Halmashauri Ya Ubungo yakanusha taarifa za kuuza shule ya Msingi Ubungo NHC

Halmashauri Ya Ubungo yakanusha taarifa za kuuza shule ya Msingi Ubungo NHC

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Baada ya kuwepo kwa sintofahamu ya kuuza kwa Shule ya Msingi Ubungo National Housing hivi karibuni, Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imekanusha uvumi unaoenea mitandaoni kuhusu kuuzwa kwa shule hiyo.

Taarifa hiyo imewataka wazazi kutokuwa na hofu, kwani shule hiyo ipo katika ukarabati mkubwa unaoendelea tangu Julai 11, 2024, kwa lengo la kuboresha miundombinu.

Soma Pia: Taharuki yazuka, Wazazi wajaa Shule ya Msingi Ubungo NHC baada ya taarifa kuwa shule inauzwa

Aidha taairfa hiyo ilidokeza kuwa umati wa wazazi uliokuwepo shuleni hapo ulikuwa ni kwa lengo la kuandaa kikao cha shule ambacho kiliahirishwa kutokana na Mwalimu Mkuu kupata changamoto ya kiafya

================================================

Kumetokea taarifa iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikionyesha wazazi wakikusanyika katika Shule ya Msingi Ubungo National Housing na kueleza kuwa shule hiyo imeuzwa na kwamba wazazi wameambiwa wakawachukue watoto wao wakawatafutie shule.

Kufuatia taharuki hiyo iliyojitokeza, mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo anapenda kuwataarifu wananchi hususan wazazi wenye watoto katika shule hiyo kuwa taarifa hizo si za kweli na zinalenga kuleta taharuki katika jamii.

NHC.jpg

Ukweli ni kwamba;

1. Shule hiyo ipo katika mkakati mkubwa wa ukarabati na ilipangwa kuwa ya mfumo wa Kiingereza. Ukarabati ulianza toka Julai 11, 2024 ambapo unahusisha ujenzi wa madarasa manne ambayo yamefikia katika hatua ya renta.

Mpango huo mkubwa wa ukarabati hauathiri wanafunzi wanaosoma kwa sasa, isipokuwa mkuu wa shule aliitisha kikao cha wazazi jana tarehe Novemba 11, 2024 ili kikao kifanyike leo Novemba 12, 2024 kuwaeleza juu ya mpango huo wa uboreshaji wa shule hiyo. Kikao hicho hakikufanyika kutokana na changamoto za kiafya za mkuu wa shule.

2. Wakati wa ukarabati wa shule, mara nyingi huwa tunakuwa makini sana na watoto. Ikionekana ni ukarabati mkubwa au ujenzi mpya, huwa tunahamisha watoto kwenda shule za karibu na baadaye kurejea. Kwa hiyo, mpango wa kuhamisha watoto ulikuwa bado haujaanza.

NHC 2.jpg

3. Tutafanya kikao na wazazi wenye watoto wanaosoma katika Shule ya Msingi Ubungo NHC ambao ndio wadau wa elimu kwenye ngazi ya msingi ili kupata picha ya pamoja ya mikakati mikubwa ya kuboresha shule hiyo na kukubaliana mfumo mpya wa shule, kwa sababu wazazi wana nafasi ya kutoa maoni yao.
Aidha, tunatoa onyo kwa mtu au kikundi chochote kinachovumisha taarifa zinazoletea taharuki hasa kipindi hiki kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mwisho, tunawakumbusha kuwa kusambaza taarifa za uongo na zisizo sahihi ni kosa kisheria. Unapokutana na habari kama hizo ambazo hazina uhakika ni vyema kuwasiliana na mamlaka husika ili kupata ufafanuzi na taarifa sahihi.
 
Tuipe muda......ni mwalimu mzuri sana tusisahau tu.....kujisahaulishaaaaa
 
English Medium za nini?

Kama tumeamua English Medium ni best channel si tufanye kwa wote?
Ukarabati wa Shule si unafanywa kipindi cha likizo?

Kuna tatizo. Halisemwi?.
 
English Medium za nini?

Kama tumeamua English Medium ni best channel si tufanye kwa wote?
Ukarabati wa Shule si unafanywa kipindi cha likizo?

Kuna tatizo. Halisemwi?.

hizo shule wanazifanya english medium sababu hakuna wateja wa swahili medium. yaani udahili wa darasa la kwanza kwenye swahili medium, umekuwa mdogo sana. ambao hautoshi kuendesha shule.

maeneo ya shule ya msingi Ubungo NHC ilipo ni mjini kabisa, wazawa ni kizazi kilichonunua viwanja mwaka 1970s na 1980s ya mwanzoni.. hicho kizazi kimeshazeeka, hivyo hakizai tena watoto wadogo wa kuanza darasa la kwanza. pia maeneo hayo ni mjini hivyo kodi za wapangaji ni bei juu sana, hivyo watu wapya wanaomudu kupanga maeneo hayo ndio wanaozaa watoto wapya, na sababu wana uwezo kipesa wanataka watoto wao wasome english medium schools na sio swahili medium schools, manispaa wameligundua hilo ndio maana shule za maeneo hayo zimefanywa english medium.


leo hii shule za msingi zote kubwa za serikali zilizopo maeneno ya ubungo shekilango, sinza na mwenge zimegeuzwa english medium. sababu kuu wazawa wameshazeeka na wapangaji wapya wanaopanga zama hizi hawataki watoto wao wasome swahili medium
 
hizo shule wanazifanya english medium sababu hakuna wateja wa swahili medium. yaani udahili wa darasa la kwanza kwenye swahili medium, umekuwa mdogo sana. ambao hautoshi kuendesha shule.

maeneo ya shule ya msingi Ubungo NHC ilipo ni mjini kabisa, wazawa ni kizazi kilichonunua viwanja mwaka 1970s na 1980s ya mwanzoni.. hicho kizazi kimeshazeeka, hivyo hakizai tena watoto wadogo wa kuanza darasa la kwanza. pia maeneo hayo ni mjini hivyo kodi za wapangaji ni bei juu sana, hivyo watu wapya wanaomudu kupanga maeneo hayo ndio wanaozaa watoto wapya, na sababu wana uwezo kipesa wanataka watoto wao wasome english medium schools na sio swahili medium schools, manispaa wameligundua hilo ndio maana shule za maeneo hayo zimefanywa english medium.


leo hii shule za msingi zote kubwa za serikali zilizopo maeneno ya ubungo shekilango, sinza na mwenge zimegeuzwa english medium. sababu kuu wazawa wameshazeeka na wapangaji hawataki swahili medium
Si wapeleke watoto wao huko English medium?
 
Wakuu,

Baada ya kuwepo kwa sintofahamu ya kuuza kwa Shule ya Msingi Ubungo National Housing hivi karibuni, Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imekanusha uvumi unaoenea mitandaoni kuhusu kuuzwa kwa shule hiyo.

Taarifa hiyo imewataka wazazi kutokuwa na hofu, kwani shule hiyo ipo katika ukarabati mkubwa unaoendelea tangu Julai 11, 2024, kwa lengo la kuboresha miundombinu.

Soma pia: Taharuki yazuka, Wazazi wajaa Shule ya Msingi Ubungo NHC baada ya taarifa kuwa shule inauzwa

Aidha taairfa hiyo ilidokeza kuwa umati wa wazazi uliokuwepo shuleni hapo ulikuwa ni kwa lengo la kuandaa kikao cha shule ambacho kiliahirishwa kutokana na Mwalimu Mkuu kupata changamoto ya kiafya

================================================

Kumetokea taarifa iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikionyesha wazazi wakikusanyika katika Shule ya Msingi Ubungo National Housing na kueleza kuwa shule hiyo imeuzwa na kwamba wazazi wameambiwa wakawachukue watoto wao wakawatafutie shule.

Kufuatia taharuki hiyo iliyojitokeza, mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo anapenda kuwataarifu wananchi hususan wazazi wenye watoto katika shule hiyo kuwa taarifa hizo si za kweli na zinalenga kuleta taharuki katika jamii.


Ukweli ni kwamba;

1. Shule hiyo ipo katika mkakati mkubwa wa ukarabati na ilipangwa kuwa ya mfumo wa Kiingereza. Ukarabati ulianza toka Julai 11, 2024 ambapo unahusisha ujenzi wa madarasa manne ambayo yamefikia katika hatua ya renta.

Mpango huo mkubwa wa ukarabati hauathiri wanafunzi wanaosoma kwa sasa, isipokuwa mkuu wa shule aliitisha kikao cha wazazi jana tarehe Novemba 11, 2024 ili kikao kifanyike leo Novemba 12, 2024 kuwaeleza juu ya mpango huo wa uboreshaji wa shule hiyo. Kikao hicho hakikufanyika kutokana na changamoto za kiafya za mkuu wa shule.

2. Wakati wa ukarabati wa shule, mara nyingi huwa tunakuwa makini sana na watoto. Ikionekana ni ukarabati mkubwa au ujenzi mpya, huwa tunahamisha watoto kwenda shule za karibu na baadaye kurejea. Kwa hiyo, mpango wa kuhamisha watoto ulikuwa bado haujaanza.


3. Tutafanya kikao na wazazi wenye watoto wanaosoma katika Shule ya Msingi Ubungo NHC ambao ndio wadau wa elimu kwenye ngazi ya msingi ili kupata picha ya pamoja ya mikakati mikubwa ya kuboresha shule hiyo na kukubaliana mfumo mpya wa shule, kwa sababu wazazi wana nafasi ya kutoa maoni yao.
Aidha, tunatoa onyo kwa mtu au kikundi chochote kinachovumisha taarifa zinazoletea taharuki hasa kipindi hiki kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mwisho, tunawakumbusha kuwa kusambaza taarifa za uongo na zisizo sahihi ni kosa kisheria. Unapokutana na habari kama hizo ambazo hazina uhakika ni vyema kuwasiliana na mamlaka husika ili kupata ufafanuzi na taarifa sahihi.
Mzushi mkubwa hapa JF ni Waufukweni , anza na huyo
 
Shule haina waalimu? Kwanini hawakuwepo wakati wa mkusqnyiko ili kutoa ufafanuzi huu?

Kuna mtu anaonekana kwenye video akielezea hili la shule kuuzwa, je! Alitoa wapi taarifa hizo na ni nani alimtuma?

Mpaka ukarabati unaanza kimyakimya bila wazazi kufahamishwa, kamati ya shule ilikuwa wapi na kwanini taarifa haikutolewa mapema?

Wanasema mkusqnyiko huo ni kwaajili ya kupanga kikao, huo ndio utaratibu wao wa siku zote kwamba wawaite wazazi ili kupanga tarehe ya kikao? Kama sio, hili la sasa limetoka wapi na kwa muktadha upi?

Maswali ni mengi
 
Back
Top Bottom