Halmashauri Kuu ya ACT-Wazalendo imeketi Dar es Salaam

Halmashauri Kuu ya ACT-Wazalendo imeketi Dar es Salaam

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
631
Reaction score
1,577
IMG-20200803-WA0008.jpg

Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha ACT-Wazalendo kinaendele muda huu Hoteli ya Lamada jijini Dar-es-salaam Tanzania.

Leo Halmashari Kuu inapitia na kupeleka majina ya wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar kwa Mkutano Mkuu utakaofanyika Agosti 05, 2020 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Hall.

Aidha leo Agosti 3, 2020 Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto Kabwe amemteua Ndugu Bernard Membe kuwa Mshauri Mkuu wa Chama. Pia amemteua, Wakili Emanuel Mvula kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu.

Tayari viongozi hao wamethibitishwa rasmi na Halmashauri Kuu ya Taifa.

IMG-20200803-WA0015.jpg
IMG-20200803-WA0014.jpg
IMG-20200803-WA0013.jpg
IMG-20200803-WA0011.jpg

Arodia Peter
Afisa Habari wa ACT–Wazalendo
0717414278
 
Msiwe na haraka subirini mamia ya wanachama watakao hamia ACT kutoka chama cha kaskazini.
 
HALMASHAURI KUU YA CHAMA.

Kiongozi wa Chama @zittokabwe
Katibu Mkuu @AdoShaibu
M/Mwenyekiti Bara @SemuDorothy
M/Mwenyekiti Zenj @jumadunihaji

Wakiwa wamemakinika na kazi iliyo mbele yao.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG_20200803_154757_584.jpg
 
Mshauri Mkuu wa Chama cha @ACTwazalendo, akiwapungia mkono Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama. Kwa mbali japo si sana, namuona Kiongozi wa Chama, Ndugu @zittokabwe

Kikao bado kinaendelea.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200803-WA0053.jpg
 
Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha @ACTwazalendo Leo inajadili mapendekezo ya Ilani ya Uchaguzi Mwaka 2020 kutoka Kamati ya Ilani iliyokuwa chini ya Bi MSALIMU kama Mwenyekiti

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG_20200803_165649.jpg
 
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya @ACTwazalendo wakiwa ukumbini wakiendelea na kikako. Hivi sasa wanajadili ilani za Uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano na ya Zanzibar.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200803-WA0052.jpg
 
Pichani, Kiongozi Mkuu wa Chama, Ndugu Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Ndugu Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama, Ndugu Ado Shaibu na M/Mwenyekiti wa Chama Zanzibar, Ndugu Juma Duni Haji wakiendelea na Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama muda huu.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200803-WA0060.jpg
 

Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha ACT-Wazalendo kinaendele muda huu Hoteli ya Lamada jijini Dar-es-salaam Tanzania.

Leo Halmashari Kuu inapitia na kupeleka majina ya wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar kwa Mkutano Mkuu utakaofanyika Agosti 05, 2020 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Hall.

Aidha leo Agosti 3, 2020 Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto Kabwe amemteua Ndugu Bernard Membe kuwa Mshauri Mkuu wa Chama. Pia amemteua, Wakili Emanuel Mvula kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu.

Tayari viongozi hao wamethibitishwa rasmi na Halmashauri Kuu ya Taifa.


Arodia Peter
Afisa Habari wa ACT–Wazalendo
0717414278
Ndugu Juma Said Sanani ambae ni katika waasisi wa ACT kule Zanzibar mmeamua kumchinjia baharini au?
Msiwasahau waasisi wa chama itakuwa hamuwatendei haki. Wamepata tabu sana tangia chama hakina wanachama wamekuwa wavumilivu.
 
Back
Top Bottom