Hamis Kiiza 'Diego' amwaga wino Simba!

kila mwaka si mnasajili na kuishia nafasi ya 3?..sioni cha ajabu.!!!!
 
kwa hyo wewe hujui dunian pote wachezaji huwa wananunuliwa kutoka katika vilabu tofauti?

Yanga ikinunua ex Simba ni makapi. Simba ikinunua ex Yanga Ni kutoka vilabu tofauti . Leo ndiyo nimelijua hili.
 
Mkuu usiwasahau Amir Maftah, Juma Kaseja na Emmanuel Okwi nao walitoka Yanga na kwenda Simba na walifanya vizuri sana.
Mkuu Maftah hakufanya vizuri akiwa simba, nadhani simba ndo imempoteza maftah kwenye ulimwengu wa soka.
 
Mkuu mbona hasira?football ni fairplay.

Umesoma vizuri sentensi yake lakini mkuu?

Yeye ndiye aliyeanza kuandika lugha ya kejeli ilihali jukwaa hili watu tunaheshimiana pamoja na utofauti wa ushabiki wetu...
 
Ni usajili mzuri. Ni mmaliziaji mzuri endapo atatengenezewa nafasi, sielewi kwa nini yanga walianza kumuweka benchi! Natumai atafanya mambo fresh!
 
Mkuu Maftah hakufanya vizuri akiwa simba, nadhani simba ndo imempoteza maftah kwenye ulimwengu wa soka.

Amir Maftah hakufanya vizuri akiwa Simba??? Maftah yupi huyo!! Ile invincible ya simba naye si alikuwa sehemu ya ukuta kama niko sahihi? au!!
 
Umesoma vizuri sentensi yake lakini mkuu?

Yeye ndiye aliyeanza kuandika lugha ya kejeli ilihali jukwaa hili watu tunaheshimiana pamoja na utofauti wa ushabiki wetu...

Mkuu ubinadam kazi.Humu jamvini usipokua na roho ngumu utaaribu furaha yako.
 
Mnhhhhh,,,,naomba kudeclare interests...mie ni mpenzi wa simba na soon nitakuwa mwanachama wa simba.

Usajili huu naona umeshinikizwa na okwi ili kumpata partner wake...na viongozi wa simba wakiamini kuwa okwi anahitaji msaidizi waliyezoeana kama kiiza...ila tatizo lipo hapo.

Kiiza alivyokuja yanga alijifunza ustaa badala ya kucheza mpira,....analewa sifa tofauti na okwi anayesikia raha kucheza mpira kuliko kusifiwa.

Kiiza atakuwa mzuri iwapo atakubali kufanya kazi ya kucheza mpira na sio kuendekeza sifa za magazetini.

Ni hayo tuu.
 
Amir Maftah hakufanya vizuri akiwa Simba??? Maftah yupi huyo!! Ile invincible ya simba naye si alikuwa sehemu ya ukuta kama niko sahihi? au!!

Uko sahihi kabisa Mkuu.. Na alifunga goli nyingi tu, wakati Simba SC a.k.a Taifa Kubwa ikiingia katika vitabu vya kumbukumbu duniani kwa kumalza ligi bila kupoteza mechi.
 
Kiiza mpira ulishakwisha huyo...

Kama Dan Sserunkuma alishindwa kucheza mpira akiwa Simba, sioni winga yoyote wa Kiganda kwa sasa kufanya maajabu yoyote hapo Msimbazi...

Kiiza ni winger? Sserunkuma alitokea ligi nyingine, alishindwa kubadilika kutokana na mazingira, kiiza ni tofauti, ila pia uwezekano wa kuwa flop upo!
 
Kweli mkuu nilishangaa sana siku nasikia kandambili mnamuacha Kiiza, nimefurahi simba wamemwona labda atatusaidia

Nafurahi kuona kuwa Simba nao wameanza zoazoa ya matakataka ya Yanga kama vile sisi Yanga tulivyozea kuzoa matakataka kutoka Simba.

Hapa equation inakuwa balanced:
Young Africans SC = Simba SC
 
Nafurahi kuona kuwa Simba nao wameanza zoazoa ya matakataka ya Yanga kama vile sisi Yanga tulivyozea kuzoa matakataka kutoka Simba.

Hapa equation inakuwa balanced:
Young Africans SC = Simba SC

Naomba kuweka kumbukumbu sahihi.. "fundi" hamis kiiza a.k.a diego si kapi, maana aliondolewa na maximo, ili jaja aweze pata nafasi.
 
Kama kiiza ni fundi ilikuaje simba wakaacha kumchukua baada ya kuachwa na yanga na badala yake wakakimbilia kumchukua serunkuma
Kama kiiza ni fundi kwa nn alikosa timu ya kuchezea muda wote baada ya kuachwa na yanga
 
Ni kweli, ila mfumo ndo unamtengeza mtu, alikuwa mtu wa magazetini sana sababu mfumo wa yanga ndo unataka hivyo!
Simba hatuna mpira wa magazetini ata-cope tuu!
 
Nafurahi kuona kuwa Simba nao wameanza zoazoa ya matakataka ya Yanga kama vile sisi Yanga tulivyozea kuzoa matakataka kutoka Simba.

Hapa equation inakuwa balanced:
Young Africans SC = Simba SC
Tuwe na shukrani wabongo, leo kweli wamponda Kiiza kisa kaja simba?? Mlimuacha sio kwamba aliwasaliti.
 
Kama kiiza ni fundi ilikuaje simba wakaacha kumchukua baada ya kuachwa na yanga na badala yake wakakimbilia kumchukua serunkuma
Kama kiiza ni fundi kwa nn alikosa timu ya kuchezea muda wote baada ya kuachwa na yanga

Kiiza alishindwa kutua Msimbazi, kwa sababu Simba ilikua ishakamilisha idadi ya wachezaji 5.. Ikumbukwe pia Kiiza alitemwa na Yanga siku chache kabla dirisha la usajili halijafungwa.

Kiiza si kwamba hakupata timu alipoachwa na Yanga.. timu kibao zilimtaka ila hazikua za kaliba yake.. Mf. Mbeya City.. Hakua na haraka, aliamini ligi ikiisha atapata timu ya hadhi yake.

Hamisi Kiiza "Diego" karibu Msimbazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…