Hamisha File lolote toka kwenye simu kwenda kwenye compyuta bila waya

Hamisha File lolote toka kwenye simu kwenda kwenye compyuta bila waya

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
1_20241112_210415_0000.png


Microsoft wameachia feature mpya kwa watumiaji wa windows 10 na windows 11 kuweza kuhamisha files lolote toka kwenye simu kwenda kwenye kompyuta bila waya, Unatumia mfumo wa wireless tu kuweza kuhamisha vitu.

2_20241112_210416_0001.png


Feature hii inaitwa show mobile device in files Explorer inakupa uwezo wa kuona file zako zilizopo kwenye simu na kuonekana kwenye kompyuta kupitia files Explorer na kukupa uwezo wa kuhamisha chochote utafikiri Unatumia USB kumbe ni wireless.

🧿KWENYE SIMU
🛡️ Pakua app ya link to windows app toka play store
🛡️ Ifungue kisha sign na akaunti yako ya Microsoft ambayo Unatumia kwenye kompyuta
🛡️ allow permission zote watakazo kuomba kisha malizia setup.

3_20241112_210416_0002.png


🧿 KWENYE KOMPYUTA
🛡️ Ingia setting kwenye kompyuta yako
🛡️ Tafuta sehemu ilipoandikwa Bluetooth & device
🛡️ Kisha ingia sehemu ya Mobile Device malizia kwa kubonyeza sehemu ya Manage device utagusa sehemu ya ku sign In.
🛡️ Chagua akaunti yako ya Microsoft ambayo ume signed kwenye simu ukimaliza sasa utaona neno "Show mobile device in files Explorer"

4_20241112_210416_0003.png


Utaweza kuweka On baada setup kuwa completed fungua sasa File explorer kwenye kompyuta yako chini ya This PC utaiona simu yako utaweza kuhamisha chochote unachotaka.

KUMBUKA
Mfumo huu unaanzia kwa watumiaji wa simu za android version 10 na kuendelea🙃.
 
Microsoft wamecomplicate sana account yao nina outlook account yao kila wakati nikitaka kuingia ni wrong password au reset password inakwaza sana
 
Yan kabisa wanaita feature mpya wakati watu wanadunda na WiFi transfer kitambo tu.

Xender wanayo hii feature miaka na miaka, na mpaka sasa wamekuja na nyingine Tena. Sasa hapo wanalazimisha watu tu kuwa na Microsoft account wakati ukidownload tu Xender unafanya yote.

Screenshot_20241116-204957.jpg


Now wamejiongeza Tena na hii
Screenshot_20241116-205024.jpg
 
Back
Top Bottom