wa MSAMAHA watendaji wake ili AGIZO la Mh. RAIS litekelezwe kinyume chake ni kupuuza AGIZO la Mh. RAIS kwani Wamiliki wengi wa ARDHI wapo tayari kulipa KODI hizo baada ya kuondolewa RIBA

Screenshot_20220812-143346_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom